Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/98 uku. 7
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Kwa Nini Mavazi na Mwonekano Wetu Ni Muhimu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 3/98 uku. 7

Sanduku La Swali

◼ Kwa nini twapaswa kukazia uangalifu wa pekee mavazi na mapambo yetu tunapozuru majengo ya Sosaiti katika Brooklyn, Patterson, na Wallkill, New York, na ofisi nyinginezo za tawi ulimwenguni?

Wakristo wanatazamiwa wadumishe adabu inayofaa. Nyakati zote mavazi na mapambo yetu yapaswa kuonyesha mwenendo mwema na adhama inayofaa watumishi wa Yehova Mungu. Inakuwa hivyo hasa tunapozuru majengo ya Sosaiti katika New York na kwenye ofisi nyinginezo za tawi ulimwenguni.

Katika 1998, mikusanyiko ya wilaya na ya kimataifa itafanywa. Maelfu ya ndugu zetu kutoka nchi nyingi yatazuru makao makuu ya Sosaiti katika New York na vilevile ofisi za tawi katika nchi nyinginezo. Tunapozuru majengo haya, na pia nyakati nyinginezo, twahitaji ‘kujipendekeza wenyewe kuwa wahudumu wa Mungu katika kila njia,’ kutia na mavazi yetu na mapambo yetu yafaayo.—2 Kor. 6:3, 4.

Katika kuzungumzia mavazi na mapambo yafaayo, kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu hueleza uhitaji wa usafi wa kimwili na mavazi na mapambo yenye kiasi tunaposhiriki katika huduma ya shambani na kuhudhuria mikutano ya Kikristo. Kisha, kwenye ukurasa wa 131, fungu la 2, husema: “Jambo ilo hilo lingehusu wakati wa kutembelea makao ya Betheli katika Brooklyn au katika yo yote ya afisi za tawi za Sosaiti. Kumbuka, jina Betheli maana yake ni ‘Nyumba ya Mungu,’ hivyo mavazi yetu, kujipamba kwetu na mwenendo wetu umepasa uwe namna ile ile tunayotazamiwa kuwa tunapohudhuria mikutano ya ibada kwenye Jumba la Ufalme.” Kiwango kilekile cha juu chapasa kushikiliwa na wahubiri wa Ufalme kutoka eneo la kwenu na wale watokao mbali vilevile ambao wamekuja kuona na kushirikiana na washiriki wa familia ya Betheli na kuzuru majengo ya ofisi ya tawi.

Kuvaa kwetu kwapaswa kuwavutie wengine wawe na maoni yanayofaa juu ya ibada ya kweli ya Yehova. Hata hivyo, imeonekana kwamba wanapozuru majengo ya Sosaiti, baadhi ya akina ndugu na dada huelekea kuvalia kiholela kupita kiasi. Kuvalia hivyo hakufai tunapozuru yoyote ya makao ya Betheli. Kuhusu jambo hili, kama ilivyo katika sehemu nyingine zote za maisha yetu ya Kikristo, twataka kudumisha viwango vilevile vya juu vinavyotofautisha watu wa Mungu na ulimwengu katika kufanya mambo yote kwa utukufu wa Mungu. (Rom. 12:2; 1 Kor. 10:31) Pia inafaa kuongea na wanafunzi wetu wa Biblia na wengine ambao huenda wakazuru Betheli kwa mara ya kwanza na kuwakumbusha umaana wa kukazia uangalifu mavazi na mapambo yafaayo.

Kwa hiyo unapozuru majengo ya Sosaiti, jiulize: ‘Je, mavazi yangu na mapambo yangu ni yenye kiasi?’ (Linganisha Mika 6:8.) ‘Je, yanamdhihirisha ifaavyo Mungu ninayeabudu? Je, wengine watakengeushwa fikira au wataudhika kwa sababu ya sura yangu? Je, ninaweka kielelezo bora kwa wengine ambao huenda wakawa wanazuru kwa mara ya kwanza?’ Sikuzote, na ‘turembe fundisho la Mwokozi wetu, Mungu, katika mambo yote,’ kwa mavazi na mapambo yetu.—Tito 2:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki