Habari Za Kitheokrasi
Ethiopia: Serikali ya Ethiopia imewatambua rasmi Mashahidi wa Yehova kuwa shirika lililosajiliwa. Akina ndugu wanafurahia kupata utambulisho wa kisheria na kusonga mbele na kazi ya Ufalme. Fasihi inapokewa, na mikusanyiko inafanywa.
Ghana: Kusimamishwa kwa kazi yetu katika nchi hii sasa kumeondolewa. Hilo limeletea ndugu zetu shangwe kuu, kwa kuwa Majumba ya Ufalme yao sasa yamefunguliwa tena na ruhusa imetolewa ya kuomba kuweza kusajiliwa chini ya sheria iliyopo.
Liberia: Baada ya miezi mingi ya kufungwa kwa ofisi ya tawi ya Liberia kwa sababu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe huko, tawi hilo limefunguliwa tena. Wamishonari wanne sasa wamerudi kutumikia katika tawi hilo, na akina ndugu wanafurahia kuweza kushirikiana pamoja tena kwa uhuru.