Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 12/15 uku. 30
  • Je, Wakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Jitahidi Kuwaona Wengine Kama Yehova Anavyowaona
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Kufaidika Kutokana na Yaliyompata Yona
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Alijifunza Kutokana na Makosa Yake
    Igeni Imani Yao
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 12/15 uku. 30

Je, Wakumbuka?

Je, umefurahia kusoma matoleo ya juzijuzi ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa umefanya hivyo, utaliona kuwa jambo lenye kupendeza kukumbuka yafuatayo:

◻ Kwa nini twaweza kutumaini uchaguzi wa Yehova wa watu wanaoongoza watu wake?

Kwa ajili ya madaraka fulani, Yehova huchagua watu walio na sifa zihitajiwazo ili kuwaongoza watu wake katika njia anayotaka watembee kwa wakati fulani maalumu.—8/15, ukurasa wa 14.

◻ Twaweza kujifunza nini kutokana na jambo lililoonwa la Yona?

Yona alijifikiria kupita kiasi na kufikiria wengine kidogo tu. Twaweza kujifunza kutokana na Yona kwa kutotanguliza hisia zetu za kibinafsi.—8/15, ukurasa wa 19.

◻ Yaweza kusemwaje kwamba “jina la BWANA [“Yehova,” NW] ni ngome imara”? (Mithali 18:10)

Kukimbilia jina la Mungu humaanisha kumtumaini Yehova mwenyewe. (Zaburi 20:1; 122:4) Humaanisha kutegemeza enzi kuu yake, kutegemeza sheria na kanuni zake, na kuwa na imani katika ahadi zake, na kumpa yeye ujitoaji usiohusisha wengine. (Isaya 50:10; Waebrania 11:6)—9/1, ukurasa wa 10.

◻ Njia ya Paulo ya kutoa ushahidi mbele ya waheshimiwa yatutoleaje kielelezo?

Alipokuwa akisema na Mfalme Agripa, Paulo alitumia busara, akikazia mambo ambayo yeye na Agripa walikubaliana. Vivyo hivyo, twapaswa kukazia mambo yafaayo ya habari njema, tukikazia matumaini yanayofanana. (1 Wakorintho 9:22)—9/1, ukurasa 31.

◻ Ni nani ambao hunufaika na subira ya Yehova?

Kwa sababu ya subira ya Yehova, leo mamilioni ya watu zaidi wanapewa fursa ya kuokoka “siku ya Yehova” inayokuja. (2 Petro 3:9-15) Subira yake pia inaruhusu kila mmoja wetu ‘afulize kufanyiza wokovu wake mwenyewe kwa hofu na kutetemeka.’ (Wafilipi 2:12)—9/15, ukurasa wa 20.

◻ Tafsiri ya Biblia ya Septuagint ilikuwa na thamani kadiri gani?

Tafsiri hii ilitimiza mengi sana katika kueneza ujuzi juu ya Yehova Mungu na Ufalme wake na Yesu Kristo akiwa Mfalme. Kupitia Septuagint, msingi wa maana uliwekwa kwa Wayahudi na Wasio Wayahudi wasemao Kigiriki katika karne ya kwanza kukubali habari njema za Ufalme.—9/15, ukurasa wa 30.

◻ Mfano wenye somo wa mwana mpotevu watufunza nini kumhusu Mungu?

Kwanza, kwamba Yehova “ni mwenye rehema na neema, asiye mwepesi wa hasira na mwingi wa fadhili-upendo na kweli.” (Kutoka 34:6, NW) Pili, kwamba yeye yu “tayari kusamehe” badiliko la moyo linapomtolea msingi wa kuonyesha rehema. (Zaburi 86:5)—10/1, ukurasa wa 12, 13.

◻ Hali za amani zinazoahidiwa kwenye Isaya 65:21-25 zitatimizwa lini?

Wakiwa waabudu wa Yehova wenye muungano katika paradiso ya kiroho leo, watiwa-mafuta hali kadhalika wale wa “kondoo wengine” sasa wanajionea amani yenye kutolewa na Mungu. (Yohana 10:16) Nayo amani hiyo itaenea ndani ya Paradiso halisi, wakati ambapo ‘mapenzi ya Mungu yatatendeka duniani pote, kama ilivyo mbinguni.’ Wakati huo ndipo maneno ya nabii Isaya yatakapotimizwa kikamili. (Mathayo 6:10)—10/15, ukurasa wa 24.

◻ Kwa nini Wakristo husherehekea ukumbusho wa arusi lakini si siku za kuzaliwa?

Biblia haiioni ndoa kwa njia isiyopendeza. Ni jambo la kibinafsi kabisa kama Wakristo watachagua kuadhimisha siku ya ukumbusho wa arusi, ili kujikumbusha shangwe ya hiyo pindi na kufanya upya azimio lao la kujitahidi kufanikiwa wakiwa mume na mke. Hata hivyo, miadhimisho ya siku ya kuzaliwa iliyorekodiwa katika Biblia ni ile ya wapagani tu, nayo ilihusianishwa na matendo makatili.—10/15, ukurasa wa 30, 31.

◻ Katika kielezi cha Paulo kilichorekodiwa kwenye 1 Wakorintho 3:12, 13, “moto” wawakilisha nini, na Wakristo wote wapaswa kujua nini?

Kuna moto ambao sisi sote hukabili maishani—majaribu ya imani yetu. (Yohana 15:20; Yakobo 1:2, 3) Kila mtu tumfundishaye kweli atajaribiwa. Tukifundisha vibaya, huenda kukawa na matokeo yenye kuhuzunisha, kama Paulo alivyoonya. (1 Wakorintho 3:15)—11/1, ukurasa wa 11.

◻ Noa ‘alitembeaje na Mungu wa kweli’? (Mwanzo 6:9)

Noa alitembea pamoja na Mungu kwa sababu alifanya yale aliyoambiwa na Mungu afanye. Kwa kuwa alijitoa kufanya mapenzi ya Mungu, Noa alifurahia uhusiano mchangamfu na wa karibu pamoja na Mungu.—11/15, ukurasa wa 10.

◻ Ni fursa gani ambazo zimetolewa kwetu kwa kutojua wakati hususa ambapo kisasi cha Mungu kitatekelezwa juu ya waovu?

Hiyo hututolea fursa ya kuthibitisha kwamba twampenda Yehova kikweli na twataka kutembea katika njia zake milele. Hilo huonyesha kwamba sisi tu waaminifu-washikamanifu kwa Mungu na twatumaini njia yake ya kushughulikia mambo. Isitoshe, hiyo hutusaidia kuwa waangalifu na kuwa macho kiroho. (Mathayo 24:42-44)—11/15, ukurasa wa 18.

◻ Kuweka imani “katika jina la Mwana wa Mungu” kwamaanisha nini? (1 Yohana 5:13)

Kwamaanisha kutii amri zote za Kristo, kutia ndani amri yake ya ‘kupendana.’ (Yohana 15:14, 17) Upendo hutafuta kufanyia wengine mema. Huondolea mbali ubaguzi wote wa kitaifa, kidini, na kijamii.—12/1, ukurasa wa 7.

◻ Kwa nini Mashahidi wa Yehova ni “vitu vya kuchukiwa”? (Mathayo 10:22)

Mashahidi wa Yehova wamechukiwa isivyo haki kwa sababu zilezile zilizofanya Wakristo wa mapema wanyanyaswe. Kwanza, Mashahidi wa Yehova hutenda kulingana na itikadi zao za kidini katika njia ambazo huwafanya wasipendwe na wengine. Pili, wamekuwa shabaha za mashtaka yasiyo ya kweli—uwongo ulio wazi na kuwasilishwa kulikopotoka kwa itikadi zao.—12/1, ukurasa wa 14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki