Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/91 uku. 4
  • Kutoa Habari Njema—Kwa Utambuzi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa Habari Njema—Kwa Utambuzi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUSHUGHULIKA NA VIZUIA MAZUNGUMZO
  • KUITIKA NIA YA MTU
  • Kutangaza Habari Njema Kwa Kutumia Ufahamu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Jinsi ya Kumjibu Mtu Anayekataa Mazungumzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Kutangaza Habari Njema Kwa Kuzungumza na Watu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Elekeza Moyo Wako Kwenye Ufahamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 7/91 uku. 4

Kutoa Habari Njema—Kwa Utambuzi

1 Mithali moja iliyopuliziwa na Mungu husema: “Ashikaye ufahamu [utambuzi, NW] atapata mema.” (Mit. 19:8) Hekima ya maneno hayo imethibitika mara nyingi kuwa kweli katika utendaji wetu wa kuhubiri. Kwa mfano, kwa kutumia utambuzi na busara, wahubiri wengi wamegeuza vizuia mazungumzo kuwa fursa za kutoa ushahidi zaidi. Au angalau wameweka msingi ili ushahidi utolewe wakati wa baadaye. Hilo laweza kufanywaje?

KUSHUGHULIKA NA VIZUIA MAZUNGUMZO

2 Mara nyingi tunapata watu ambao husema, “Nina shughuli.” Je! kwa kweli mwenye nyumba ana shughuli nyingi, au je! anasema hivyo ili asihusishwe katika mazungumzo marefu? Utambuzi watakwa. Ikiwa haonekani kuwa na shughuli kikweli, tungeweza kujaribu kushinda kizuia mazungumzo hicho. Tungeweza kusema, “Basi nitasema kwa ufupi.” Baada ya hapo, tungeweza kusema kwa muhtasari tuliyokusudia kuzungumza, tukikumbuka maafikiano ya kusema kwa ufupi. Kama tokeo la kumfikiria na maelezo yenye kuamsha kupendezwa, huenda mtu huyo hata akaonyesha tamaa ya kuendelea na mazungumzo papo hapo.

3 Vipi kama kwa kweli yule unayeendea ana shughuli. Ijapokuwa hatutaki kuondoshwa kwa urahisi, tukisisitiza au kukazana, huenda tukaacha wazo lisilofaa. Mwenye nyumba akija mlangoni akiwa na vyombo vya upishi mikononi nasi tunuse harufu ya chakula kinachotayarishwa, yaelekea sana kwa kweli ana shuhuguli. Hivyo utambuzi na uamuzi mzuri vyahitajiwa. Haingeonyesha kumfikiria tukiendelea na mazungumzo wakati huo. Ingekuwa afadhali kama nini kumpa mwenye nyumba trakti na kudokeza urudi baadaye. Hilo litaacha wazo lifaalo zaidi, na ushahidi mzuri huenda ukatolewa wakati mwingine Shahidi azurupo.

KUITIKA NIA YA MTU

4 Pindi fulani twapata watu mmoja mmoja wanaokatiza mara moja bila uungwana tunapowatembelea katika huduma ya nyumba kwa nyumba. Twapaswa kufanya nini ikitukia hivyo? Mithali 17:27 hushauri hivi: “Mwenye roho ya utulivu ana busara [utambuzi, NW].” Ni shauri zuri kama nini! Sauti pole yenye kuonyesha kuhangaikia mara nyingi humtuliza mtu kama huyo. Zaidi ya hilo, tukiweza kwa busara kumfanya ajieleze juu ya suala ambalo lamhangaisha, huenda akapunguza hali yake ya kuteta. Hata akikatisha mazungumzo, pengine jibu letu pole litamwacha akiwa na hali ya akili ifaayo zaidi kuelekea kazi ya Mashahidi wa Yehova. Hilo lingekuwa jambo zuri lililotimizwa. Bila shaka, mwenye nyumba akiudhika na kukasirika, ingekuwa afadhali kuondoka kwa utulivu na labda kujaribu kumtolea ushahidi wakati mwingine.

5 Halafu kuna watu ambao, wajapokuwa wenye ubishi, huenda wakawa wenye moyo mweupe. Katika hali hizo, lingeweza kuwa jaribu kweli kweli la subira yetu kuendeleza mazungumzo pamoja nao. Lakini tukiwa wenye kutambua, kwa lazima, hatutakata maneno kwamba mwenye nyumba hapendezwi kwa sababu tu anajieleza kwa uthabiti juu ya maoni tofauti. Huenda tukataka kuuliza maswali ya busara katika jitihada ya kujua kwa nini yeye anaamini hivyo kisha tumwonyeshe yale ambayo Biblia husema juu ya habari hiyo. (Mit. 20:5) Ikitegemea itikio lake, twaweza kuamua kama lingekuwa jambo lenye manufaa kuendelea na mazungumzo.

6 Mhubiri mwenye utambuzi ajua kwamba mara nyingi wakati na hali hubadili maoni ya mwenye nyumba kuelekea ujumbe wa Ufalme. Itikio lake huenda likawa tofauti kabisa tuzurupo wakati mwingine. Ni lazima tuwe waangalifu tusidhani kwamba tutapata itikio lisilofaa kwa sababu ya njia ambayo mwenye nyumba aliitikia wakati uliopita tulipozuru mlangoni pake.

7 Kuamua kama twapaswa kufuatia mazungumzo si rahisi. Hata hivyo, kwa kusitawisha ustadi wa kufundisha, tutakuwa wenye mafanikio zaidi katika kutoa habari njema kwa utambuzi, huku tukimtegemea Yehova abariki jitihada zetu.—1 Kor. 3:6; Tito 1:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki