Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 9/1 uku. 3
  • Nyakati Ngumu kwa Wazee-Wazee

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nyakati Ngumu kwa Wazee-Wazee
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Familia ya Kikristo Huwasaidia Wazee-Wazee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Utunzaji wa Wazee-Wazee Tatizo Lenye Kukua
    Amkeni!—1991
  • Kutimiza Mahitaji ya Walio na Umri Mkubwa Kati Yetu—Takwa Gumu la Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Ni Daraka la Kikristo Kuwatunza Walio Wazee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 9/1 uku. 3

Nyakati Ngumu kwa Wazee-Wazee

MAMA ONIYAN, mwenye umri wa miaka 68, anaishi katika jiji moja kuu la Afrika Magharibi. Alipokuwa mchanga, alijiwazia akifurahia miaka yake ya uzeeni katika kustaafu kutulivu, akiwa amezingirwa na watoto na wajukuu wake. Badala ya hivyo, yeye hupisha siku zake akiuza maji baridi chini ya jua kali. Fedha kidogo anazochuma humsaidia kuendelea kuishi. Wana wake wawili wanaishi katika nchi nyingine iliyo mbali sana. Muda mrefu umepita tangu walipomtumia fedha zozote.

Nyakati zilizopita, wazee-wazee katika Afrika waliheshimiwa sana. Walistahiwa kwa sababu ya uzoefu na ujuzi wao, pamoja na hekima na utambuzi ambao hutokana nazo. Walisaidia kulea wajukuu. Wachanga walitafuta shauri lao na kibali chao. Watu waliishi kulingana na shauri hili la Biblia: “Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee.”—Mambo ya Walawi 19:32.

Nyakati zimebadilika. Umaskini, infleshoni, ukosefu wa kazi za kuajiriwa, na watu wengi kuhamia majijini ni mambo ambayo yameacha wazee-wazee walio wengi wajitegemee. Mkurugenzi wa shirika la HelpAge Kenya, Camillus Were, asema hivi: “Utamaduni wa kutegemeza na kutunza wazee-wazee umezidi kudhoofika.”

Bila shaka, kudhoofika kwa vifungo vya familia si jambo linalotukia katika nchi za Afrika pekee. Likisema juu ya Japani, Guardian Weekly laripoti hivi: “Ujitoaji wa watoto ulikuwa msingi wa mfumo wa Kijapani wa viwango vilivyopitishwa na Dini ya Confucius, lakini haukuokoka kule kuhamia kwa watu majijini na kudhoofika kwa vifungo vya familia: leo, asilimia 85 ya Wajapani hufa katika hospitali mbalimbali au katika makao ya watu wazee.”

Kwa hali yoyote ile, wanaotaka kumpendeza Mungu kikweli hujitahidi kuwaheshimu wazazi wao. Wanatii shauri hili la Biblia: “Heshimu baba yako na mama yako . . . ili ipate kuwa vema kwako nawe upate kudumu muda mrefu juu ya dunia.” (Waefeso 6:2, 3) Ingawa sikuzote si rahisi kuheshimu na kutunza wazee-wazee, kwaweza kuleta thawabu nyingi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki