Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/92 kur. 7-8
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Habari Njema Kwa Kutumia Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Chochea Wengine Wamtazame Yesu Kwa Mkazo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Alika Wengine Wamfuate Yule Mtu Mkuu Zaidi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Kitabu Kipya Chawasisimua Mamilioni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 11/92 kur. 7-8

Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi

1 Tulipopokea kitabu hicho kipya, tulisisimuliwa na kichwa chacho, Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Kutambua mtu mmoja kuwa ndiye mkuu zaidi kungemaanisha kwamba yeye anapita kwa ubora mabilioni yote ya wanadamu ambao wamepata kuishi duniani. “-kuu” hufasiliwa kuwa “bora zaidi katika namna au sifa.” Mtu anayestahili kupewa sifa hiyo lazima awe wa kutokeza kwelikweli!

2 Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, anastahili kabisa kutambuliwa hivyo. Yale aliyotimiza duniani hayakuhusiana na utajiri, matimizo ya kimwili, au utawala wa kisiasa. Alikuwa na malezi sahili na akatumia sehemu kubwa ya maisha yake bila kujulikana. Hata hivyo, alipokuwa mwenye miaka 30, alianza kuvuta uangalifu wa wote katika bara la Palestina kwa yale aliyosema na kufanya. Alifunua utu na makusudi ya Yehova Mungu kwa njia isiyopata kuonwa kamwe na mwanadamu. Alitimiza kazi ya kuhubiri iliyo kubwa zaidi isiyopata kufanywa na mwanadamu mmoja, akafanya miujiza yenye kutokeza, na akaweka msingi wa jamii ya ulimwengu mpya.

3 Uhitaji wa Kitabu Hicho: Paulo alituhimiza ‘tumtazame Yesu kwa mkazo sana’ akiwa kielelezo na kiolezo cha maisha yetu. (Ebr. 12:2, NW) Kuanzia 1985 hadi 1991, Sosaiti ilitangaza katika Mnara wa Mlinzi mfululizo wa makala 149 juu ya maisha na huduma ya Yesu. Makala hizo zilitufanya sote tukatambua kwa uwazi zaidi yale ambayo Yesu alisema na kufanya kwa ajili yetu. Zilikazia uhitaji wetu kuiga mfano wake. Habari hizo zote zimewekwa pamoja na kufanywa zipatikane kwetu katika kitabu. Ni kifaa kizuri jinsi gani cha kusaidia wengine wamtazame Yesu kwa mkazo na kuwa raia za yule ambaye Yehova ameweka “juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani”!—Efe. 1:21.

4 Mambo Yenye Kutokeza: Unapotoa kitabu hicho, huenda ukauliza: “Ni nini kilichomfanya Yesu kuwa yule mtu mkuu zaidi ulimwenguni?” Ungeweza kujibu hilo kwa kuelekeza kwenye sura chache kati ya zile 133 zinazokazia maisha yake, utu wake, mafundisho yake, na kazi zake. Sura ya 24 inaeleza kusudi lake la kuja duniani. Sura ya 35 inapitia Mahubiri ya Mlimani yaliyo maarufu. Sura ya 43 inakazia uwezo wa Yesu wenye kutokeza wa kufundisha wengine kwa vielezi. Sura ya 133 inatoa mwono mdogo wa baraka zitakazofurahiwa na ainabinadamu atakapokamilisha kazi yake. Huenda ukaona utumizi wa maswali mwishoni mwa kila sura kuwa wenye msaada katika kuchochea mazungumzo; marejezo ya maandiko yaliyotajwa yanaonyesha mahali ambapo simulizi hilo laweza kupatikana katika Biblia. Unaweza kutaja juu ya vielezi vyenye kutokeza vinavyofunua uwezo wa utu wa Yesu, kina cha huruma yake kwa wengine, na bidii yake nyingi katika kuhubiri.—Ona sura 44, 95, 117, na 123.

5 Tutatoa kitabu hicho kipya wakati wa Desemba. Sehemu zacho zisizo na kifani zinatupatia sababu nzuri za kukipendekeza na kukitoa kwa wengine kwa idili nyingi. Kila mtu anayetaka uhai wa milele ni lazima atwae maarifa juu ya Yesu Kristo. (Yn. 17:3) Jitihada zetu nyingi za kugawanya kitabu hicho zitawezesha maisha za watu wengi wenye mioyo myeupe kuguswa na yule mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki