Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w17 Oktoba uku. 32
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Kula Viapo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Mahubiri ya Mlimani—“Usiape Kabisa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
w17 Oktoba uku. 32

Je, Wajua?

Kwa nini Yesu alishutumu zoea la Wayahudi la kuapa?

Mtu akiapa hekaluni

VIAPO fulani vilikubalika katika Sheria ya Musa. Hata hivyo, lilikuwa jambo la kawaida sana kwa watu wa siku za Yesu kuapa hivi kwamba waliapa ili kuthibitisha ukweli wa kila jambo walilosema. Ingawa zoea hilo lilikusudiwa kuthibitisha ukweli wa mambo ambayo mtu alisema, Yesu alishutumu zoea hilo katika pindi mbili tofauti. Alifundisha hivi: “Acheni tu neno lenu Ndiyo limaanishe Ndiyo, Siyo yenu, Siyo.”—Mt. 5:33-37; 23:16-22.

Kamusi Theological Dictionary of the New Testament, inasema kwamba “zoea la Wayahudi la kuthibitisha kila jambo kwa kuapa” lilikuwa limekita mizizi sana; jambo hilo linaonekana wazi katika mistari ya Talmud ambayo inataja kihususa viapo ambavyo vingeweza kukubalika na ambavyo vingeweza kuvunjwa.

Si Yesu peke yake aliyeshutumu mazoea hayo mabaya. Kwa mfano, mwanahistoria Myahudi Flavius Josephus alisema hivi kuhusu dhehebu fulani la Kiyahudi: “Waliepuka kuapa, kwa kuwa waliona kufanya hivyo kuwa jambo baya zaidi kuliko kusema uwongo, na walisema kwamba ikiwa mtu haaminiki bila kuapa kwa Mungu, tayari yeye ni mwenye hatia.” Pia, maandishi ya Kiyahudi ya apokrifa yanayoitwa Wisdom of Sirach, au Ecclesiasticus, (23:11) yanaeleza hivi: “Mwanamume mwenye zoea la kuapa ameasi sheria kabisa.” Hivyo, Yesu alishutumu zoea la kuapa kivivihivi. Ikiwa tunazungumza kweli wakati wote, hatuhitaji kuapa ili maneno yetu yaaminike.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki