Endelea Kusema, “Njoo!” kwa Wale Wenye Mwelekeo wa Kusikiliza
1 Yesu alikazia uhitaji wa watu kusikiliza ujumbe wa ukweli kwa umakini. (Mt. 11:15; 13:9, 43) Alijua kwamba lilikuwa jambo la muhimu wapate maana ya fundisho lake, kwa kuwa alikuwa akitoa maarifa ambayo yangeongoza wasilizaji wenye uthamini kwenye uhai wa milele.—Yoh. 17:3.
2 Maarifa hayo yenye kutoa uhai ni sehemu ya muhimu ya “maji ya uzima” ambayo sasa yanapatikana kwa wenye kiu. (Ufu. 22:17) Kama inavyoonyeshwa na maneno ya Yohana, si kitu kinachopatikana kwa wachache waliopendelewa peke yao, wala si kitu kinachouzwa kwa wale walio na pesa na kunyimwa wale wasio nazo. Wote ambao sasa wanaona kiu cha uadilifu wanahitaji kutiwa moyo wajifaidi na zawadi ya ukarimu ya Yehova iliyo ya bure. (Isa. 55:1) Je! wewe umo miongoni mwa mamilioni ambao leo wanasema, “Njoo!” kwa wale wenye mwelekeo wa kusikiliza?
UNAVYOWEZA KUSEMA, “NJOO!”
3 Mei ni mwezi wa pili wa kampeni yetu ya uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi. Kungekuwa na chombo gani bora zaidi cha kuelekezea fikira uandalizi wa ajabu wa Yehova wa uhai? Kufunuliwa kwa njia mbovu za Babuloni Mkubwa kunakaziwa kwa njia ya pekee. Mnara wa Mlinzi unaweza kuwasaidia wengi wawekwe huru na ushirikina na mafundisho bandia ya kidini. Wewe unapata fursa gani za kutoa uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi?
4 Njia nzuri ya kutoa uandikishaji ni nyumba kwa nyumba. Lakini pia kuna njia nyingine nyingi, kama vile wakati unapofanya ziara za kurudia au kuwapelekea matoleo ya karibuni watu unaopelekea magazeti kwa ukawaida. Wahubiri fulani wanapata mafanikio kupata maandikisho kutoka kwa watu wanaopendezwa wanaokutana nao katika kazi ya barabarani. Tunaweza kuwatia moyo wengine ambao tayari ni waandikishaji wawapelekea marafiki na watu wa ukoo zawadi ya uandikishaji. Huenda wewe pia ukataka kutoa zawadi chache za uandikishaji. Uandikishaji unaweza pia kutolewa kwa wafanya biashara unaofahamiana nao, wafanya kazi wenzi, au wanashule wenzako. Unaweza kufikiria uwezekano mwingine.
ENDELEA KUSEMA, “NJOO!”
5 Endelea kuonyesha upendezi katika kuwasaidia wale ambao waliandikisha katika Aprili. Hakikisha unawarudia upesi. Hakikisha kwamba wanapokea magazeti. Kwenye ziara hizo, unaweza kuonyesha makala fulani hasa na uwatie moyo waisome. Labda unaweza hata kuanzisha mafunzo ya Biblia nao na udokeze kwamba wahudhurie mikutano ya kundi pamoja nawe. Kwa kuwaonyesha upendezi wa moyo mweupe, huenda wakaitikia kwa kupendelea na wakasukumwa wafanye maendeleo ya kiroho.
6 Tarakimu za hudhurio la Ukumbusho katika Afrika Mashariki zinaonyesha kwamba watu zaidi ya 24,000 ambao bado si wahubiri wa habari njema wanahudhuria tukio hili la maana sana. Je! unafahamu watu hawa wanaopendezwa katika kundi lenu ni akina nani? Je! wao ni waandikishaji wa Mnara wa Mlinzi? Ni nini kinachofanywa ili kuwasaidia wakue kiroho?
7 Ule mwaliko, “Njoo!” unatolewa kwa watu wa mataifa yote. Kupitia Mwana wake Yesu, kwa neema Yehova amefanya zawadi ya uhai ipatikane kwa wote wanaoitikia mwaliko, “Njoo!” na ‘uyatwae maji ya uzima bure.’ Je! wewe utakuwa na ushiriki kamili kuwatoleo wengine mwaliko huo wakati wa Mei.