Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp17 Na. 5 kur. 7-8
  • Jinsi Malaika Wanavyoweza Kukusaidia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Malaika Wanavyoweza Kukusaidia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MALAIKA WALILITEGEMEZA KUTANIKO LA MAPEMA LA KIKRISTO
  • JINSI MALAIKA WANAVYOWEZA KUKUSAIDIA
  • Namna Malaika Wanavyoweza Kukusaidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Malaika—Jinsi Wanavyohusika Katika Maisha Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Malaika—Je! Wao Wanaathiri Maisha Yako Wewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
wp17 Na. 5 kur. 7-8

HABARI KUU | MALAIKA​—JE, WANAHUSIKA KATIKA MAISHA YAKO?

Jinsi Malaika Wanavyoweza Kukusaidia

Malaika waaminifu wanapendezwa na mambo yanayohusu wanadamu, nao wanashiriki katika kutimiza mapenzi ya Yehova. Mungu alipoiumba dunia, malaika walipiga “vigelegele pamoja kwa shangwe, na wana wote wa Mungu wakaanza kupaaza sauti kwa kushangilia.” (Ayubu 38:4, 7) Katika historia yote, malaika wametamani “kuchungulia” ndani ya unabii unaohusu matukio ya wakati ujao duniani.—1 Petro 1:11, 12.

Biblia inaonyesha kwamba, ili mapenzi ya Mungu yatimie, nyakati fulani malaika waliandaa ulinzi wa kiasi fulani kwa waabudu wa kweli. (Zaburi 34:7) Kwa mfano:

  • Yehova alipoharibu majiji yenye uovu ya Sodoma na Gomora, malaika walimsaidia mwanamume mwadilifu, Loti, na familia yake kukimbia.—Mwanzo 19:1, 15-26.

  • Katika Babiloni la kale, vijana watatu Waebrania walipohukumiwa kifo katika tanuru la moto, Mungu alimtuma “malaika wake na kuwaokoa watumishi wake.”—Danieli 3:19-28.

  • Baada ya mwanamume mwadilifu Danieli kukaa usiku kucha katika shimo lenye simba wakali, alisema kuwa alibaki hai kwa sababu “Mungu . . . alimtuma malaika wake na kufunga vinywa vya simba.”—Danieli 6:16, 22.

Malaika akimlinda Danieli asiumwe na simba

Kwa muda mrefu malaika wamekuwa wakiwasaidia wanadamu waaminifu

MALAIKA WALILITEGEMEZA KUTANIKO LA MAPEMA LA KIKRISTO

Nyakati fulani malaika walio wajumbe wa Mungu waliingilia kati utendaji fulani wa kutaniko la mapema la Kikristo ilipohitajika ili kutimiza mapenzi ya Yehova. Kwa mfano:

  • Malaika alifungua milango ya gereza na kuwaagiza mitume waliokuwa wamefungwa humo waendelee kuhubiri katika hekalu.—Matendo 5:17-21.

  • Malaika alimwelekeza Filipo mweneza injili aende katika barabara ya jangwani inayotoka Yerusalemu kwenda Gaza na kumhubiria Mwethiopia ambaye alienda Yerusalemu kuabudu.—Matendo 8:26-33.

  • Wakati wa Mungu ulipofika kwa watu wasio Wayahudi kuwa Wakristo, malaika alimtokea katika maono ofisa Mroma aliyeitwa Kornelio na kumwagiza amwalike mtume Petro nyumbani kwake.—Matendo 10:3-5.

  • Mtume Petro alipokuwa gerezani, malaika alimtokea na kumwachia huru.—Matendo 12:1-11.

JINSI MALAIKA WANAVYOWEZA KUKUSAIDIA

Hakuna uthibitisho wa kwamba siku hizi Mungu anawatumia malaika kuwasaidia watu kimuujiza kama ilivyo kwenye visa vinavyotajwa katika Biblia. Hata hivyo, kuhusu wakati wetu, Yesu alisema hivi: “Na hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Je, unajua kwamba wanafunzi wa Kristo wanafanya kazi hiyo chini ya mwongozo wa malaika?

Watu wakipita karibu na kigari cha machapisho

Malaika husaidia kutangaza habari njema duniani pote

Kitabu cha Ufunuo kinaonyesha kwamba kwa bidii malaika wanawasaidia watu duniani kote kujifunza kumhusu Yehova Mungu na kusudi lake kwa wanadamu. Mtume Yohana aliandika hivi: “Nami nikamwona malaika mwingine akiruka katikati ya mbingu, naye alikuwa na habari njema ya milele ili aitangaze kuwa habari za furaha kwa wale wanaokaa duniani, na kwa kila taifa na kabila na lugha na watu. Akisema kwa sauti kubwa: ‘Mwogopeni Mungu na kumpa utukufu, kwa sababu saa ya hukumu yake imefika, na kwa hiyo mwabuduni Yeye aliyezifanya mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji.’” (Ufunuo 14:6, 7) Leo kuna visa vingi vinavyothibitisha kwamba malaika wanaunga mkono kazi ya kuhubiri Ufalme ulimwenguni pote. Kwa kweli, hata mtenda dhambi mmoja tu anapotubu na kumrudia Yehova, “shangwe hutokea kati ya malaika za Mungu.”—Luka 15:10.

Ni nini kitakachotokea baada ya kazi ya kuhubiri kukamilika? ‘Majeshi ya mbinguni’ ya malaika yataungana na Yesu Kristo, Mfalme wa wafalme, ili kupigana “vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote,” katika Har–Magedoni. (Ufunuo 16:14-16; 19:14-16) Malaika wenye nguvu watatumika wakiwa watekelezaji wa hukumu ya Mungu wakati Bwana Yesu “anapoleta kisasi juu ya wale . . . wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.”—2 Wathesalonike 1:7, 8.

Uwe na hakika kwamba malaika wanapendezwa na hali yako njema. Wanahangaikia sana hali ya wale wanaomtumikia Mungu, na Yehova amewatumia mara kwa mara kuwaimarisha na kuwalinda watumishi wake waaminifu duniani.—Waebrania 1:14.

Hivyo basi, kila mmoja wetu ana uamuzi muhimu sana anaopaswa kufanya. Je, utasikiliza na kutii habari njema inayohubiriwa duniani pote? Mashahidi wa Yehova walio katika eneo lako watafurahi kukusaidia ufaidike na msaada wenye upendo wa malaika wa Mungu wenye nguvu.

Ili kupata ufafanuzi zaidi wa Biblia kuhusu malaika wazuri na waovu, soma sura ya 10 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Pia, kinapatikana kwenye www.jw.org/sw.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki