Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 12/1 uku. 25
  • Mpanuko wa Kitheokrasi Nchini Namibia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mpanuko wa Kitheokrasi Nchini Namibia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Sehemu ya 4—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Sababu kwa Nini Watu wa Namna Zote Wanakuwa Mashahidi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Tulikotumwa Kuwa Mishonari Kumekuwa Nyumbani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 12/1 uku. 25

Wapiga-mbiu wa Ufalme Waripoti

Mpanuko wa Kitheokrasi Nchini Namibia

HABARI njema za Ufalme wa Mungu zilifika Namibia kwa mara ya kwanza mwishoni mwa miaka ya 1920. Tangu wakati huo, mamia ya watu wenye mioyo minyofu wameitikia ujumbe wa wokovu wa Mungu. Mambo yafuatayo yaliyoonwa yaonyesha jinsi Yehova anavyokusanya kwenye kundi lake watu hao wenye kutamanika.—Hagai 2:7.

◻ Paulus, mkulima wa mazao ya chakula anayeishi kaskazini-mashariki mwa Namibia, alihubiriwa na Mashahidi wa Yehova kwa mara ya kwanza alipozuru Windhoek, jiji kuu. Muda si muda, Paulus akasadiki kwamba alikuwa ameipata kweli. Alirudi nyumbani akiwa na kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Kisha alipokuwa akisafiri kwenda Rundu, mji ulio karibu zaidi ambapo kuna Jumba la Ufalme, Paulus akaonana na Mashahidi na kuwasihi wamtembelee.

Hata hivyo, kwa kuwa aliishi mbali sana, Mashahidi hao walishindwa kwenda kujifunza Biblia pamoja na Paulus kila juma. Bila kuvunjika moyo, Paulus alianza kujifunza Biblia peke yake. Na zaidi, yeye pia alihubiria wengine mambo aliyokuwa akijifunza. Baada ya muda, kikundi cha kujifunza Biblia kikaanzishwa. Wakati watu kwenye kikundi hicho waliposikia kupitia redio kwamba kusanyiko la Mashahidi wa Yehova lingefanywa mjini Rundu, walikusanya mapato yao kidogo, na kufanya mipango kwa ajili ya usafiri ili wahudhurie.

Walisisimka kama nini kushirikiana na Mashahidi wa Yehova kwa mara ya kwanza! Upesi mipango ikafanywa ili ndugu wenye kustahili wawe wakikitembelea kikundi hicho kwa ukawaida. Leo, kuna wahubiri sita katika kijiji ambako Paulus anaishi.

◻ Johanna alianza kupendezwa na jina la Mungu aliposikia mtu fulani akiwasema vibaya Mashahidi wa Yehova. Yeye akumbuka: “Mara ya kwanza kabisa niliposikia jina Yehova, sikulisahau hata kidogo, nami nikaanza kujiuliza Yehova ni nani. Nilikuwa nikiishi na mume wangu karibu na Ghuba ya Walvis kwenye pwani ya Namibia. Wakati mmoja tulikwenda mjini, nami nikaona Mashahidi fulani wakitoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi barabarani. Nilichukua gazeti moja na kuomba funzo la Biblia, kwa kuwa nilikuwa na maswali mengi. Nililia waliponiambia kwamba hawangeweza kuja kwa sababu gari lao lilikuwa limeharibika. Muda mfupi baadaye, mume wangu akafa, nami nikaenda kuishi Keetmanshoop. Painia wa pekee (mweneza-evanjeli wa wakati wote) alikuwa amepewa mgawo wa kuhubiri huko, naye akanipa kitabu Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele. Niliitambua kweli tangu hapo mwanzoni.

“Hatimaye, nikaombwa nishiriki katika kazi ya kuhubiri, lakini kuogopa mwanadamu kukanifanya hoi kabisa. Nilipokuwa nikitembea kutoka mlango hadi mlango, nilisali kwa Yehova aniache nife badala ya kunitaka nihubiri. Nilipohubiri barabarani kwa mara ya kwanza, nilijificha katika kichochoro chembamba, nikitumaini kwamba hakuna yeyote ambaye angeniona. Hatimaye nilipiga moyo konde na kumtolea gazeti mtu aliyekuwa akipita, na wakati huo tu ndipo nilipoweza kusema kitu. Kwa msaada wa Yehova, siku hiyo nilizungumza na watu wengi juu ya tumaini langu lenye kutegemea Biblia.

“Leo, miaka 12 baadaye, japo umaskini, mimi ningali nathamini utumishi wa painia na ninaendelea kupata furaha nyingi sana kutokana na kuzungumza na wengine juu ya kweli ya Ufalme.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki