Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w10 5/1 kur. 14-15
  • Onyesha Usadikisho!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Onyesha Usadikisho!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Uharibifu wa Sodoma na Gomora
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Yesu Ashinda Vishawishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Yesu Anawaponya Watu Kimuujiza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Waliopanga Njama ya Kuua Wauawa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
w10 5/1 kur. 14-15

Kwa Ajili ya Vijana Wetu

Onyesha Usadikisho!

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Yeremia, Ebed-meleki, Mfalme Sedekia

Muhtasari: Yeremia anapingwa vikali sana anapotangaza ujumbe wa Mungu kwamba watu wa Yuda wanapaswa kujisalimisha kwa Wakaldayo.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA YEREMIA 38:1-5.

Unafikiri Yeremia alihisi namna gani alipokuwa akizungumza na watu wa Yuda?

․․․․․

Unafikiri sauti ya Yeremia ilionyesha hisia gani alipotangaza onyo la Yehova?

․․․․․

CHIMBA ZAIDI.

Yeremia alikuwa na usadikisho gani ambao ulimwezesha kutoa tangazo hilo kwa ujasiri?

․․․․․

2 CHUNGUZA TUKIO HILO.—SOMA YEREMIA 38:6-13.

Unawazia tangi hilo la maji lilikuwa na umbo, upana, kina, na harufu gani?

․․․․․

Huenda Yeremia alikuwa na mawazo gani alipoanza “kuzama katika yale matope”? (Soma tena mstari wa 6.)

․․․․․

CHIMBA ZAIDI.

Ukitumia vifaa vya kufanyia utafiti unavyoweza kupata, chunguza jambo ambalo hukujua kuhusu matangi ya maji yaliyotumiwa nyakati za Biblia.

․․․․․

Ebed-meleki alisadiki nini alipoomba Yeremia aokolewe? (Soma tena mistari ya 7-9.)

․․․․․

Kwa nini Sedekia alishawishiwa kwa urahisi sana, kwanza na wakuu na baadaye na Ebed-meleki? (Soma tena mstari wa 5 na 10.) Hilo linaonyesha nini kuhusu utu wake? jinsi alivyokosa usadikisho?

․․․․․

Ni watu gani katika simulizi hili ambao walionyesha usadikisho wenye nguvu, na ni nani ambaye hakuonyesha? Kwa nini unajibu hivyo?

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Ujasiri.

․․․․․

Usadikisho.

․․․․․

Jinsi Yehova anavyowalinda wale wanaomtii bila kuogopa.

․․․․․

Kuwa na usadikisho kunaweza kukusaidia jinsi gani kufanya yaliyo sawa unapokabili mkazo?

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

SOMA HABARI ZAIDI ZA BIBLIA, KWENYE INTANETI www.watchtower.org

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki