Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w08 4/1 uku. 24
  • Timotheo—Alikuwa Tayari na Mwenye Nia ya Kutumikia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Timotheo—Alikuwa Tayari na Mwenye Nia ya Kutumikia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Habari Zinazolingana
  • “Mtoto Wangu Mpendwa na Mwaminifu Katika Bwana”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Timotheo alitaka kuwasaidia watu
    Wafundishe Watoto Wako
  • Paulo, Sila, na Timotheo
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Timotheo—“Mtoto Halisi Katika Imani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
w08 4/1 uku. 24

Wafundishe Watoto Wako

Timotheo​—Alikuwa Tayari na Mwenye Nia ya Kutumikia

“JE, UKO tayari?” Je, umewahi kuulizwa swali hilo?— Mtu aliyekuuliza swali hilo alitaka kujua ikiwa ulikuwa umejitayarisha. Kwa mfano, huenda mtu huyo alikuwa akiuliza hivi: ‘Je, vitabu vyako viko tayari? Umepitia masomo yako?’ Kama tutakavyoona, Timotheo alikuwa tayari.

Timotheo alikuwa mwenye nia pia. Unajua hilo linamaanisha nini?— Timotheo alipoombwa amtumikie Mungu, alikuwa na mtazamo kama wa mtumishi mwingine wa Mungu, ambaye alisema: “Mimi hapa! Nitume mimi.” (Isaya 6:8) Kwa kuwa alikuwa tayari na mwenye nia ya kutumikia, Timotheo aliishi maisha yenye kusisimua. Je, ungependa kusikiliza simulizi la maisha yake?—

Timotheo alizaliwa huko Listra, jiji lililokuwa mamia ya kilomita kutoka Yerusalemu. Nyanya yake Loisi na mama yake Eunike, walijifunza Maandiko kwa bidii. Hata Timotheo alipokuwa angali mchanga, walianza kumfundisha kuhusu Neno la Mungu.—2 Timotheo 1:5; 3:15.

People helping the apostle Paul

What has happened?

People helping the apostle Paul

What has happened?

Huenda Timotheo bado alikuwa kijana wakati mtume Paulo, akiandamana na Barnaba, alipotembelea Listra katika safari yake ndefu ya kwanza ya kuhubiri. Inaelekea huo ndio wakati ambapo mama na nyanya ya Timotheo walikuwa Wakristo. Je, ungependa kusikia kuhusu matatizo ambayo Paulo na Barnaba walikabili?— Watu ambao hawakuwapenda Wakristo walimpiga Paulo kwa mawe na kumwangusha chini, kisha wakamkokota nje ya jiji. Walifikiri kwamba alikuwa amekufa.

Wale walioamini mambo ambayo Paulo alifundisha walimzunguka naye akainuka. Siku iliyofuata, Paulo na Barnaba waliondoka, lakini wakarudi Listra muda mfupi baadaye. Waliporudi, Paulo aliwatolea wanafunzi hotuba na kuwaambia hivi: “Lazima tuingie katika ufalme wa Mungu kupitia dhiki nyingi.” (Matendo 14:8-22) Je, unajua Paulo alimaanisha nini?— Alimaanisha kwamba wengine wangewaletea matatizo wale wanaomtumikia Mungu. Baadaye Paulo alimwandikia Timotheo hivi: ‘Wote wanaotamani kuishi maisha ya kimungu watateswa pia.’—2 Timotheo 3:12; Yohana 15:20.

Baada ya kuondoka Listra, Paulo na Barnaba walirudi nyumbani. Miezi kadhaa baadaye, Paulo alimchukua Sila ili asafiri pamoja naye, na wakiwa pamoja walirudi katika maeneo ambayo Paulo alikuwa ametembelea ili wakawatie moyo wanafunzi wapya. Walipofika Listra, Timotheo alifurahi kama nini kumwona Paulo tena! Timotheo alifurahi hata zaidi alipoombwa aandamane na Paulo na Sila. Timotheo alikubali. Alikuwa tayari na mwenye nia ya kuandamana nao.—Matendo 15:40–16:5.

Watu hao watatu walisafiri pamoja, wakitembea kilomita nyingi kwa miguu, kisha wakapanda mashua. Baada ya kufika pwani, walifunga safari kwa miguu hadi Thesalonike huko Ugiriki. Watu wengi katika eneo hilo wakawa Wakristo. Lakini wengine walikasirika na kufanyiza kikundi chenye ghasia. Uhai wa Paulo, Sila, na Timotheo ulikuwa hatarini, kwa hiyo wakaondoka kwenda Beroya.—Matendo 17:1-10.

Paulo aliwahangaikia waamini wapya wa Thesalonike, hivyo akamtuma Timotheo arudi huko. Unajua ni kwa nini?— Baadaye Paulo aliwaeleza hivi Wakristo waliokuwa Thesalonike: ‘Kusudi awaimarishe ninyi na kuwafariji ili yeyote asivunjike moyo.’ Unajua kwa nini Paulo alimpa Timotheo mgawo huo hatari?— Ni kwa sababu wapinzani hawakumjua vizuri Timotheo, na pia kwa sababu alikuwa mwenye nia ya kwenda. Alihitaji kuwa na ujasiri mwingi! Safari yake ilikuwa na matokeo gani? Timotheo aliporudi kwa Paulo, alimwambia jinsi Wathesalonike walivyokuwa waaminifu. Hivyo, Paulo akawaandikia hivi: “Tumefarijiwa juu yenu ninyi.”—1 Wathesalonike 3:2-7.

Timotheo alitumikia pamoja na Paulo kwa miaka kumi iliyofuata. Kisha, Paulo akafungwa gerezani huko Roma, naye Timotheo, ambaye alikuwa ameachiliwa kutoka gerezani, akaenda kukaa pamoja naye. Akiwa huko, Paulo aliwaandikia barua Wafilipi, na huenda alimtumia Timotheo kuiandika. Paulo alisema: ‘Ninatumaini kumtuma Timotheo kwenu, kwa maana sina mwingine aliye mwaminifu hivyo na ambaye atawatumikia vema kuliko yeye.’​—Wafilipi 2:19-22; Waebrania 13:23.

Hapana shaka kwamba maneno hayo yalimfurahisha sana Timotheo! Paulo alikuja kumpenda sana Timotheo kwa sababu alikuwa tayari na mwenye nia ya kutumikia. Tunatumaini kwamba utamwiga.

Maswali:

  • Timotheo alilelewa wapi, na ni nini kilichotukia Paulo alipotembelea eneo hilo mara ya kwanza?

  • Timotheo alifanya nini alipoombwa asafiri pamoja na Paulo na Sila?

  • Timotheo alionyesha ujasiri jinsi gani, na kwa nini Paulo alimpenda sana?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki