Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp16 Na. 1 kur. 4-5
  • Athari za Kukosa Unyoofu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Athari za Kukosa Unyoofu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUKOSA UNYOOFU HUFANYA WATU WASIKUAMINI
  • UDANGANYIFU HUZAA UDANGANYIFU
  • Kushinikizwa Usiwe Mnyoofu
    Amkeni!—2012
  • Kwa Sababu Gani Uwe Mwaminifu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Kwa Sababu Gani Udanganyifu Ni Mwingi Sana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Je! Unyofu Una Faida?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
wp16 Na. 1 kur. 4-5
Wanawake wawili wakiongea

HABARI KUU | KWA NINI UWE MNYOOFU?

Athari za Kukosa Unyoofu

“Kwa kawaida, kuna matatizo ambayo yanaweza kusuluhishwa ikiwa mtu atakosa unyoofu.”—Samantha, Afrika Kusini.

Je, unakubaliana na maneno hayo? Kama Samantha, sote tumewahi kukabili hali ngumu. Jinsi tunavyotenda tunapokabili hali inayojaribu unyoofu wetu, kutaonyesha wazi viwango tunavyofuata. Kwa mfano, huenda tukakosa kuwa wanyoofu ili kuepuka aibu. Hata hivyo, kukosa unyoofu husababisha matokeo mabaya ukweli unapojulikana. Fikiria mambo yafuatayo.

KUKOSA UNYOOFU HUFANYA WATU WASIKUAMINI

Mahusiano hujengwa na uaminifu. Watu wawili wanapoaminiana, wanahisi wakiwa salama salimini. Lakini uaminifu hautokei mara moja tu. Uaminifu hujengeka watu wanapotumia wakati mwingi pamoja, wanapowasiliana kwa unyoofu, na wanapotenda bila ubinafsi. Hata hivyo, tendo moja tu la kukosa unyoofu linaweza kufanya tusiaminiwe. Na uaminifu unapovunjika, inaweza kuwa vigumu sana kuujenga upya.

Je, umewahi kudanganywa na mtu ambaye ulifikiri ni rafiki mzuri? Ikiwa ndivyo, ulihisije? Huenda ulivunjika moyo na kuhisi umesalitiwa. Jambo hilo linaeleweka. Bila shaka, kukosa unyoofu kunaweza kuharibu uhusiano mzuri.

UDANGANYIFU HUZAA UDANGANYIFU

Uchunguzi uliofanywa na profesa wa uchumi Robert Innes wa Chuo Kikuu cha California, ulionyesha kwamba “ukosefu wa unyoofu huambukiza.” Hivyo, kukosa unyoofu kunaweza kulinganishwa na virusi kwani kadiri unavyoshirikiana na mtu mwongo, ndivyo unavyokuwa katika mazingira hatari zaidi ya “kuathiriwa” na uwongo.

Unawezaje kuepuka kunaswa na mtego wa kukosa unyoofu? Biblia inaweza kukusaidia. Tafadhali chunguza kanuni chache za Biblia.

Aina za Ukosefu wa Unyoofu

Kusema Uwongo

Mwanaume akivua pete ya ndoa

KUNAMAANISHA NINI? Kumweleza uwongo mtu anayepaswa kujua ukweli. Kusema uwongo kunaweza kuhusisha kupotosha habari ili kumficha mtu ukweli, kutoeleza habari za msingi ili kumdanganya mtu, na kutia chumvi habari fulani.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: “Mtu mwenye hila ni chukizo kwa Yehova, lakini urafiki Wake uko pamoja na watu wanyoofu.” (Methali 3:32) “Sasa kwa kuwa mmeuondolea mbali uwongo, semeni kweli kila mmoja wenu na jirani yake.”—Waefeso 4:25.

Uchongezi

Wanaume wakinong’ona wakati mwenzao akiingia chumbani

UNAMAANISHA NINI? Kusema uwongo na maneno ya hila ili kuharibu sifa nzuri ya mtu.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: “Mtu mwenye hila huendelea kutokeza ugomvi nyakati zote, na mchongezi anawatenganisha wale wanaofahamiana.” (Methali 16:28) “Pasipo na kuni moto huzimika, na pasipo na mchongezi ugomvi hutulia.”—Methali 26:20.

Ulaghai

Mwanaume akionyesha saa za mkononi alizoficha kwenye koti

UNAMAANISHA NINI? Kumshawishi mtu akupatie pesa au mali kwa ahadi ya uwongo.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: “Hupaswi kumpunja mfanyakazi wa kukodiwa aliye katika taabu na aliye maskini.” (Kumbukumbu la Torati 24:14, 15) “Yeye anayempunja mtu wa hali ya chini amemletea shutuma Mtengenezaji wake, lakini anayemwonyesha maskini kibali anamtukuza Yeye.”—Methali 14:31.

Wizi

Mtu akiiba pochi kwenye mkoba

UNAMANISHA NINI? Kuchukua mali ya mtu mwingine bila ruhusa.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: “Mwizi asiibe tena, bali afanye kazi ya bidii, akifanya kwa mikono yake kazi iliyo njema, ili awe na kitu cha kumgawia mtu aliye na uhitaji.” (Waefeso 4:28) “Msipotoshwe. . . . Wezi, wala watu wenye pupa, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi hawataurithi Ufalme wa Mungu.”—1 Wakorintho 6:9, 10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki