Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/88 uku. 2
  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • JUMA LINALOANZA AGOSTI 1
  • JUMA LINALOANZA AGOSTI 8
  • JUMA LINALOANZA AGOSTI 15
  • JUMA LINALOANZA AGOSTI 22
  • JUMA LINALOANZA AGOSTI 29
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 8/88 uku. 2

Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi

JUMA LINALOANZA AGOSTI 1

Wimbo 27 (53)

Dak. 12: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyochaguliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Tia moyo kuunga mkono utumishi wa shambani Jumapili ya kwanza ya mwezi.

Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Broshua.” Fanya mazungumzo mafupi ya mafungu 1 na 2, kisha toa maonyesho matatu yaliyotayarishwa vizuri, kila mmoja kwa kila broshua inayotolewa. Watie moyo wahubiri vijana kujifunza utoaji ulio katika fungu 4. Sihi wahubiri wajitayarishe vizuri ili wawe wenye matokeo katika kuingia kwao katika toleo. Wakumbushe kwamba broshua zinaweza kutumiwa kuanzisha mafunzo ya Biblia.

Dak. 13: “Sehemu Mpya ya Kalenda ya 1989.” Hotuba yenye idili. Eleza waziwazi jinsi ya kuagiza kalenda kama inavyoonyeshwa katika Matangazo.

Wimbo 109 (204) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA AGOSTI 8

Wimbo 101 (186)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu na shukrani kwa michango. Tia moyo wote washiriki katika kutoa ushuhuda kwa magazeti siku za Jumamosi. Tia ndani wonyesho mfupi wa kutoa magazeti ya karibuni.

Dak. 20: “Timiza Huduma Yako Kikamili.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Wakati wa kuzungumzia mafungu 3 na 4, rejeza kwenye Fahirisi chini ya “ENEO,” kichwa kidogo “kueneza,” kichwa cha pili kidogo “kwa kurudia,” ili kupata mambo yaliyoonwa kuhusu manufaa za kutumia maandishi ya nyumba kwa nyumba. Mambo yaliyoonwa ya yaliyotayarishwa mahali pa kwenu yanaweza kutumiwa pia.

Dak. 15: Uwe Msikilizaji Mzuri! Hotuba yenye kutia moyo na yenye kufundisha. Kusikiliza kuna sehemu ya muhimu katika kujifunza. (Mit. 1:5) Kufanya maendeleo kwetu tukiwa wahudumu Wakristo kunategemea sana jinsi tunavyosikiliza mikutanoni, makusanyikoni, na kuwasikiliza wazee. (Mit. 18:15) Msikilizaji mzuri hasikii tu kwa masikio yake bali pia anatoa uangalifu kwa akili zake na moyo wake. Anasukumwa na moyo wake kupata maana ya jambo na kulifanyia jambo fulani. Anamotishwa na yale anayosikia. (Mt. 13:23) Kupendezwa ni jambo la muhimu sana ili kusikiliza vizuri. Kupendezwa kwetu katika ukweli kwapasa kutusaidie tufanyie maendeleo kusikiliza kwetu mikutanoni na makusanyikoni. Tunaweza kufanya nini ili tufanyie maendeleo kusikiliza kwetu? Ona Somo 5 katika Kiongozi cha Shule ili upate madokezo zaidi. Watie moyo wote wakumbuke shauri la Yesu, “Toa uangalifu jinsi wewe unavyosikiliza.”—Luka 8:18, NW.

Wimbo 29 (57) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA AGOSTI 15

Wimbo 20 (86)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Eleza kifupi mipango ya kundi ya utumishi wa shambani. Hoji vijana ambao wametumikia wakiwa mapainia wasaidizi wakati wa Julai au Agosti. Wamenufaika jinsi gani, nao wamekuwa na shangwe zipi? Simulia kifupi mambo mazuri waliyoona katika utumishi wa shambani.

Dak. 20: “Funzo la Biblia la Jamaa—Jambo la Kwanza kwa Wakristo.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu.

Dak. 15: Hoji kikundi cha vijana mchanganyiko katika kundi. Ni matatizo gani ya mahali penu ambayo Mashahidi vijana wanakabili shuleni? Wanaweza kufanya nini kibinafsi ili washirikiane na wazazi wao kufanya funzo la Biblia liwe lenye mafanikio? Tunaweza kufanya nini tuwasaidie? Je! wao wana mradi wa kumtumikia Yehova wakati wote?

Wimbo 73 (157) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA AGOSTI 22

Wimbo 41 (77)

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Tia moyo kuunga mkono utumishi wa shambani kwa magazeti siku za Jumamosi. Toa maonyesho ya utoaji unaofaa.

Dak. 18: Tunaweza Kuwa Wenye Matokeo Zaidi Jinsi Gani? Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Pitieni pamoja na kundi njia ambazo katika hizo wote wanaweza kushiriki katika pande mbalimbali za utumishi ambamo huenda zikahitaji uangalifu. Habari zinaweza kufanyiwa uchunguzi kwa kutumia Fahirisi chini ya “HUDUMA YA SHAMBANI.” Watolee wasikilizaji madokezo yenye mafaa. Onyesho moja kufika matatu mafupi yanaweza kutumiwa ili kutoa kielezi cha mambo yaliyozungumziwa.

Dak. 17: “Je! Wakati Mmoja Wewe Ulishirikiana na Tengenezo la Yehova?” Hotuba yenye kusihi ikitolewa na mzee mwenye ujuzi, ikieleza hangaiko linalofaa la kundi kwa watu wasiotenda na jambo linaloweza kufanywa ili kuwasaidia watu wa aina hiyo ambao huenda wanajulikana kwa washiriki wa kundi.—wSW88/1/15, kur. 21-3.

Wimbo 63 (123) na sala ya kumalizia.

JUMA LINALOANZA AGOSTI 29

Wimbo 107 (190)

Dak. 5: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani upesi mwishoni mwa mwezi.

Dak. 13: Toeni broshua wakati wa Septemba. Hotuba yenye kuamsha pamoja na maonyesho. Kazia thamani ya broshua kwa watu waliomo katika eneo lenu. Dokeza hali mbalimbali ambazo katika hizo mahubiri yanaweza kutolewa. Toa wonyesho wa utoaji wa nyumba kwa nyumba kwa kutumia Kichwa cha Mazungumzo, na toa onyesho jingine moja ambalo lingefaa mahali penu.

Dak. 12: “Kuabudu Yehova kwa Umoja.” Mazungumzo.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu au hotuba kuhusu “Jinsi ya Kuwa Mzazi Mwenye Mafanikio.” Ona Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 1988, kurasa 3-6.

Wimbo 71 (138) na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki