Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/91 kur. 1-2
  • Uwe Mwenye Subira na Kufanya Huduma Kikamili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Mwenye Subira na Kufanya Huduma Kikamili
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KATIKA MAENEO MBALIMBALI
  • KUTOA BROSHUA
  • Toa Broshua Ili Ushiriki Tumaini Lako la Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Kutumia Broshua kwa Matokeo Katika Julai
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Tumia Broshua Mbalimbali Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 7/91 kur. 1-2

Uwe Mwenye Subira na Kufanya Huduma Kikamili

1 Mtume Paulo aliendelea kujiona sana kuwa na daraka mbele za Yehova la kuwa mwenye subira na ukamilifu alipokuwa akihubiri habari njema kwa wote ambao wangesikia. Aliwaambia kwa uhakika hivi waangalizi waliokusanyika kutoka Efeso: “Siyahesabu maisha yangu kuwa kitu cha thamani kwangu kama kuumaliza mwendo wangu na huduma ile niliyopokea kwa Bwana Yesu, kuishuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.” (Mdo. 20:24) Je! sisi twahisi sharti lililowekwa juu yetu tufanye ivyo hivyo?—1 Kor. 9:16.

KATIKA MAENEO MBALIMBALI

2 Subira inahitajiwa hasa eneo letu linapofanyiwa kazi mara nyingi sana. Eneo lijapokuwa dogo, twapaswa kusukumwa tuzuru tena na tena. Tujitahidi kuzungumza na wakaaji wote katika kila nyumba, na kuendelea kusaidia watu wanyoofu wathamini tumaini lenye msingi wa Biblia la Ufalme wa Mungu.

3 Wakati wa Julai na Agosti tutakaza fikira kwenye maeneo yanayofanyiwa kazi mara chache na yale yaliyo peke yayo. Katika sehemu hizo watu wengi hawajapata kupokea ushahidi. Hivyo chukua wakati uongee na wenye nyumba. Sikiliza maelezo yao juu ya Kichwa cha Mazungumzo au mambo yanayowapendeza. Uwe chonjo kurekebisha mahubiri yako inapohitajiwa. Saidia wenye nyumba kwa subira wajifunze jinsi ya kutambua dini ya kweli na yale ambayo lazima wafanye ili wapate kibali cha Mungu. Kutoa ushahidi kikamili katika maeneo yanayofanyiwa kazi mara chache na yale yaliyo peke yayo kutasaidia wengi zaidi wampate Yehova kabla haijawa kuchelewa mno.

4 Huenda kukawa na pindi ambapo twazuru watu ambao, ingawa wanadhihirisha kadiri fulani ya kupendezwa, hawakubali fasihi yetu. Twapaswa kuitikiaje? Jitihada yetu ya kutoa ushahidi kikamili itatusukuma tuendelee kusitawisha kupendezwa huko. Kusitawisha kile ambacho kimepandwa mioyoni mwao huenda kukawasukuma hatimaye wakubali funzo la Biblia. Ndugu mmoja alizuru mwenye nyumba mmoja mwenye kupendezwa kwa majuma matano mfululizo bila kuangusha fasihi. Katika ziara ya sita, mwenye nyumba huyo alikubali fasihi, na hatimaye funzo la Biblia likaanzishwa.

KUTOA BROSHUA

5 Wakati wa Julai na Agosti, Kichwa cha Mazungumzo chetu kitakuwa “Dini Inayompendeza Mungu.” Kichwa hicho ni chenye kubadilikana vya kutosha kuweza kutumiwa wakati wa kutoa broshua yoyote kati ya zifuatazo: Furahia Milele Maisha Duniani!, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, na Serikali Itakayoleta Paradiso. Tukichukua wakati kufahamiana na broshua hizo, tutapata mambo kadhaa yafaayo ya kuzungumzia ya kutumiwa pamoja na Kichwa cha Mazungumzo.

6 Kwa mfano, tungeweza kujijulisha kisha tuseme hivi: “Watu wengi leo wana wasiwasi na wamevurugika kuona dini nyingi sana na zenye kupingana. Ndivyo na wewe, sivyo? Wengine wamesema kwamba dini mbalimbali ni barabara tofauti tu zinazoongoza mahali pale pale pamoja pa wokovu. Je! hayo ndiyo maoni aliyokuwa nayo Yesu Kristo? Angalia maneno yake kwenye Mathayo 7:13, 14: (Soma.) Kwa hiyo Yesu hakufundisha kwamba dini zote zinakubalika kwa Mungu. Basi tunaweza kuhakikishaje tuko kwenye ile njia nyembamba inayoongoza kwenye wokovu na kwamba tunamwabudu Mungu katika njia inayokubalika Kwake? Biblia inaonyesha hapa kwenye Waefeso 4:5, 13 kwamba takwa moja ni umoja kati ya waabudu. (Soma.) Kwa wazi, kwapaswa kuwe amani wala si migawanyiko wala vita kati ya wale walio na dini inayompendeza Mungu. Angalia pia katika mstari wa 13 umaana wa kuwa na maarifa sahihi ya Mwana wa Mungu. Hilo linataka kupata kujua ambayo Biblia inafundisha juu ya Yesu na uhusiano wake pamoja na Mungu. Ndiyo sababu tunatia watu moyo wajifunze Biblia. Takwa moja la mwisho ambalo tungependa kutaja wakati huu ni kwamba ili kuwa na dini inayompendeza Mungu ni lazima mtu aishi kulingana na viwango vya adili vya juu vya Biblia kama inavyoonyeshwa kwenye Tito 1:16 (Soma. Toa mfano mmoja au miwili kama vile kuhusu haki au maadili katika ngono.)” Halafu tungeweza kumtia moyo mwenye nyumba asome mojawapo broshua. Ikiwa tunatumia broshua “Tazama!”, tungeweza kuteua jambo moja miongoni mwa mengi katika mafungu 52 hadi 55. Tutoapo broshua Serikali, tungeweza kukazia yanayotaarifiwa kwenye ukurasa wa 30. Picha ya 53 hadi ya 56 katika broshua Maisha Duniani zavutia sana na zafaana sana na Kichwa cha Mazungumzo.

7 Kueneza eneo letu na habari njema kwa subira na kikamili kutatokeza wokovu kwa wale watakaotusikiliza. (1 Tim. 4:16) Wakati unaisha haraka! kwa hiyo, na tutumie subira na kutoa ushahidi kikamili tuwapo na ushiriki kamili katika kuhubiri ujumbe huu wa wokovu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki