Habari za Kitheokrasi
◆ Barbados ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 1,800 katika Septemba.
◆ Cote d’Ivoire ilianza mwaka mpya wa utumishi katika Septemba ikiwa na wahubiri 3,465, wakiripoti kilele chao mfululizo cha 12. Akina ndugu huko wanasaidia pia akina ndugu na dada wengi wakimbizi wanaokuja kutoka Liberia kwa sababu ya magumu wanayopata katika nchi hiyo yenye kusumbuliwa na vita.
◆ Kilele kipya cha Japani katika Septemba kilikuwa 148,452. Walikuwa na mapainia wa kawaida wapya 3,582 waliojiandikisha mwanzoni mwa Septemba. Wakati wa Septemba madarasa ya shule ya painia 165 yaliongozwa katika mizunguko 111, na mapainia wa kawaida 3,920 walifurahia mtaala huo.
◆ Katika Septemba Lesotho ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 1,347. Wastani wa saa 13.1 kwa wahubiri wa kundi huonyesha kwamba wanajitahidi katika utumishi wa Yehova.
◆ Mauritius ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 907 katika Septemba.
◆ Katika Septemba Nigeria ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 146,703. Hilo lilikuwa ongezeko la zaidi ya 4,600 kupita kilele cha Agosti.
◆ Réunion ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 1,854 katika Septemba. Mkusanyiko wao ulihudhuriwa na 3,591, na 114 wakabatizwa.
◆ St. Vincent ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 208 katika Septemba. Hilo lilikuwa ongezeko la asilimia 14. Wahubiri wa kundi walikuwa na wastani wa saa 14.2.
◆ Katika Tanzania programu ya Siku ya Kusanyiko la Pekee iliyokamilishwa hivi karibuni ilihudhuriwa na 5,707 na 115 wakabatizwa.