Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 12/1 kur. 25-27
  • Wahitimu wa Gileadi Watamani Kueneza Habari Njema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wahitimu wa Gileadi Watamani Kueneza Habari Njema
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hotuba Kuu
  • Shule ya Gileadi—Ina Umri wa Miaka 50 na Yaendelea Kufanikiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Wamisionari Zaidi kwa Ajili ya Mavuno ya Duniani Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Wahitimu wa Gileadi Waondoka Wakiwa Wavunaji Wenye Bidii!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Wachochewa Kutumikia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 12/1 kur. 25-27

Wahitimu wa Gileadi Watamani Kueneza Habari Njema

“NI JAMBO la ajabu zaidi tulilopata kuwazia.” Ndivyo Anders na Amalia Groth walivyohisi juu ya mazoezi yao ya mishonari. Wao walionyesha hisia za wahitimu wote 48 wa darasa la 97 la Watchtower Bible School of Gilead wakiongezea hivi: “Mazoezi ya Gileadi yametuchochea na kututayarisha, kwa hiyo tunatamani kwenda kwenye migawo yetu mipya.”

Twaweza kuhisi shangwe hiyo wanafunzi watoapo maelezo juu ya programu ya uhitimu; watu 6,420 walikusanyika Septemba 4, 1994, kwa ajili ya tukio hilo.

“Theodore Jaracz wa Baraza Linaloongoza alifungua programu kwa kusema juu ya kichwa ‘Kufundishwa na Yehova,’” wakasema David Abel na mke wake, Kelli. “Jambo ambalo hatutasahau ni wakati Ndugu Jaracz alisema: ‘Ni lazima tutambue udogo wetu sisi wenyewe kwa kulinganishwa na Yehova,’ naye alitoa kielezi cha jambo hilo kwa somo lenye nguvu lipatikanalo katika Ayubu sura 38 na 39. Ndugu Jaracz alisema kwamba ingawa tumeongeza ujuzi wetu wa Biblia kupitia Shule ya Gileadi, hatujui jibu la kila swali. Ni lazima tuendelee kujifunza Neno la Mungu.”

Sasa Christian na Angele Coffy wakasema: “Tulivutiwa sana na hotuba iliyotolewa na Max Larson yenye kichwa ‘Ni Nini Thamani ya Msingi Mzuri?’ Tulipenda jinsi alivyotufananisha na jengo linalohitaji msingi wenye kina katika ardhi ngumu ili liweze kubaki imara hata linapopatwa na tetemeko la dunia. Kwa kujifunza kwa bidii, twaweza kukuza uhusiano wa karibu zaidi pamoja na Yehova nasi twaweza kutegemeza imani yetu kwa ujuzi wenye kina ili tuweze kubaki imara katika nyakati za magumu.”

“Hotuba ya Milton Henschel, msimamizi wa shule hiyo, yenye kichwa ‘Mashamba ni Meupe kwa Mavuno’ itakumbukwa kwa muda mrefu sana,” wakasema Gary na Lynn Elfers. “Andiko la msingi, Yohana 4:35-38, lilikazia pendeleo ambalo tunalo la kuingia katika shamba ambalo tayari limepandwa na wafanyakazi wa awali. Hili litatuchochea kufanya kazi tukiwa na hisia ya uharaka.” Wakikubaliana na hilo, Jan na Sirpa Vaahtola walionelea: “Ndugu Henschel aliamsha matarajio yetu juu ya kazi ya kuvuna ambayo ingali iko mbele kwa kutoa ripoti ya karibuni zaidi kutoka Mataifa ya Baltiki. Ongezeko katika Estonia lilikuwa asilimia 51, katika Latvia asilimia 106, na katika Lithuania asilimia 51. Ni jambo la kusisimua kama nini! Ndugu huko wanaomba Bwana-Mkubwa apeleke wafanyakazi zaidi. Tulifurahi hasa kusikia hiyo, kwa kuwa mgawo wetu ni kwenda Estonia!”

“Joel Adams alifuata kwa hotuba yenye kichwa ‘Mtumaini Yehova,’” wakumbuka Kevin na Evelyn Cortina. “Alitushauri kwamba tusifikirie kamwe kwamba nyakati nyingine twaweza kumtumaini Yehova na nyakati nyingine tutegemee hekima yetu wenyewe. Katika migawo yetu tutakabili magumu mengi—afya, chakula, lugha, desturi, na kadhalika. Yote hayo yatahitaji kwamba tumtumaini Yehova.”

Kisha akafuatia Gerrit Lösch, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, aliyeongea juu ya kichwa “Endeleeni Kuonyesha Rehema ya Yehova.” Alen na Ann Marie Gokavi wakasema: “Yeye alitaja kwamba ni ishara ya ukomavu wa Kikristo kuwaonyesha rehema wamishonari wenzetu na wale ambao tunawaeleza habari njema. Migawo ya kwenda nchi ya kigeni hutia dhabihu, lakini ikiwa rehema inakosa, basi dhabihu yetu haitakuwa na thamani kubwa.” (Mathayo 9:13) Peter na Fleur Hupston waliongezea hivi: “Ndugu Lösch alisema twapaswa kuwa wenye rehema kwa ndugu na dada zetu pia, tukiwaona kwa upande wa mbele wa darubini, ili makosa yao yawe madogo zaidi badala ya kuwa makubwa zaidi.”

“Jack Redford, mmoja wa wafunzi wa Gileadi, alifuata kwa kichwa ‘Je, Unaweza Kutii Karipio?’” wakumbuka Mickey na Sherry Minsky. “Yeye alitaja kwamba kiburi hufanya iwe vigumu kukubali karipio na kwamba ikiwa sisi ni wenye hisia nyepesi kwa shauri, tutapoteza manufaa zalo. Kisha akatoa madokezo kadhaa juu ya kukubali karipio yanayotegemea Maombolezo 3:27-31.” Charles na Joan Held waliongezea hivi: “Mara nyingi sisi hukosa kuona mapungufu yetu wenyewe; kwa hiyo, ni lazima tuone karipio kuwa njia ya kuona mambo ambayo sisi hatuyaoni. Karipio au shauri kutoka kwa Yehova ni uthibitisho wa upendo wake kwetu.”

“Mfunzi mwingine, Ulysses Glass, alisema juu ya kichwa ‘Pata Hekima Itumikayo Inayoongoza Kwenye Uhai.’ Yeye aliuliza: ‘Mtafanya nini na yale mliyojifunza?’” wakasema Kenneth na Lisbeth Ardkäll. “Kisha akatoa kielezi kinachotegemea Mithali 30:24-26 juu ya mnyama mdogo aitwaye wibari na jinsi Yehova amemwandalia vifaa ili aweze kuishi. Sisi, kwa upande mwingine, si wenye hekima kisilika, kwa hiyo twahitaji kujibidiisha ili kupata hekima. Yehova ametuandalia kila kitu tunachohitaji ili kufanya hivyo. Maadamu tunamkaribia Yehova na kwa kila mmoja kwa upendo, tutatimiza mambo mengi.”

Hotuba Kuu

“Ndugu Karl F. Klein, mshiriki wa Baraza Linaloongoza, alizungumzia kwa uchangamfu Zaburi 19 pamoja nasi katika hotuba yake ‘Kito Miongoni mwa Vito,’” wakasema Jay na Gwen Abraczinskas. “Yeye alikazia uthamini wa kina sana wa mtunga-zaburi Daudi kwa Yehova na jinsi alivyopenda Neno la Mungu.” “Ndugu Klein aligawanya zaburi hiyo katika sehemu tatu,” wakataja Keith na Donna Hornback. “Sehemu 1 (mistari 1-6) yaonyesha uthamini wa Daudi kwa uumbaji wa Mungu, sehemu 2 (mistari 7-10) yaeleza uthamini wake kwa sheria za Mungu, na sehemu 3 (mistari 11-14) yatukumbusha kwamba, kama Daudi, twapaswa kutaka kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Yehova.”

“Tulifurahia lile jambo la kwamba hofu ya Yehova ni muhimu ikiwa tutaepuka mabaya. Jambo hilo hutuongoza kufanya yaliyo safi machoni pake,” wakasema David na Raylene Long. Frank na Vibeke Madsen waliunga mkono jambo hilo. “Maelezo ya Ndugu Klein juu ya jinsi vikumbusha, sheria, na amri za Yehova zilivyo na manufaa yaeleza vizuri kwa ufupi yale tuliyojifunza katika Gileadi,” wao wakasema. “Hilo lilitufanya tuazimie hata zaidi kushikamana na Neno la Mungu wakati ujao na kuliona kama sanduku la hazina la vito.”

Baada ya hotuba kuu, wanafunzi walipokea diploma zao, na migawo yao ya nchi za nje ilitangazwa. Baada ya pumziko la kupata viburudisho, wote walikusanyika tena kwa ajili ya kipindi cha alasiri. Wahitimu walishiriki katika kujibu maswali yaliyoulizwa katika Funzo la Mnara wa Mlinzi lililofupishwa.

“Kisha programu ya wanafunzi ikaja ‘Twazoezwa Kuwa Watangazaji wa Ufalme Duniani Pote,’” wakumbuka Bob na Shannon Lakatos. “Sehemu ya kwanza ya programu hiyo ilishughulikia maono ya wanafunzi katika utumishi wa shambani wakati wa mtaala wao wa miezi mitano. Ilikazia kutumia maswali kwa ustadi katika huduma yetu. Sehemu ya mahoji ilionyesha njia nzuri za kukabili magumu na hali zenye kubadilika za maisha ya mishonari. Maonyesho matatu ya slaidi, ya Kosta Rika, India, na Malawi, yalitupa mwono wa tengenezo la Yehova la ulimwenguni pote.”

“Drama iliyofuata, Uwe wa Kitheokrasi, Si wa Kilimwengu, ilionyesha matokeo mabaya ambayo watu fulani wa ukoo wa kilimwengu wenye kufikiria kivyao waweza kuleta,” wakasema Jesse na Michelle Duncan. “Ilionyesha kwamba ni lazima Wakristo watambue miongozo na mielekezo ya Kitheokrasi kuwa ya lazima na yenye manufaa,” akaongezea Wenzel na Kelly Koula.

Sala na wimbo wa mwisho ulimalizia programu hiyo ya kupendeza. Wahitimu walipoondoka wakitazamia kwenda kwenye migawo yao katika nchi za kigeni 18, mawazo yao yalionyeshwa vema na maelezo ya kuaga ya Tommi na Jael Kauko: “Tunatamani sana kwenda kwenye migawo yetu na kutumia yale ambayo tumejifunza. Tumepokea mengi sana—sasa ni wakati wetu wa kutoa.”

[Picha katika ukurasa wa 26]

Darasa la 97 la Kuhitimu la Watchtower Bible School of Gilead

Katika orodha iliyopo chini, mistari imepewa nambari kuanzia mbele kurudi nyuma, na majina yameorodheshwa kuanzia kushoto kuelekea kulia katika kila mstari.

(1) Hong, J.; Hong, D.; Groth, A.; Cortina, E.; Lakatos, S.; Hornback, D.; Acevedo, L.; Coffy, A. (2) Elfers, L.; Gokavi, A.; Ardkäll, L.; Abraczinskas, G.; Knott, K.; Lizer, T.; Abel, K.; Abel, D. (3) Duncan, M.; Gokavi, A.; Held, J.; Hupston, F.; Lakatos, B.; Long, R.; Minsky, S.; Acevedo, E. (4) Ardkäll, K.; Kauko, J.; Vaahtola, S.; Cortina, K.; Carson, N.; Minsky, M.; Lizer, G.; Koula, K. (5) Duncan, J.; Abraczinskas, J.; Vaahtola, J.; Madsen, F.; Madsen, V.; Long, D.; Carson, C.; Elfers, G. (6) Kauko, T.; Hupston, P.; Held, C.; Groth, A.; Hornback, K.; Koula, W.; Knott, D.; Coffy, C.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki