Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/89 uku. 8
  • Kitambulisho Chetu Tukiwa Mashahidi wa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitambulisho Chetu Tukiwa Mashahidi wa Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Habari Zinazolingana
  • Maandalizi ya Kutusaidia Tujiepushe na Damu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Je, Napaswa Kuchukua Kadi ya Mkopo?
    Amkeni!—1999
  • Miaka Mia Moja ya Utawala wa Ufalme!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Uandalizi Mpya wa Kutusaidia Kujiepusha na Damu
    Huduma ya Ufalme—2006
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 8/89 uku. 8

Kitambulisho Chetu Tukiwa Mashahidi wa Yehova

Tukiwa wahudumu wa habari njema, tunajulikana waziwazi kuwa Mashahidi wa Yehova. Kushiriki kwetu utumishi wa shambani kwa kujitoa kunachochewa na upendo kwa Mungu na jirani. Hakufanywi kwa kushurutishwa na mwanadamu yeyote au tengenezo bali kulingana na utume tuliopewa na Mungu kuhubiri “habari njema” na kufanya wanafunzi. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Basi, ni jambo linalofaa wahubiri waepuke kujitambulisha wenyewe kuwa wajumbe au wawakilishi wa Sosaiti au shirika jingine lolote linalotumiwa na “mtumwa mwenye imani na mwenye uangalifu” kusongeza mbele masilahi ya Ufalme.—Mt. 24:45-47.

Aksidenti ikitokea au dharura yoyote au matatizo yakikabiliwa wakati wa kufanyia eneo fulani kazi, huenda wahubiri wakahitaji kitambulisho cha kibinafsi cha aina fulani zaidi ya kutoa jina lao pamoja na maelezo mafupi ya Kimaandiko kuhusu aina ya kazi yetu ya kidini. Ikiwa anahojiwa, au anaombwa hati, mhubiri aliyebatizwa anaweza kutumia kadi ya kitambulisho (S-65) ikiwa imetiwa sahihi na mwangalizi msimamizi, ambacho kinaonyesha kwamba mmoja anahubiri habari njema za Ufalme kwa kushirikiana na kundi la mahali ambalo jina limeandikwa kwenye kadi ile.

Akiba ya kadi za utambulishi (S-65), ambazo zinaweza kupewa wahubiri waliobatizwa kukiwa na uhitaji, zitatiwa ndani katika upakizi wa kila mwaka wa fomu za kundi katika nchi fulani fulani. Ikiwa wahubiri wowote wanatumia kadi ya kibinafsi yenye jina kuhusiana na utendaji wao wa utumishi wa shambani, hawapaswi kuandika humo kwamba wao ni wawakilishi wa Sosaiti.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki