Sanduku la Swali
● Ni ratiba gani inayopasa kufuatwa katika mkutano wa pekee unaotia ndani Funzo la Kitabu wakati wa juma la ziara ya mwangalizi wa mzunguko?
Wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko, mipango hufanywa kwa ajili ya kundi lote kukusanyika kwenye Jumba la Ufalme kwa ajili ya mkutano wa pekee ambao unatia ndani Funzo la Kitabu la Kundi, mfikirio wa habari ya Kimaandiko na ya kitengenezo yenye kichwa “Ukae Katika Mambo Yale Uliyofundishwa,” na hotuba ya utumishi ikitolewa na mwangalizi wa mzunguko. Mkutano huu kwa kupendelea hufanywa Alhamisi au Ijumaa au siku na wakati ambao Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi hufanywa kwa kawaida.
Mkutano huo huanza na wimbo na sala, na kisha mmoja wa wazee huongoza Funzo la Kitabu la Kundi la dakika 45. Jitihada yapasa kufanywa ili kumaliza habari yote iliyogawiwa juma hilo, ikihakikishwa mafungu yote yanasomwa, kama ambavyo kwa desturi hufanywa katika funzo la kawaida la kila juma. Funzo la Kitabu la Kundi lafuatwa na kuimba wimbo mwingine wa Ufalme. Kisha mwangalizi wa mzunguko hutumia dakika 30 ili kuongoza kisehemu “Ukae Katika Mambo Yale Uliyofundishwa.” Baada ya hilo, yeye hutoa hotuba ya utumishi ya dakika 30 iliyorekebishwa hasa kulingana na mahitaji ya kundi linalotumikiwa. Katika hotuba ya utumishi, yeye hutoa pongezi na ushauri unaofaa kwa kusudi la kujenga kundi na kutia moyo akina ndugu wabaki thabiti katika utumishi wa Ufalme.
Mkutano huo humaliziwa kwa wimbo na sala. Nyimbo zote zinazotumiwa zitachaguliwa na mwangalizi wa mzunguko. Programu yote, kutia ndani nyimbo na sala, haipasi kuzidi saa mbili.
Mpango huu ulioanzishwa katika 1977 umechangiza mengi katika kufanya ziara ya mwangalizi wa mzunguko kuwa jambo maalumu kwa ajili ya shangwe na manufaa ya kundi lote na kwa ajili ya wahubiri mmoja mmoja wanaohudhuria na kushiriki katika uandalizi huu mzuri wa tengenezo la Yehova.