Kitambulisho Chetu Tukiwa Mashahidi wa Yehova
Tukiwa wahudumu wa habari njema, tunajulikana waziwazi kuwa Mashahidi wa Yehova. Kushiriki kwetu utumishi wa shambani kwa kujitoa kunachochewa na upendo kwa Mungu na jirani. Hakufanywi kwa kushurutishwa na mwanadamu yeyote au tengenezo bali kulingana na utume tuliopewa na Mungu kuhubiri “habari njema” na kufanya wanafunzi. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Basi, ni jambo linalofaa wahubiri waepuke kujitambulisha wenyewe kuwa wajumbe au wawakilishi wa Sosaiti au shirika jingine lolote linalotumiwa na “mtumwa mwenye imani na mwenye uangalifu” kusongeza mbele masilahi ya Ufalme.—Mt. 24:45-47.
Aksidenti ikitokea au dharura yoyote au matatizo yakikabiliwa wakati wa kufanyia eneo fulani kazi, huenda wahubiri wakahitaji kitambulisho cha kibinafsi cha aina fulani zaidi ya kutoa jina lao pamoja na maelezo mafupi ya Kimaandiko kuhusu aina ya kazi yetu ya kidini. Ikiwa anahojiwa, au anaombwa hati, mhubiri aliyebatizwa anaweza kutumia kadi ya kitambulisho (S-65) ikiwa imetiwa sahihi na mwangalizi msimamizi, ambacho kinaonyesha kwamba mmoja anahubiri habari njema za Ufalme kwa kushirikiana na kundi la mahali ambalo jina limeandikwa kwenye kadi ile.
Akiba ya kadi za utambulishi (S-65), ambazo zinaweza kupewa wahubiri waliobatizwa kukiwa na uhitaji, zitatiwa ndani katika upakizi wa kila mwaka wa fomu za kundi katika nchi fulani fulani. Ikiwa wahubiri wowote wanatumia kadi ya kibinafsi yenye jina kuhusiana na utendaji wao wa utumishi wa shambani, hawapaswi kuandika humo kwamba wao ni wawakilishi wa Sosaiti.