Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/89 kur. 1-3
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia ya Nyumbani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia ya Nyumbani
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Vichwa vidogo
  • UNAWEZA KUFANYA HIVYO
  • KUENDELEZA KUPENDEZWA KULIKOONYESHWA MWANZONI
  • ONO ZURI AJABU
Huduma Yetu ya Ufalme—1989
km 5/89 kur. 1-3

Kuongoza Mafunzo ya Biblia ya Nyumbani

1 Kuwafundisha wengine ukweli kuhusu Yehova, Yesu Kristo, na Ufalme ni pendeleo la ajabu. (1 Kor. 3:6-9) Mwaka uliopita wastani wa mafunzo ya Biblia ya nyumbani 16,342 yaliongozwa kila mwezi katika Afrika Mashariki! Je! wewe unaona shangwe ya pendeleo hili la ajabu?

UNAWEZA KUFANYA HIVYO

2 Ikiwa huongozi funzo la Biblia kwa ukawaida, sali kuhusu jambo hilo na uliweka kuwa mradi wa kufanyia kazi. Hakikisha unafuatia kupendezwa kokote kunakopatikana nyumba kwa nyumba na katika sehemu nyingine za huduma. Tumia vizuri kikaratasi cha nyumba kwa nyumba kwa kuandika kwa uangalifu habari zinazohitajika, hasa habari iliyompendeza mwenye nyumba. Kisha hakikisha unarudi upesi kabla mbegu za ukweli hazijanyakuliwa na hasimu. (Luka 8:12) Kwa kufuatia madokezo haya ya msingi wengi wetu wanaweza kusaidia watu wenye mioyo myeupe kupitia funzo la Biblia, ili wapate maarifa ya kujua Mungu na Kristo.—Yoh. 17:3.

KUENDELEZA KUPENDEZWA KULIKOONYESHWA MWANZONI

3 Ni sababu gani zinazofanya watu tunaoanza mafunzo nao wayakomeshe baada ya muda mfupi? (Mt. 13:18-23) Tunaweza kufanya nini kuendeleza kupendezwa kulikoonyeshwa? Kwanza, hakikisha unaanza na habari au maswali ambayo mwenye nyumba anapendezwa nayo. Katika visa fulani habari yenye upendezi inaweza kuwa sehemu fulani ya Kichwa cha Mazungumzo au inaweza kuwa jambo jingine ambalo limemsumbua mwenye nyumba. Tambua anapendezwa na nini na ufuatie jambo hilo. Kisha jaribu kukuza tamaa yao kuhusu habari ambayo itazungumziwa katika ziara itakayofuata kwa kuzusha swali moja au mawili kuhusu habari hiyo. Maswali yaachwe bila kujibiwa kwa kuwa unataka kuamsha tamaa kwa ziara inayokuja. Hakikisha kwamba mwenye nyumba anajifunza jambo fulani lenye thamani katika kila ziara. Onyesha jinsi habari hiyo ikitumiwa itamnufaisha mwenye nyumba au washiriki wa jamaa yake. Au, onyesha jinsi ukweli unavyoweka mtu huru na imani na mafundisho bandia. (Yoh. 8:31, 32) Pia, uwe mchangamfu, mwenye urafiki, mwenye idili na usifuate sana kawaida za funzo. Onyesha unapendezwa sana kibinafsi na mwenye nyumba na jamaa yake.

4 Ili kuendeleza upendezi katika funzo tafadhali epuka kutoa hotuba kwa kuzungumza peke yako bila kumwingiza mwenye nyumba. Kumbuka kuuliza maswali yenye utambuzi, kama alivyofanya Yesu. Hata hivyo, uwe mwangalifu usiulize maswali ya kumwaibisha mwenye nyumba au magumu. Utataka kuepuka kufanya funzo au mazungumzo yawe yenye kutatanisha au yaonekana magumu. Usifanye hali ionekane kama ya darasani kana kwamba mwanafunzi amerudia shule ya msingi. Uwe mwangalifu usikae kwa muda mrefu zaidi ya ulivyoahidi mwenye nyumba. Kadiri funzo liendeleavyo kwa kawaida kipindi cha kujifunza kitakuwa cha saa moja hivi. Mara nyingi sura moja inaweza kumalizwa katika kila ziara, lakini hii inategemea uwezo wa mwanafunzi. Kwa ukawaida, unaweza kumaliza zaidi ya mafungu 3 au 4 katika kila ziara. Kujifunza polepole sana na kutumia mambo yote katika kila fungu kunaweza kufanya funzo lisipendeze na liwe lenye kuchosha mwanafunzi mwenye maendeleo. Kwa hiyo endeleza funzo kwa utaratibu unaolingana na uwezo wa mwanafunzi kushika na kuelewa habari. Ikiwa jambo kuu au fungu limefahamika basi endelea kwenye jambo linalofuata. Kadiri mwanafunzi anavyojitayarisha vizuri zaidi mapema ndivyo habari zaidi itazungumzwa katika kila ziara. Basi, mtie moyo ajitayarishe mapema na atoe majibu kwa maneno yake mwenyewe.

ONO ZURI AJABU

5 Kuongoza funzo la Biblia la nyumbani ni mojapo maono yenye kuleta shangwe zaidi ambayo tunaweza kupata katika huduma yetu. (Mt. 28:19, 20) Yehova Mungu na atege sikio kwa sala zetu na kubariki jitihada zetu zenye bidii za kuongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani yenye maendeleo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki