Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/88 uku. 3
  • Tegemeza Mipango ya Utumishi wa Katikati ya Juma

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tegemeza Mipango ya Utumishi wa Katikati ya Juma
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MIPANGO ILIYOPANGWA KITENGENEZO YAHITAJIWA
  • TEGEMEZA MIPANGO YA KWENU
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani Inayotimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Kutangaza Habari Njema—Katika Kutoa Ushuhuda Tukiwa Kikundi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 3/88 uku. 3

Tegemeza Mipango ya Utumishi wa Katikati ya Juma

1 Katika unabii wake kuhusu wakati wa mwisho, Yesu alisema, “Katika mataifa yote habari njema zapasa kuhubiriwa kwanza.” (Marko 13:10, NW) Katika kutii amri hii, watu wa Yehova ulimwenguni pote ni watendaji katika huduma si katika miisho-juma tu lakini wakati wote wa juma pia. Wazee wa mahali penu wanatiwa moyo kuratibu mikutano inayofaa kwa utumishi wa shambani wakati wa juma. Je! wewe unaweza kushiriki katika utumishi wa shambani wa katikati ya juma pamoja na wengine katika kundi lako?

MIPANGO ILIYOPANGWA KITENGENEZO YAHITAJIWA

2 Mwangalizi wa utumishi apaswa aongoze katika kufanya mipango halisi ya utumishi wa katikati ya juma. Mahali, siku, na wakati wapaswa uwe wenye kufaa kwa wahubiri walio wengi. Mikutano ya utumishi wa shambani inadhaminiwa na kundi na kwa kawaida ingesimamiwa na wazee, watumishi wa huduma, au ndugu wengine waliobatizwa wanaostahili. Ikiwa ndugu hao wanaostahili hawapatikani, akina dada wenye uwezo waliobatizwa wanaweza kupewa mgawo huo. (Angalia Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, ukurasa 77, fungu 3.) Dada aliyepewa mgawo huo apaswa kufunga kitambaa na kwa kawaida angeketi akiwa anaongoza mkutano wa utumishi wa shambani.

3 Wale ambao wamepewa mgawo wa kuongoza mikutano hii wapaswa kuwa wamejitayarisha vizuri. Andiko la siku laweza kuzungumziwa, hasa ikiwa linafaa utumishi wa shambani. Habari kutoka Mikutano ya Utumishi wa Shambani zapaswa kutumiwa. Eneo linalofaa na migawo ya vikundi-vikundi yapaswa yafanywe. Upendezi wa kipekee unaweza kuonyeshwa katika kuwasaidia wahubiri wapya ambao huenda wakawa wanashiriki katika huduma.

TEGEMEZA MIPANGO YA KWENU

4 Wale wanaotegemeza mipango ya katikati ya juma kwa ajili ya utumishi wa shambani wana nafasi nyingi za kuwakuta wenye nyumba ambao huenda wasiwe nyumbani wakati wa miisho-juma. Huenda ukafanya kazi pamoja na wahubiri na mapainia wengine ambao wanashiriki katika utumishi wa shambani wakati wa juma. Akina dada wengi ambao wana watoto shuleni wanathamini mpango huu. Wahubiri wengine wenye wenzi wasioitikadi wamepata kwamba mpango wa kwenda katika utumishi wa shambani siku za juma ni wenye msaada sana. Vijana wanaolikiza kutoka kwa shule wanaweza kutegemeza mipango ya utumishi wa katikati ya juma. Mara nyingi mapainia na wahubiri wenye ujuzi wanakuwapo ili waambatane na wapya na walio na ujuzi mdogo katika sehemu mbalimbali za huduma wakati wa juma.

5 Wote wanatiwa moyo wafike kwa saa na kushiriki mazungumzo na sala. Kufanya kwako hivyo kutakusaidia ushiriki kwa bidii katika huduma ya shambani na kutafuta watu wanaostahili katika eneo ulilogawiwa.—Mt. 10:11.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki