Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/90 uku. 3
  • Kuonyesha Tegemeo Katika Yehova kwa Kupainia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuonyesha Tegemeo Katika Yehova kwa Kupainia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • PITIA TENA MASTAKIMU (HALI) ZA KIBINAFSI
  • Utumishi wa Painia—Je, Wakufaa Wewe?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Kutembea kwa Nafsi Yote katika Njia ya Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Mapainia Hutoa na Kupokea Baraka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Je! Waweza Kumtumikia Yehova Ukiwa Painia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 2/90 uku. 3

Kuonyesha Tegemeo Katika Yehova kwa Kupainia

1 Kuweka masilahi ya Ufalme kwanza kunataka tegemeo katika Yehova. (Zab. 56:11; Mit. 3:5; Mt. 6:33) Ni lazima tugeuze akili zetu mbali na yale ambayo ulimwengu huyaona kuwa ya maana na kukaza fikira kwenye thamani za kiroho. Ingawa ulimwengu unavutia kwenye tamaa ya mambo ya kimwili, Yehova anatusihi turidhike na mambo ya maana kweli kweli.—1 Tim. 6:8; Flp. 1:10.

2 Hasa hicho ni takwa gumu kwa vijana Wakristo wanaotaka kuchukua amri za Yehova kwa uzito. Huenda wakakazwa na walimu wao na marika wao shuleni wanaoiona elimu ya juu kuwa ya lazima ili kufaulu maishani. Wajapotambua wana mahitaji ya kimwili, kwa hekima vijana wengi Wakristo wanakinza mkazo huo na kuchagua huduma ya painia kuwa kazi-maisha yao. Wakiitegemea katika ahadi za Yehova, wanamtegemea atimize mahitaji yao.—Zab. 62:2; 68:19; 1 Tim. 5:8; 6:9, 10.

PITIA TENA MASTAKIMU (HALI) ZA KIBINAFSI

3 Mnara wa Mlinzi wa Aprili 15, 1983, ulitia moyo kila mmoja wetu aulize: “Je! mimi naweza kweli kupata sababu nzuri ya kujitetea mbele za Yehova juu ya kinachofanya nisiwe painia?” Kwa wazi, wengi wakati huo hawakuwa katika hali ya kupainia. Lakini hawakuvunjika moyo, wakijua kwamba utumishi wa moyo wote wa kiasi chochote sikuzote unakubalika kwa Yehova. (Mika 6:8; 2 Kor. 8:12) Baadaye, kwa kadiri mastakimu za kibinafsi zilibadilika, ufikirio mwingine kwa njia ya sala wa makala hiyo ya Mnara wa Mlinzi wa 1983 umewezesha wengine wawe kati ya maelfu ya watu ambao hivi karibuni zaidi wamechukua utumishi wa painia wa kawaida.

4 Ikiwa mastakimu za kibinafsi zilikuzuia usiingie utumishi wa painia wakati taarifa iliyo juu ilipochapishwa mwaka 1983, je! mastakimu zako zimebadilika? Katika Afrika ya Mashariki, maombi ya upainia 291 yalishughulikiwa mwaka jana! Bila shaka wengi wa waombaji hao walitaka kuwa mapainia hapo mbeleni lakini walilazimika kungojea badiliko la mastakimu.

5 Katika visa fulani, badiliko linalohitajiwa huenda likahusu mtazamo wa kiakili wa mtu juu ya utumishi wa painia. Au huenda ikatia ndani kufanya ratiba nzuri kwa ajili ya utumishi. Nyakati nyingine badiliko katika madaraka na majukumu ya kibinafsi lahitajiwa ili kufungua njia ya kuingia utumishi wa painia. Kwa hiyo, ni vizuri kufanya hilo kuwa jambo la kawaida la sala kwa Yehova pamoja na kujiichangua wenyewe na mastakimu zetu kwa unyofu. Maelfu wamefanya hivyo nao wanashangilia sasa baraka za utumishi wa painia.

6 Ikiwa kupima kwa unyofu mastakimu zako kunadokeza waweza kuwa mmoja anayeweza kuanza kupainia katika wakati ujao usio mbali sana, kwa nini usianze utumishi wa painia msaidizi kwa mfululizo sasa? Baada ya miezi michache, yaelekea utasitawisha ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia. Jambo hilo laweza kukusaidia uingie kwa ushwari utumishi wa painia wa kawaida, labda kabla ya kuanza mwaka wa utumishi mpya.

7 Yehova anatimiza mambo makubwa katika siku za mwisho za mfumo mbovu uliopo. Sasa ndio wakati kwa sisi sote kumkaribia yeye na kulibariki jina lake “mchana kutwa.” (Zab. 145:2, NW; Yak. 4:8) Mastakimu zako zikikuruhusu kufanya hivyo na ukistahili, acha utumishi wa painia uwe ushuhuda mwingine wa tegemeo lako katika Yehova.—Zab. 94:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki