Habari za Kitheokrasi
◆ Kilele kipya cha wahubiri cha Japani kwa ajili ya Septemba kilikuwa 138,975. Hesabu ya mapainia wa kawaida iliongezeka kwa karibu 2,200 kuzidi kilele kilichotangulia katika Agosti. Mizunguko mitano mipya imeanzishwa katika mwaka mpya wa utumishi. Katika Septemba, madarasa 128 ya Shule ya Utumishi wa Painia yalifanywa katika mizunguko 99, na jumla ya mapainia wa kawaida 3,068 walipitia mtaala huu.
◆ Papua New Guinea ilikuwa na ongezeko la asilimia 9 katika Septemba na kilele kipya cha wahubiri 2,272 wakiripoti.
◆ Sri Lanka ilikuwa na kilele kipya cha wahubiri 1,249 wakiripoti katika Septemba.