Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/90 uku. 7
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Kwa Nini Mavazi na Mwonekano Wetu Ni Muhimu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 8/90 uku. 7

Sanduku la Swali

● Kwa nini twapaswa kutoa uangalifu wa pekee kwa mavazi na mapambo yetu tunapozuru Betheli ya Brooklyn, Watchtower Farms, na vifaa vyote vya tawi ulimwenguni kote?

Wakristo wanatazamiwa wadumishe sura inayofaa. Mavazi na mapambo yetu nyakati zote yapasa kuonyesha uungwana na heshima inayostahili watumishi wa Yehova Mungu. Ndivyo ilivyo hasa tunapozuru Betheli ya Brooklyn, Watchtower Farms, na maofisi ya tawi na vifaa vyayo kuzunguka ulimwengu. Kikizungumza juu ya umaana wa mavazi na mapambo yanayofaa Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu chaeleza juu ya uhitaji wa usafi wa kimwili na mavazi na mapambo yenye kiasi wakati wa kushiriki katika huduma ya shambani na kuhudhuria mikutano ya kundi. Kisha, kwenye ukurasa 131, fungu 2, chataarifu hivi: “Jambo lilo hilo lingehusu wakati wa kutembelea makao ya Betheli katika Brooklyn au katika yo yote ya afisi za tawi za Sosaiti. Kumbuka, jina Betheli maana yake ni ‘Nyumba ya Mungu,’ hivyo mavazi yetu, kujipamba kwetu na mwenendo wetu umepasa uwe namna ile ile tunayotazamiwa kuwa tunapohudhuria mikutano ya ibada kwenye Jumba la Ufalme.”

Mtume Paulo alisema kwamba sisi ni “tamasha kwa dunia; kwa malaika na wanadamu.” (1 Kor. 4:9) Kwa hiyo, mavazi na mapambo yetu yapasa kuwa na uvutano chanya juu ya wengine kuhusu namna wanavyoona ibada ya kweli ya Yehova. Hata hivyo, imeonekana kwamba baadhi ya ndugu na dada, wanapozuru matawi ya Sosaiti, huwa na mbetuko wa kuvaa mavazi ya kivivi hivi mno. Mavazi hayo hayafai wakati wa kuzuru vifaa vya tawi. Katika jambo hili, kama ilivyo katika sehemu nyinginezo za maisha ya Mkristo, twataka kudumisha viwango vile vile vya juu vinavyopambanua watu wa Mungu kuwa tofauti na ulimwengu kwa kufanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu. (Rum. 12:2; 1 Kor. 10:31) Pia ni vema kusema na wanafunzi wa Biblia wetu na wengine ambao huenda wakawa wanazuru Betheli ya Brooklyn au yoyote ya maofisi ya tawi ya Sosaiti kwa mara ya kwanza kuwakumbusha juu ya umaana wa kutoa uangalifu kwa mavazi na mapambo yanayofaa.

Kwa hiyo wakati wa kuzuru vifaa vya Sosaiti, jiulize: ‘Je! kuvaa na kujipamba kwangu ni kwenye kiasi? (Mik. 6:8) Je! kunaangaza vizuri kwa Mungu ninayeabudu? Je! wengine wangekengeushwa au kuudhiwa na sura yangu? Je! mimi nawekea wengine wanaoweza kuwa wakizuru kwa mara ya kwanza kielelezo kinachofaa?’ Sikuzote na ‘tuyapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu katika mambo yote.’—Tito 2:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki