Sanduku La Swali
◼ Watu wanapaswa kuvaaje na kujipambaje wanapotembelea Betheli?
Tunapotembelea Betheli, iwe twataka kuona majengo hayo au kutembelea washiriki wa familia ya Betheli, “mavazi yetu, kujipamba kwetu na mwenendo wetu umepasa uwe namna ile ile tunayotazamiwa kuwa tunapohudhuria mikutano ya ibada kwenye Jumba la Ufalme.” (om-SW 131) Hata hivyo, imeonekana kwamba akina ndugu na dada wengine wanapotembelea ofisi za tawi wanapita kiasi katika kuvaa mavazi yasiyo rasmi. Hiyo haifai. Sura yetu yapaswa kuwa mfano mzuri, yenye mpangilio mzuri na kiasi, tukionyesha heshima na adhama ambayo watumishi wa Yehova Mungu wanapaswa kuwa nayo.—1 Tim. 2:9, 10.
Hilo ni jambo la maana hasa tunapotembelea Betheli hizo kwa sababu watu wengi wasio Mashahidi wanatazama wanaotembea huko. Watazamaji hao huenda wakawa na maoni fulani kuhusu watu wa Mungu na tengenezo lake ikitegemea kile wanachoona. Ingefaa kuongea na wanafunzi wa Biblia pamoja na wale ambao huenda wanapanga kutembea ili kuwakumbusha umuhimu wa kukazia fikira mavazi na mapambo yanayofaa. Familia ya Betheli itathamini sana mkifanya hivyo.
Tukiwa wahudumu Wakristo, lazima tuwe waangalifu ili sura yetu isiwakwaze wengine. (2 Kor. 6:3, 4) Badala yake, kwa kujipamba ifaavyo, sikuzote na ‘turembe fundisho la Mwokozi wetu, Mungu, katika mambo yote.’—Tito 2:10.