Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 7/15 kur. 2-4
  • Kutafuta Matabiri Yanayotumainika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutafuta Matabiri Yanayotumainika
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uhitaji wa Kiasili wa Binadamu
  • Sababu Waweza Kuutumaini Unabii wa Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Ugiriki—Ile Serikali Kubwa ya Tano ya Ulimwengu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Ni Nani Atakayeutawala Ulimwengu?
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Kitabu Kinachotegemeka—Sehemu ya 5
    Amkeni!—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 7/15 kur. 2-4

Kutafuta Matabiri Yanayotumainika

PUNDE baada ya kuanza kutawala mwaka wa 336 K.W.K., Mfalme wa Makedonia aliyekuja kuitwa Aleksanda Mkuu alizuru madhabahu ya uaguzi ya Delphi huko Ugiriki ya kati. Katika mipango yake ya wakati ujao, yeye alikuwa na lengo la kushinda sehemu kubwa ya ulimwengu wa wakati huo. Lakini alitaka uhakikisho wa kimungu kwamba angefanikiwa katika shughuli hiyo kubwa. Hekaya husema kwamba siku ambapo alizuru Delphi, haikuruhusika kuwasiliana na mwaguzi wa madhabahu hiyo. Kwa kuwa hakutaka kuondoka bila jibu, Aleksanda alisisitiza, akimlazimisha kuhani huyo wa kike kutabiri. Kwa kukata tamaa, alisema hivi kwa sauti kubwa: “Ee, mtoto, hushindiki!” Mfalme huyo mchanga alichukua maneno hayo kuwa ishara ya mema—iliyotoa ahadi ya ushindi katika kampeni yake ya kijeshi.

Hata hivyo, Aleksanda angaliarifiwa vema zaidi juu ya matokeo ya kampeni yake kama angalichunguza unabii mbalimbali unaopatikana katika kitabu cha Biblia cha Danieli. Kwa usahihi wenye kutokeza, kilitabiri juu ya ushindi wake wa haraka-haraka. Mapokeo husema kwamba hatimaye Aleksanda alipata fursa ya kuona yale Danieli aliyokuwa ameandika kumhusu. Kulingana na Josephus, mwanahistoria Myahudi, mfalme huyo wa Makedonia alipoingia Yerusalemu, alionyeshwa unabii wa Danieli—huenda sura ya 8 ya kitabu hicho. (Danieli 8:5-8, 20, 21) Yasemekana kwamba kwa sababu hiyo, majeshi ya Aleksanda yenye kuharibu yaliachilia jiji hilo.

Uhitaji wa Kiasili wa Binadamu

Mfalme au mtu wa kawaida, mtu wa kale au wa kisasa—mwanadamu ameona uhitaji wa kupata matabiri yenye kutumainika kuhusu wakati ujao. Tukiwa viumbe wenye akili, sisi wanadamu huchunguza wakati uliopita, tuna habari juu ya wakati uliopo, na tunapendezwa hasa na wakati ujao. Mithali moja ya Kichina yasema hivi kwa kufaa: “Mtu ambaye angeweza kujua mambo yatakayotukia siku tatu kimbele, angekuwa tajiri kwa maelfu ya miaka.”

Katika enzi zote, mamilioni ya watu wamejaribu kuchungua wakati ujao kwa kutafuta habari kutokana na walichokiona kuwa mungu. Kwa mfano, fikiria Wagiriki wa kale. Walikuwa na madhabahu nyingi takatifu za uaguzi, kama zile za Delphi, Delos, na Dodona, ambapo walikuwa wakienda kutafuta habari kutoka kwa miungu yao kuhusiana na matukio ya kisiasa na ya kijeshi na pia mambo ya kibinafsi kama vile safari, ndoa, na watoto. Mbali na wafalme na viongozi wa kijeshi, makabila mazima-mazima pia yalitafuta mwongozo kutoka kwa makao ya roho kupitia habari hizi za waaguzi.

Kulingana na profesa mmoja, sasa kuna “ongezeko kubwa la ghafula la matengenezo ambayo yanajishughulisha na kuchunguza wakati ujao peke yake.” Hata hivyo, watu wengi hupendelea kupuuza chanzo pekee cha unabii sahihi—Biblia. Wao hupuuza waziwazi uwezekano wowote wa kwamba unabii mbalimbali wa Biblia una habari zilezile wanazotafuta. Wasomi wengine hata hulinganisha unabii wa Biblia na matabiri yaliyotolewa na waaguzi wa kale. Na kwa kawaida, watu wa kisasa wenye kutilia shaka hawapendelei unabii wa Biblia.

Twakualika uchunguze mwenyewe rekodi hiyo. Kulinganisha kwa makini matabiri ya Biblia na habari za waaguzi wa kibinadamu hufunua nini? Je, unaweza kuutumaini unabii wa Biblia kuliko habari za waaguzi wa kale? Na je, unaweza kutegemeza maisha yako juu ya unabii mbalimbali wa Biblia?

[Picha katika ukurasa wa 3]

Biblia ilitabiri ushindi wa haraka-haraka wa Aleksanda

[Hisani]

Cortesía del Museo del Prado, Madrid, Spain

[Picha katika ukurasa wa 4]

Aleksanda Mkuu

[Hisani]

Musei Capitolini, Roma

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 2]

COVER: General Titus and Alexander the Great: Musei Capitolini, Roma

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki