Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/91 uku. 1
  • Kutwaa Daraka Letu Tufanye Mema kwa Wengine

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutwaa Daraka Letu Tufanye Mema kwa Wengine
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Habari Zinazolingana
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Njia za Kupanua Huduma Yako
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Je, Tutaufanya Tena?—Mwito Mwingine wa Mapainia-Wasaidizi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 9/91 uku. 1

Kutwaa Daraka Letu Tufanye Mema kwa Wengine

1 Mtume Paulo aliwashauri kwa upole Wakristo wa karne ya kwanza hivi: “Msisahau kutenda mema na kushirikiana [kushiriki vitu na wengine, NW].” (Ebr. 13:16) Jitihada zao za kusaidia ndugu zao hata chini ya hali mbaya zingeongeza nguvu upendo wao kwa Mungu na kwa mmoja na mwenzake. (Yn. 13:35) Sisi pia tunatiwa moyo tufanye mema na kushiriki pamoja na wengine.

2 Ili kutimiza hilo, Yehova amefanya uandalizi kwetu tulishwe kiroho vizuri na kutayarishwa kwa vifaa. Lo! ni habari nyingi kama nini tunayopata katika kila Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ni furaha iliyoje tunayopata kusoma kila toleo upesi iwezekanavyo baada ya kulipokea! Tunapotafakari juu ya habari hiyo ya Kimaandiko, twaweza kuandika mambo ya kutumia katika huduma ya shambani na katika mazungumzo yetu na wengine. Vivyo hivyo, twaweza kukomboa wakati kutayarisha kila mkutano na hasa funzo la kila juma la Mnara wa Mlinzi. Funzo la kibinafsi la Neno la Mungu hutusaidia kusitawisha “nia ya Kristo” na kutuwezesha kushiriki yanayopendeza pamoja na wale tuwapatao.—1 Kor. 2:14-16; Zab. 19:14.

3 Madaraka Yanayostahili Kukubali- wa: Wote wanaopata kumpenda Yehova huweka maisha zao wakfu kwake. Kwa kukubali madaraka yanayoshirikishwa na wakfu, twaonyesha kwamba sisi tuko upande wa Yehova na tumejitenga wenyewe na ulimwengu wa Shetani na njia zao zenye kuchukiza. Kwa kufuata kiolezo alichoacha Kristo Yesu, twawekea wengine kielelezo chema. (1 Pet. 2:21) Programu za kusanyiko la mzunguko kama ile iliyopangiwa mwaka wa utumishi wa 1992, yenye kichwa “Kuchukua Furushi Letu Wenyewe la Daraka,” hututia moyo tuishi kupatana na wakfu wetu.

4 Kuhudhuria mikutano ya kundi kwa ukawaida hutupa nafasi ya kushiriki kujenga mawazo ya mmoja na mwenzake. Funzo letu la kibinafsi na kujitayarishia mikutano hutuandalia habari nyingi ambayo twaweza kushiriki na wengine. Kuonyesha kupendezwa kibinafsi hivyo na wengine huendeleza roho ya uchangamfu na ya kirafiki kama ya familia. Kwa kuchangia mikutano, sisi twaonyesha kwamba twakubaliana kikweli na maneno ya Paulo yaliyoandikwa kwenye Waebrania 10:24, 25 na kukubali daraka letu la kutia wengine moyo.

5 Jitahidi Kufikia Madaraka Zaidi: Wakati wa mwaka wa utumishi wa 1992, je, sisi twaweza kujitahidi kufikia madaraka zaidi, kama vile utumishi wa painia msaidizi au wa kawaida? Badala ya kukazia isivyostahili takwa la saa, kwa nini tusikaze fikira zetu juu ya kuongeza fursa za kushiriki kazi ya kukusanya? (Yn. 4:35, 36) Kufanya kazi kwa ukawaida na wahubiri wengine wenye ujuzi na mapainia kutatusaidia kufanyia maendeleo stadi zetu katika huduma. Hesabu iliyoongezeka ya mapainia wasaidizi hutumika pia kuwa kichocheo chenye kuleta usitawi katika kundi. Ikiwezekana, kwa nini usijaze fomu ya ombi la kuwa painia wa kawaida au upange kuwa painia msaidizi kwa ukawaida au mara nyingi kadiri iwezekanavyo katika mwaka huu?

6 Madaraka yanatolewa kwa urahisi kwa washiriki wanaume wa kundi wanaostahili walio wakfu na kubatizwa. (1 Tim. 3:1-10, 12, 13) Wote wanaweza kuonyesha nia yao ya kutumika kwa maelezo yao yaliyofikiriwa vizuri kwenye mikutano, kushiriki katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, na kukubali migawo ya kutoa wonyesho au kushugulikia sehemu nyinginezo katika Mkutano wa Utumishi. Hata watoto waweza kuwa kielelezo chema katika njia hizo katika mwenendo wao kwenye Jumba la Ufalme. Wanaweza kuwa wenye kusaidia katika kufanya kazi pamoja na kikundi chao cha funzo la kitabu kinapopewa mgawo wa kusafisha Jumba la Ufalme au kushughulikia mahitaji mengine kama hayo.—km-SW 4/76 uku. 1.

7 Yesu alionyesha nia yake ya kukubali daraka la kufanya mema kwa wengine kwa maneno haya: “Nataka.” (Luka 5:12, 13) Tukifuata kielelezo chake, sisi vilevile twaweza kutia moyo na kusaidia ndugu zetu, wenye kupendezwa, na watu wenye moyo mweupe tunaopata katika utumishi wa shambani washirikiane kwa ukawaida na tengenezo la Yehova. Kukubali daraka “tuwatendee watu wote mema” kwataka jitihada yenye kuazimia na pengine kujidhabihu kibinafsi kwa upande wetu. (Gal. 6:10) Lakini wakati tunapoona mema yanayotimizwa, twaweza kukubaliana na Paulo, aliyesema hivi: “Sadaka [dhabihu, NW] kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu.”—Ebr. 13:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki