Kutangaza Habari Njema—Katika Kutoa Ushuhuda Tukiwa Kikundi
1 Kukutana na wengine kwa kujitayarisha kwa ajili ya utumishi wa shambani ni jambo lenye mafaa na lenye kujenga pia. Uandalizi huo unatia moyo ndugu zetu wafanye kazi bega kwa bega katika kutangaza habari njema.
2 Huenda makundi fulani yakaratibu kuwe na mkutano wa utumishi wa shambani baada ya mikutano ya kawaida kwenye Jumba la Ufalme. Ingawa huenda hesabu inayounga mkono mpango huu ikawa kubwa sana, bado viongozi wa mafunzo ya kitabu wanaelekeza fikira kwa mahitaji ya wahubiri walio katika vikundi vyao. Huenda mpango huu ukawafaa walio wengi wa wahubiri ambao watoka kwenda shambani siku hiyo. Ikitegemea hali yao, makundi mengine yanafanya mikutano yao ya utumishi wa shambani wa mwisho-juma katika kila Funzo la Kitabu la Kundi. Kuna faida zinazoonekana waziwazi katika mpango huu. Inatambuliwa kwamba hali zinatofautiana kundi moja na jingine. Kuunganisha vikundi fulani vidogo sana huenda kukafaa nyakati nyingine. Kwa hiyo baraza la wazee linahitaji kufikiria hali ya kundi lao na kuamua ni mipango ipi itakayofaa zaidi.—Ona Huduma Yetu, kurasa 96-7.
UNGA MKONO MIKUTANO YA UTUMISHI WA SHAMBANI
3 Kutoa ushuhuda kama kikundi kunakopangwa kwa kiwango cha funzo la kitabu kunaandaa fursa nzuri kwa kiongozi kutoa msaada wa kibinafsi. Wahubiri wapya pamoja na wale ambao wana ujuzi zaidi wanaweza kunufaika kwa kufanya kazi pamoja na wazee na watumishi wa huduma.
4 Mikutano ya utumishi wa shambani wa katikati ya juma yaweza kufanyiwa kwenye Jumba la Ufalme au mahali mbalimbali panapofaa wahubiri. Iwe mikutano miwili au zaidi inafanywa inategemea hali ya kundi lenu na kupatikana kwa wazee, watumishi wa huduma au watu wengine mmoja mmoja wenye uwezo ambao wamepewa mgawo wa kutunza mikutano hiyo na kuongoza huduma ya shambani.
5 Kwa sababu ya uharaka wa nyakati, tunataka kufikia watu wengi iwezekanavyo tukiwa na ujumbe wa Ufalme. Viongozi wa funzo la kitabu na wale ambao wamepewa mgawo wa kutunza kikundi wanaweza kufanya nini ili wahakikishe kwamba wote wanatumia vizuri wakati ambao wameratibu kwa ajili ya kutoa ushuhuda wakiwa kikundi? Viongozi wanaweza kukumbuka kwamba mkutano wa utumishi wa shambani haupasi kuzidi dakika 10 mpaka 15. (Ona Huduma Yetu, ukurasa 77.) Wakati mwingi unaweza kuokolewa ikiwa eneo linagawiwa watu kabla ya kwenda shambani, hivyo kuepuka kukutana kwa vikundi vikubwa katika pembe za barabara na kuonekana kama hawana utaratibu. Wengine wameliona kuwa jambo lenye msaada kugawa sehemu za eneo kwa wahubiri wanaostahili kwa kipindi cha wakati. Hivyo, mara vikundi vinapopangwa, vinaweza kuondoka mara moja kuelekea kwenye eneo lao. Mwangalizi wa utumishi apaswa kuwa macho kutatua matatizo kwa kupanga vikundi kitengenezo ili wakati mwingi utumiwe shambani.
6 Wahubiri wengi wa muda mrefu wanakumbuka kwa furaha mambo yaliyoonwa waliyoshiriki katika muda wa miaka mingi huku wakifanya kazi pamoja na wengine katika utendaji wa kikundi. Mambo yaliyoonwa kama hayo yanatia nguvu umoja wa kundi na vifungo vya upendo wa Kikristo. Ingawa huenda nyakati nyingine kukawa na sababu nzuri kwa wahubiri wawili kufanya kazi pamoja, katika maeneo mengi, mengi yanaweza kutimizwa kwa kufanya kazi peke yako huku wengine wakitoa ushuhuda karibu karibu. Kufanya kazi peke yako katika utumishi wa shambani, mahali ambapo hali zinaruhusu, kunaturuhusu kufikia watu zaidi, na kunaweza kuwa mazoezi mazuri kwa ajili ya wakati ujao ikiwa vizuizi visivyotazamiwa vinawekwa juu ya kazi yetu ya kuhubiri. (Ona Mnara wa Mlinzi, Novemba 15, 1985, ukurasa 14, fungu 11.) Kuhukumu kuzuri, vilevile tamaa ya kutimiza mengine iwezekanavyo, kwapasa kuongoze mipango tunayofanya.
7 Mtume Paulo alitia moyo Wakristo wenzake wa siku yake ‘washike sana ungamo la tumaini letu.’ Pia, maneno yake yaliyovuviwa yanatuambia “tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; wala tusiache kukusanyika pamoja . . . bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.” (Ebr. 10:23-25) Kupitia kwa kuunga mkono mipango ya kundi letu ya kutoa ushuhuda tukiwa kikundi, na tufaulu katika kuhimiza watangazaji wa Ufalme wenzetu “katika upendo na kazi nzuri.” Tunapoendelea kufanya hivyo, tutavuna thawabu nyingi nzuri katika utumishi wa Yehova.