Tumia Vitolewaji Vipya Ili Kufanya Mapenzi ya Mungu
1 Pasipo shaka Yehova Mungu, ‘ametuandaa sisi kwa kutupatia kila kitu chema ili tufanye mapenzi yake.’ Kwa sababu hiyo, tunapotumia kwa matokeo mazuri vitu ambavyo yeye anaandaa, Yehova ‘anafanyiza ndani yetu kupitia Yesu Kristo kile ambacho kinapendeza machoni pake.’—Ebr. 13:20, 21, NW.
2 Historia ya ki-siku-hizi ya watu wake inaonyesha kwamba Yehova Mungu ametoa mwelekezo na ametuandalia vichapo tunavyohitaji ili tutimize kazi ambayo yeye ametupa sisi tuifanye. (Mt. 24:14; 28:19, 20; Ufu. 9:17, 19) Yehova amebariki matumizi mazuri ya vifaa hivi, na kundi la Kikristo linazidi kupata ukuzi wenye kutokeza.
VITOLEWAJI VIPYA
3 Hivi majuzi, kwenye “Tumaini Katika Yehova” Mikusanyiko ya Wilaya yetu, sisi tulisisimuka kupokea vichapo vipya ili kuwasaidia wengine waweke tumaini lao imara katika Mungu. Mwishoni mwa hotuba yake Ijumaa asubuhi, mwenyekiti alitoa trakti mpya, Sababu Kwa Nini Unaweza Kuitumaini Biblia. Halafu, alasiri maonyesho yenye kufaa yalitolewa kutuonyesha jinsi ya kuitumia.
4 Je! wewe umekuwa ukitumia trakti hizi? Zinafaana na Kichwa cha Mazungumzo cha sasa. Wengine ambao wanahitaji kutumia utoaji mfupi wataona trakti hii kuwa yenye msaada sana. Walio wengi wetu tutaweza kuitumia kwa matokeo mazuri katika huduma yetu katika njia mbalimbali—pengine kutoa utangulizi wa utoaji wetu, kuitoa wakati mwenye nyumba ana shughuli, na kuiacha wakati tunapokuta kwamba hakuna mtu nyumbani.
5 Ilikuwa furaha kujua kwamba sasa trakti tatu zaidi zinapatikana. Hizo ni Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini?, Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani, na Kuna Tumaini Gani Kwa Wapendwa Waliokufa? Pia trakti hizi zitawasaidia wengine wajifunze yale ambayo Biblia inafundisha na sababu kwa nini wao wanaweza kuitibari ahadi za Mungu. Hakikisha kwamba unachukua nyingine zazo ili uzitumie katika kutoa ushuhuda wa kawaida na wa vivi hivi.
6 Kitolewaji kipya kwenye “Tumaini Katika Yehova” Mkusanyiko wa Wilaya kinachothaminiwa sana ni ile Biblia ya chapa ya mfukoni ya New World Translation of the Holy Scriptures. Kwa miaka iliyopita, sisi tumetumia Biblia mbalimbali katika huduma ya shambani, lakini sasa tuna moja inayoweza kuchukuliwa mfukoni au mkobani. Hii ni ithibati nyingine kwamba Yehova Mungu ‘ametuandaa sisi kwa kutupatia kila kitu chema ili tufanye mapenzi yake.’ Hivyo tuwe tunashiriki katika sehemu za kawaida za utumishi au kutoa ushuhuda wa vivi hivi, sisi tunaweza kuwa na nakala ya Neno la Mungu tayari ili litutegemeze kwa yale tunayosema. Jinsi tulivyo wenye furaha kuwa na Biblia hii mpya ya chapa ya mfukoni New World Translation of the Holy Scriptures!
VITUMIE VIZURI
7 Wakati vitolewaji hivi vipya vilipotangazwa makofi yalipigwa kwa nguvu. Mara moja tungeweza kuona wema ambao ungetimizwa katika kazi ya kuhubiri na kufundisha kwa msaada wa maandalio haya ya wakati unaofaa kutoka kwa Yehova, ‘Mpaji wa kila zawadi njema na kamilifu.’ (Yak. 1:17, NW) Kwa kiasi tunachotumia vichapo hivi, tunaweza kutazamia shangwe yetu iongezeke kwa sababu ya tunda jema la Ufalme ambalo litatokezwa.—Yohana. 15:8.
8 Tukipata somo kutokana na mfano wa maneno wa Yesu kuhusu zile talanta, tunajua kwamba Yehova anatutazamia tutumie vizuri kila kitu ambacho yeye ametupa. Basi, na tutimize huduma yetu kikamili kwa kutumia maandalio haya yake, kutia ndani vitolewaji vipya. Kama matokeo, sisi tutapokea upendeleo wa Bwana wetu na baraka.