Uwe Na Bidii Kwa Ajili ya Ibada Safi
1 Yehova ni Mungu mwenye bidii. (Isa. 9:7; 59:17) Inatazamiwa kwamba wote wampendao Yehova wangejithibitisha wenyewe kuwa wenye bidii katika kuabudu yeye. Kama Yesu, wanaonyesha hangaiko la kweli kwa utukufu wa Yehova na hali ya kiroho ya aina ya kibinadamu.—Zab. 69:9; Yn. 2:17.
2 Kupitia tengenezo la Yehova tunapokea vikumbusho daima vitusaidie tuwe wenye bidii katika utumishi wetu kwa Yehova. Kwa kutii vikumbusho hivi, hatutakuwa wenye moyo nusu-nusu katika ibada yetu. (Zab. 119:113) Tutawaiga wanaume wenye bidii kama Yehu na mtume Paulo, pia watumishi wengine wa Mungu wenye imani.—2 Fal. 10:16; 1 Kor. 14:12.
KATIKA HUDUMA YA SHAMBANI
3 Wakati wa mwezi wa Mei, tutakuwa na nafasi nyingi nzuri kuonyesha bidii tunapoendelea kutoa uandikisho wa Mnara wa Mlinzi. Tangu 1879 Mnara wa Mlinzi umepatikana kwa uandikisho, na mamilioni ya watu wanaendelea kunufaika wakiwa waandikishaji wa kawaida. Zaidi ya milioni tatu ya wasomaji walo kwa idili sasa wanawatolea wengine ujumbe wa Biblia unaotegemea Mnara wa Mlinzi. Wakati wa kampeni ya uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi, tunataka kutumia Kichwa cha Mazungumzo cha sasa, “Biblia Inanufaisha Maisha ya Jamaa.” Hili linaweza kufanywa jinsi gani?
4 Baada ya kujifahamisha, huenda ukauliza: “Je! wewe umepata kuona kwamba jamaa nyingi zinapata tatizo la kuvumilia mikazo ya maisha leo? [Ruhusu jibu.] Huku nyingine zikionekana kuwa zinaendelea vizuri sana, nyingi zinapatwa na matatizo magumu kuanzia watoto wasiotii kufikia kutendwa vibaya kwa watoto na kutoka ukosefu wa itibari kwa ujumla kufikia mvunjiko wa ndoa na jamaa. Wewe unafikiri washiriki wa jamaa wenye kuhangaika wanaweza kugeukia wapi ili wapate shauri na msaada wenye kuitibarika? [Ruhusu jibu.] Aliyeanzisha ndoa, Muumba mwenyewe, anatupa shauri bora zaidi kuhusu maisha ya jamaa. Angalia jinsi Mwanzo 1:27, 28 hutaarifu kusudi la Mungu kwa ajili ya jamaa ya kibinadamu. [Soma.] Kwa kuwa Mungu alianzisha mpango huo, Yeye ndiye anayejua jamaa inahitaji nini ili ipate furaha ya kweli. Sisi sote tunaweza kunufaika kwa kufuata maagizo ya Mungu kuhusu maisha ya jamaa. [Soma Isaya 48:17, 18.] Kwa miaka zaidi ya mia moja, Mnara wa Mlinzi umeelekeza fikira za wasomaji walo kwenye kanuni za Biblia ambazo zinanufaisha maisha ya jamaa.” Kisha, baada ya kuvuta fikira kwenye jambo fulani katika toleo la karibuni, toa uandikisho.
5 Huenda ukalipata kuwa jambo lenye msaada kurudia matangulizi yanayopatikana katika kitabu Reasoning kwenye kurasa 10 na 11 chini ya vichwa “Biblia/Mungu” na “Jamaa/Watoto.” Matangulizi haya yanaweza kubadilishwa ili yafaane na hali zinazopatikana katika eneo lenu la kundi.
6 Acha bidii ya kweli ya Kikristo ikusukume wewe uzungumze juu ya ujumbe wa ibada safi ambayo imechapishwa katika Mnara wa Mlinzi. Zungumza ukiwa na mwelekeo unaofaa, ukiwa na usadikisho. Watu wa aina ya kondoo watasikia ujumbe wa Biblia kwa uthamini nao wataitikia kwa kupenda.
7 Tunapotumia kila nafasi kujulisha habari njema, watu wenye moyo wa haki na waone kwamba sisi tu “watu . . . wenye bidii kwa ajili ya kazi njema.”—Tito 2:14, NW.