Habari za Kitheokrasi
◆ Kuwekwa wakfu kwa majengo ya Makao ya Betheli, Ofisi, na kiwanda katika Argentina kulifanywa katika Jumamosi, Oktoba 27. Kilele kisichopata kufikiwa cha wahubiri 83,936 kilifikiwa wakati wa mwezi huo.
◆ Vilele vipya vya wahubiri viliripotiwa katika Austria, Ugiriki, na Switzerland.
◆ Cyprus ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 1,286 katika Oktoba. Jumba la Ufalme jingine lilikamilishwa huko.
◆ Grenada ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 425 katika Oktoba.
◆ Guam iliripoti kilele kisichopata kufikiwa cha wahubiri 383 katika Oktoba. Jambo kuu katika mwezi huo lilikuwa kusanyiko la mzunguko. Kulikuwako kilele cha hudhurio cha 590, na 7 wakabatizwa.
◆ Ureno iliripoti kilele kisichopata kufikiwa cha wahubiri 37,308 katika Oktoba. Kilele cha mapainia wa kawaida 1,378 kilifikiwa pia.
◆ Romania ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri katika Septemba. Walikuwako 19,734 wakiripoti—ongezeko la asilimia 16 kupita Septemba 1989.
◆ Tahiti ilikuwa na kilele cha wahubiri 1,190 katika Oktoba. Hilo lilikuwa ongezeko la asilimia 9 na kilele chayo mfululizo cha 36.
◆ Katika Oktoba vilele vipya vya zaidi ya saa 70,000 na magazeti zaidi ya 100,000 viliripotiwa na wale wahubiri 1,755 katika Taiwan. Wahubiri wa kundi walikuwa na wastani wa saa 13.2 na magazeti 19.1.
◆ Zimbabwe ilikuwa na kilele cha wahubiri 18,902 katika Oktoba. Kulikuwako mafunzo ya Biblia nyumbani 22,114 yaliyoongozwa.
◆ “Lugha Iliyo Safi” Mikusanyiko ya Wilaya 11 ilifanywa katika Kenya, Tanzania, na Uganda kukiwa na jumla ya hudhurio la 20,537 na 553 wakabatizwa. Kenya ilikuwa na mikusanyiko minne na kilele cha hudhurio cha 12,913 na 310 waliobatizwa; kilele cha hudhurio cha Tanzania kilikuwa 5,607 na 185 wakabatizwa; na mikusanyiko mitatu ya Uganda ilivutia kilele cha hudhurio cha 2,017 na 58 wakabatizwa.