Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 12/15 uku. 30
  • Je! Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Mwe Wenye Huruma Nyororo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Wazee Wanaosimamia Vema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Thamini Ushikamanifu na Msamaha wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Uangalizi Wenye Upendo Hujenga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 12/15 uku. 30

Je! Wakumbuka?

Je, Umeona matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi kuwa yenye kutumika kwako? Basi mbona usijaribu kumbukumbu lako kwa maswali yafuatayo:

▫ Kwa nini Mashahidi wa Yehova huendelea kutembelea majirani wao?

Mashahidi wa Yehova wenyewe wanataka baraka ya Mungu kupitia Ufalme ulioahidiwa, na kwa sababu wanawapenda majirani wao, wanataka wawe na baraka iyo hiyo. Hivyo, wakifuata kielelezo cha Yesu, wanahisi kushurutishwa na upendo usio na ubinafsi kuwatembelea majirani wao. (Mathayo 6:9, 10; 22:37-39)—8/15, kurasa 8, 9.

▫ Kwa nini itikadi katika mageuzi ni jambo la imani?

Wanasayansi hawajapata kuona migeuko-papale—hata ile inufaishayo—ikitokeza aina mpya za uhai, na huku wanadai kwamba ndivyo aina mpya za uhai zilivyoanza. Wanamageuzi hawajaona uhai ukianza kutoka kwa kitu kisicho na uhai, na huku wanasisitiza kwamba uhai ulianza hivi.—9/1, ukurasa 5.

▫ Twaweza kushindaje kwa njia bora zaidi kuvunjika-moyo kunakotokana na vizuizi katika maisha?

Hata hali yetu iwe nini, tukizingatia akilini mambo tuwezayo kufanya badala ya kuudhika juu ya mambo tusiyoweza kufanya, maisha yataridhisha zaidi, nasi tutapata shangwe katika utumishi wa Mungu. (Zaburi 126:5, 6)—9/1, ukurasa 28.

▫ Ni zipi manufaa za kusamehe?

Kuwasamehe wengine huendeleza uhusiano mzuri. (Waefeso 4:32); haileti tu amani kati yako na wanadamu wenzako bali pia amani ya ndani (Warumi 14:19; Wakolosai 3:13-15); kuwasamehe wengine hufungulia njia dhambi zetu zisamehewe (Mathayo 6:14); pia hutusaidia kukumbuka kwamba sisi wenyewe twahitaji msamaha. (Warumi 3:23)—9/15, ukurasa 7.

▫ Kielelezo cha nabii Amosi chatusaidiaje katika utendaji wetu wa kuhubiri?

Kama Amosi, hatubadili wala kupunguza ujumbe wa Mungu. Badala ya hivyo, kwa utii twautangaza bila kujali itikio la wasikilizaji.—9/15, ukurasa 17.

▫ Ni sifa zipi za Mungu twahitaji kuiga?

Mbili muhimu ni uwezo wa Yehova wa kupanga mambo kitengenezo na furaha yake. (1 Wakorintho 14:33; 1 Timotheo 1:11) Sifa hizo za Mungu zimesawazika hivi kwamba moja yazo haijitokezi sana kwa hasara ya sifa nyingine.—10/1, ukurasa 10.

▫ Ni zipi baadhi ya hatua nzuri ambazo wazazi wamechukua ili kusaidia watoto wao kumtumikia Yehova?

Jambo muhimu ni kuanza mapema. Mawazo yapokewayo na masomo yasomwayo katika miaka ya mapema yatadumu muda wote wa maisha. (Mithali 22:6) Ni muhimu kuwafundisha utii na staha kwa Yehova na ibada yake katika mikutano yote. Wazazi wanaofanikiwa hujifunza kutambua mielekeo mibaya, nao husaidia watoto wao kuirekebisha. (Mithali 22:15) Mwishowe, anza mapema kumwekea mtoto wako miradi ya kitheokrasi anayoweza kufikia.—10/1, kurasa 27-8.

▫ Ni pande gani iliyo tofauti ya msamaha wa Yehova tunayopaswa kujaribu kutumia?

Yehova husamehe na kusahau. (Yeremia 31:34) Hili ni jambo gumu kwa viumbe vya kibinadamu kufanya. Umaana wa kufanya hivyo ulikaziwa na Yesu, kama ilivyorekodiwa katika Mathayo 6:14, 15.—10/15, kurasa 25-6.

▫ Ni vipi vikwazo vitatu vya kuwa kwetu wenye huruma?

Kwa sababu ya asili yetu ya kibinadamu ya dhambi, hisia za wivu zaweza kutokea. Tukimwonea mtu wivu, twaweza kumtendeaje kwa huruma nyororo? Kujiachilia kusivyofaa kwa jeuri ni kikwazo kingine. Kufanya hivyo huelekea kutufanya tukose hisia kwa wengine. Na zaidi, mtu mwenye ubinafsi aelekea kukosa huruma. (1 Yohana 3:17)—11/1, ukurasa 18-20.

▫ Twaweza kujifunza masomo gani kutokana na masimulizi ya Kimaandiko kuhusu Ayubu?

Masimulizi ya Ayubu yatufanya tutambue zaidi mbinu za Shetani na kutusaidia kuona jinsi enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote mzima inavyohusiana na uaminifu wa maadili wa binadamu. Kama Ayubu, ni lazima wote wampendao Mungu wajaribiwe. Sisi pia twaweza kuvumilia kama Ayubu alivyofanya, kumthibitisha Shetani kuwa mwongo, na kufurahia baraka za Ufalme wa Mungu.—11/15, ukurasa 20.

▫ Mwenyekiti wa baraza la wazee aweza kuonyeshaje staha ifaayo kwa mmoja na mwenzake?

Iwezekanapo, mwenyekiti apaswa kutoa orodha ya mambo ya kujadiliwa mapema sana vya kutosha ili kuruhusu wazee wengine kuwa na nafasi ya kutoa ufikirio wenye uangalifu na sala kwa kila jambo lililoorodheshwa. Katika mkutano wa wazee, yeye hatajaribu kushawishi maoni ya wazee, bali kuwatia moyo kutumia “uhuru mwingi wa usemi” kwa mambo yanayojadiliwa. (1 Timotheo 3:13)—12/1, ukurasa 30.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki