Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 7/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tunapaswa kusali jinsi gani?
  • Kumkaribia Mungu Katika Sala
    Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Yesu Anatufundisha Kusali
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 7/1 uku. 16
Mwanamume aliyezeeka akisali

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Kwa nini tunapaswa kusali?

Yehova Mungu anataka tumweleze mahangaiko yetu kwa uhuru na kwa ukawaida. (Luka 18:1-7) Anatusikiliza kwa sababu anatujali. Kwa kuwa Baba yetu wa mbinguni anatualika kwa fadhili tusali, basi tunapaswa kusali.—Soma Wafilipi 4:6.

Sala si njia ya kuomba tu msaada. Zaidi ya hilo, sala hutusaidia kumkaribia Mungu. (Zaburi 8:3, 4) Tunapomweleza Mungu hisia zetu kwa ukawaida, tunakuwa na urafiki wa karibu zaidi pamoja naye.—Soma Yakobo 4:8.

Tunapaswa kusali jinsi gani?

Tunaposali, Mungu hataki tutumie maneno ya kujionyesha au turudie sala zilizokaririwa. Wala si lazima tukae katika njia fulani hususa. Yehova anatualika tusali kutoka moyoni. (Mathayo 6:7) Kwa mfano, katika Israeli la kale, Hana alisali kuhusu tatizo la familia lililomsumbua. Baadaye, huzuni yake ilipogeuka na kuwa shangwe, alimshukuru Mungu kwa sala ya kutoka moyoni.—Soma 1 Samweli 1:10, 12, 13, 26, 27; 2:1.

Tuna nafasi nzuri ajabu! Tunaweza kumwambia Muumba mahangaiko yetu. Tunaweza pia kumsifu na kumshukuru kwa yale anayofanya. Kwa kweli, hatupaswi kupuuza nafasi hiyo yenye thamani.—Soma Zaburi 145:14-16.

Kwa habari zaidi, soma sura ya  17 ya kitabu hiki kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Kinapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki