Kutangaza Habari Njema—Kwa Kutumia Biblia
1 “Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu.” (Ebr. 4:12) Ili litumie nguvu zalo kwa ukamili na liwe hai, lazima lisomwe na kutumiwa. Kutimiza jambo hili zaidi, tengenezo la Yehova, lilianza hasa katika 1954, kututia moyo tutumie Biblia katika huduma yetu ya nyumba kwa nyumba. Tulizoezwa kutoa hotuba ya dakika tatu mpaka nane katika ziara za nyumba kwa nyumba na kuwafahamisha wenye nyumba yale ambayo Biblia inayo kuhusu habari muhimu.
2 Katika miaka ya karibuni zaidi, kwa ukawaida Huduma ya Ufalme Yetu imekuwa na Kichwa cha Mazungumzo, kikionyesha maandiko mawili au matatu juu ya habari ya kutumia katika utumishi wa shambani. Mathalani, kwa wakati huu Kichwa cha Mazungumzo ni juu ya kichwa “Dini Ambayo Ina Thamani ya Kweli.” Maandiko yatakayotumiwa yanakazia tofauti baina ya dini ya bandia na ya kweli.
3 Kutumia Biblia kwa matokeo mazuri kunahitaji mazoezi na tamaa ya kuwasaidia watu wang’amue kwamba hilo kweli kweli ni Neno la Mungu na li hai na lina nguvu. Huku sisi tukitiwa moyo tutumie utoaji mfupi, wenye kupiga kichwa cha msumari katika utendaji wa siku ya magazeti, hatutaki kuwa wenye kuzembea kutumia Biblia katika sehemu nyingine za huduma ya shambani. Ingawaje, sisi tu wanafunzi wa Biblia, na kuna njia gani ambayo ni bora zaidi ya kutoa ithibati hivyo isipokuwa kwa kujitahidi kuwaonyesha watu kutoka Neno la Mungu lenyewe yale ambayo Yehova anayo akibani kwa ajili ya aina ya wanadamu na dunia hii?
MSAADA KUTOKA KITABU REASONING
4 Kwa kuongezea Kichwa cha Mazungumzo katika Huduma ya Ufalme Yetu, tuna kitabu Reasoning From the Scriptures. Unapopitia matangulizi yaliyo kwenye kurasa 9-15, utapata marejezo kwenye mistari ya Biblia ambayo yanaweza kutumiwa katika kutoa ujumbe wa Ufalme. Kuna njia nyingi mbalimbali ambazo kwazo tunaweza kuiendea Biblia ili kuwaonyesha watu yale ambayo inasema.
5 Mathalani, ikiwa wenye nyumba fulani wanahangaikia wazee-wazee, huenda likawa jambo lenye msaada kufuata yale ambayo yamedokezwa kwenye kitabu Reasoning katika ukurasa 14 chini ya kichwa “Uzee/Kifo.” Jinsi swali lifuatalo lingekuwa lenye kufaa sana: “Je! umetaka kujua kwa nini tunazeeka na kufa? Mimi ningependa kukuonyesha wewe yale ambayo mwandikaji wa Biblia alisema katika Warumi 5:12.” Kisha ungeweza kusema: “Lakini ingawa Biblia inaonyesha kwa nini tunazeeka na kufa, hiyo pia inatutolea sisi tumaini la ajabu sana kwa wakati ujao, kama inavyopatikana katika Ufunuo 21:3, 4.” Toleo la sasa la kitabu lingeweza kuonyeshwa.
6 Mara nyingi sana siku hizi watu wanasema, “La, mimi nina shughuli.” Kwa kweli wengi wana shughuli, na sisi twapaswa kuthamini kwamba huenda ikawa hivyo kwa hali yao. Hata hivyo, ikiwa hali zinafaa, huenda ukasema: “Ninajua hisi hiyo, kwa kuwa hizi ni nyakati zenye shughuli mno. Hata hivyo, ningependa kukuacha na wazo hili moja tu,” kisha ufungue mojapo maandiko katika Kichwa cha Mazungumzo yetu cha sasa. Baada ya kulisoma, huenda ukataja mara moja kitabu unachotoa, acha trakti inayofaa, au useme kwamba utakuwa katika eneo hilo tena karibuni na utapitia ili ushiriki habari zaidi kuhusu uwezekano wenye kupendeza wa kuishi bila kufa.
7 Ni vema sana watu wanapoona kwamba sisi tu wanafunzi wa Biblia, walio stadi katika kutumia Neno la Mungu katika huduma yetu! Hilo linawasaidia kutambulisha watu ambao leo wanategemea Neno la Mungu na kulitumia katika maisha yao ya kila siku. Hivyo, zaidi ya siku ya kutoa magazeti, uwe tayari kutumia Biblia wakati unapotoa toleo la kawaida la kitabu. Jitihada zetu za kutumia Biblia zitaleta baraka ya Yehova kwa huduma yetu na kukaza akilini mwa wengi kwamba kweli kweli Neno la Mungu li hai, lina nguvu, na linaweza kuathiri maisha zao.