Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA MEI 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Tangaza mipango ya utumishi wa shambani kwa mwisho-juma, na utie moyo vikundi vya jamaa vishiriki katika huduma ya nyumba kwa nyumba.
Dak. 17: “Endelea Kusema, ‘Njoo!’ kwa Wale Wenye Mwelekeo wa Kusikiliza.” Maswali na majibu. Maono yaliyochaguliwa ya mahali penu yasimuliwe wakati unavyoruhusu. Kazia kutoa uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! katika kila pindi inayofaa. Watie moyo wahubiri wafanye ziara za kurudia bila kuchelewa na wajitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani pamoja na watu wenye kupendezwa.
Dak. 18: Utumishi wa Habari wa Hospitali. Ishughulikiwe na mzee anayestahili. Pitia mambo makuu kutoka makala “Kufanya Mambo Yanayohitajiwa Sana Ili Kupendeza Mungu,” katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1988. Ripoti zinaonyesha kwamba wengine bado hawajazungumza na madaktari wao kama ilivyoonyeshwa humo. Uliza: Je! umejaza kikamili na kutia sahihi na kuwaomba wengine watie sahihi katika kadi yako ya Hati ya Kitiba? Kazia kwamba wazee wa mahali penu wana daraka la kutembelea wahubiri wagonjwa na wenye kulazwa hospitalini na kutimiza mahitaji yao. (1 Pet. 5:2; 1 The. 2:7, 8) Watie moyo wote wafahamiane kikamili na habari iliyochapishwa katika Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1989, kurasa 30-1, na Awake! ya Februari 22, 1989, kurasa 26-7.
Wimbo 216 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA MEI 8
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 20: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia ya Nyumbani.” Maswali na majibu. Mhubiri au painia mwenye uwezo aonyeshe jinsi ya kutumia maswali kuamsha kupendezwa katika ziara itakayofuata. Watie moyo wote washiriki katika kazi ya maana sana ya kufanya wanafunzi.
Dak. 15: Kutumia Broshua, Mashahidi wa Yehova Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote. Utangulizi mfupi na maelezo ya kumalizia yakionyesha umaana wa kutumia dakika kama 10 katika kila kipindi cha funzo ili kuzungumzia habari zilizomo katika broshua hatua kwa hatua. Kazia kwamba matumizi ya broshua yanasaidia mwanafunzi afahamiane na tengenezo la ulimwenguni pote. Wonyesho ukitolewa na mhubiri anayestahili akizungumzia habari pamoja na mwanafunzi wa Biblia chini ya kichwa “Mikutano ya Kuhimizana Ili Kupenda na Kufanya Kazi Nzuri.”
Wimbo 211 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA MEI 15
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Sifu kundi kwa msaada wa kimwili, na usome shukrani za uthamini kwa michango iliyopokewa na Sosaiti. Onyesha mipango ya utumishi wa shambani kwa mwisho-juma, na utie moyo wahubiri wafanye kazi pamoja na vikundi Jumamosi na Jumapili.
Dak. 20: “Kuingiza Sheria ya Mungu ‘Ndani ya Sehemu Zetu za Ndani.’” Kipindi cha maswali na majibu kwa mafungu manne ya kwanza. Kisha ndugu anayeshughulikia sehemu hii aalike jukwaani wahubiri wawili wenye kielelezo kizuri kwa mazungumzo ya watatu juu ya mafungu 5-7. Waweza kuomba maelezo mafupi ya uthamini kwa vichapo vipya. Kikundi kinaweza kueleza jinsi wao au wengine wamenufaika na funzo la kibinafsi na kufanya utafiti.
Dak. 12: Hotuba juu ya “Mahari—Wakristo Wawe na Rai Gani Kuihusu?” kutoka Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1989. Fanya matumizi ya mahali penu inavyohitajiwa.
Dak. 5: Maono. Wahubiri wasimulie maono mawili au matatu mafupi kuhusu kupendezwa kulikopatikana wakati wa kampeni ya uandikishaji.
Wimbo 92 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA MEI 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Sanduku la Swali. Watie moyo wahubiri waende kwenye utumishi wa shambani mwisho-juma.
Dak. 20: Arusi na Ndoa Zinazoletea Yehova Staha. Pitio la mambo makuu kutoka Mnara wa Mlinzi wa Septemba 15, 1984, kurasa 8, 9, 13-19. Pia tia ndani mambo makuu kutoka Huduma Yetu ya Ufalme, Aprili 1976, kurasa 7 na 8. (Habari hizo hizo zinapatikana katika broshua inayohusu Desturi Zisizo za Kikristo, mafungu 24-29.)
Dak. 15: Vikumbusha vya Kila Siku kwa Kujenga Hali ya Kiroho. Ndugu anayestahili anazungumza pamoja na wahubiri wawili au watatu walio kielelezo kizuri jinsi watu mmoja mmoja na vikundi vya jamaa wananufaishwa na vikumbusha vya kila siku kama vile andiko la kila siku, andiko la mwaka, na habari zilizo katika kalenda. Tunahitaji vikumbusha kutoka kwa Yehova. (Zab. 119:2; Mdo. 17:11) Onyesha jinsi vikumbusha vya mara kwa mara vinaweza kututia moyo na kuthibitika kuwa vyenye manufaa katika huduma.
Wimbo 91 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA MEI 29
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wahubiri wote waende katika utumishi wa shambani siku ya magazeti Jumamosi. Toa wonyesho wa sekunde 30 hadi 60 wa utoaji wa magazeti ambao ungefaa katika eneo la kwenu.
Dak. 20: “Chanzo cha Amani na Usalama wa Kweli.” Mwangalizi wa utumishi afanye pitio la Kichwa cha Mazungumzo kipya kuanzia Juni pamoja na wasikilizaji. Mhubiri aliyejitayarisha vizuri atumie madokezo yanayofuata katika wonyesho wa Kichwa kipya:
“Tunapata kwamba karibu kila mtu anasema kwamba anataka kuishi katika ulimwengu usio na vita na ukosefu wa usalama. Hata hivyo, katika karne hii peke yake kumekuwa na mamia ya vita, kutia na vita viwili vya ulimwengu. Kwa nini amani yenye kudumu ni ngumu sana kupata? Hata Biblia ilitabiri kwamba amani yoyote yenye kutokezwa na mwanadamu haingekuwa yenye kudumu kama tunavyosoma kwenye 1 Wathesalonike 5:2, 3: (Soma.) Kama mstari wa 2 unavyoonyesha, uharibifu wa ghafula utatokea kutoka mikononi mwa Mungu anapokomesha uovu wote. Kisha Mungu mwenyewe atatokeza amani na usalama wenye kudumu kama ule unaosimuliwa kwenye Mika 4:3, 4: (Soma.) Unafikiri utimizo wa unabii huu utamaanisha nini kwa aina ya binadamu yenye kuteseka? (Kazia kwamba hii haimaanishi kutokuwako kwa vita tu, bali pia ulimwengu usio na kufuli na makomeo, n.k.) Je! wewe ungependa kuona unabii huu ukitimizwa katika wakati wetu?” Kisha unaweza kufungua picha iliyo kwenye ukurasa 98 wa kitabu Amani ya Kweli, toa maelezo kuihusu, kisha elekeza fikira kwenye taarifa moja au mbili zinazofaa zilizochaguliwa kwenye kurasa zinazofuata za kitabu hicho ambazo zinaonyesha tumaini lenye kutegemeka la amani na usalama wa duniani pote.
Dak. 15: “Kutangaza Habari Njema—Kwa kitabu Amani ya Kweli.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu.
Wimbo 156 na sala ya kumalizia.