Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp16 Na. 1 uku. 3
  • Je, Unyoofu Umepitwa na Wakati?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unyoofu Umepitwa na Wakati?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Habari Zinazolingana
  • Faida ya Kuwa Mnyoofu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Ni Kitu Gani Chenye Thamani ya Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Je! Nibatizwe?
    Amkeni!—1991
  • Kitabu cha Hekima Chenye Ujumbe Unaofaa Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
wp16 Na. 1 uku. 3
Mwajiri akimnyooshea kidole mfanyakazi

HABARI KUU | KWA NINI UWE MNYOOFU?

Je, Unyoofu Umepitwa na Wakati?

Hitoshi alikuwa mhasibu katika kampuni ya uwakala wa ajira huko Japani. Alipokuwa akifanya hesabu pamoja na bosi wake, Hitoshi aliambiwa aandike ripoti ya uwongo. Hitoshi alimweleza kwamba dhamiri yake haimruhusu kudanganya. Baada ya muda, Hitoshi alifukuzwa kazi.

Kwa miezi kadhaa, Hitoshi alivunjika moyo kwa sababu ya kukosa ajira. Kwa mfano, katika mahojiano ya kazi fulani, Hitoshi alieleza kwamba hangeweza kudanganya. Yule aliyemhoji akamwambia, “Unastaajabisha sana!” Ingawa watu wa familia na marafiki walimtia moyo awe imara na aendelee kuwa mnyoofu, Hitoshi alianza kuwa na mashaka. Kwa mfano, alisema hivi: “Nilianza kufikiria ikiwa ni jambo linalofaa kuwa mnyoofu kuhusu imani yangu.”

Mambo aliyokabili Hitoshi yanatukumbusha kwamba si kila mtu anapenda unyoofu. Kwa kweli, wengine wanaona unyoofu kuwa kizuizi hasa katika biashara. Mwanamke mmoja huko Afrika Kusini alisema hivi, “Nimezungukwa na watu wasio wanyoofu, na wakati mwingine ni vigumu kuwa mnyoofu.”

Kusema uwongo ni aina moja ya ukosefu wa unyoofu ulioenea sana leo. Miaka kadhaa iliyopita, utafiti uliofanywa na mwanasaikolojia Robert S. Feldmana wa chuo kikuu cha Massachusetts Amherst ulionyesha kwamba asilimia 60 ya watu hudanganya angalau mara moja katika kila mazungumzo ya dakika kumi. Feldman alisema hivi: “Matokeo hayo yalitushangaza sana, hatukutarajia uwongo uwe sehemu ya kawaida katika maisha yetu ya kila siku.” Inashangaza kwamba watu wengi wanachukia kudanganywa ilhali wao wenyewe husema uwongo.

Kwa nini kusema uwongo, kuiba, na aina nyingine za kukosa unyoofu ni mambo ya kawaida leo? Kukosa unyoofu kunawezaje kuiathiri jamii? Zaidi ya yote, tunawezaje kuepuka kunaswa na mazoea ya kukosa unyoofu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki