Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei
Juma Linaloanza Mei 4
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Watie moyo wahubiri washiriki katika utumishi mwisho-juma huu.
Dak. 20: “Kutoa Mnara wa Mlinzi Katika Mei.” Makala ipitiwe kwa maswali na majibu. Tia ndani mazungumzo ya kusudi la Mnara wa Mlinzi kama inavyoonyeshwa kwenye sehemu ya juu ya ukurasa wa 2 wa kila toleo. Utoaji wa ziada unaweza kudokezwa, ukitegemea magazeti yatakayotumiwa kwenye utumishi wa shambani juma hili.
Dak. 15: “Utangulizi Unaweza Kutokeza Hali Tofauti.” Zungumzia makala pamoja na wasikilizaji. Je! wamejaribu kutumia baadhi ya matangulizi yaliyodokezwa katika matoleo ya hivi karibuni ya Huduma ya Ufalme Yetu, mengi yayo yakiwa yametolewa kwenye kitabu Kutoa Sababu? Ni matangulizi gani ambayo wamepata kuwa yenye matokeo zaidi katika eneo la kwenu? Wahubiri hujitayarisha na kujizoeza lini matangulizi yao kwa ajili ya utumishi wa shambani? Uwe na maonyesho mawili au matatu mafupi ya matangulizi ambayo yamekuwa na matokeo katika eneo lenu.
Wimbo 32 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu.
Dak. 20: “Fanya Ziara za Kurudia Zenye Matokeo.” Zungumza pamoja na wasikilizaji mambo makuu katika makala, labda ukitia ndani ono fupi la hivi karibuni ambapo ziara ya kurudia ilichochea kupendezwa zaidi. Tumia dakika za mwisho sita hadi nane kuonyesha jinsi kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kundi anavyosaidia wahubiri wawili au watatu wajitayarishe kurudia watu waliopendezwa waliowapata hivi karibuni katika eneo lenu. Iwapo inawezekana, tumia ziara za kurudia hususa ambazo wahubiri hao watafanya baadaye.
Dak. 15: “Je! Unatoa Mafunzo ya Biblia?” Maswali na majibu na wonyesho. Pangia wonyesho wa dakika 5 kuonyesha jinsi funzo linavyoweza kuongozwa kwa trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani kwa kutumia habari iliyo chini ya kichwa kidogo “Uzima Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu.”
Wimbo 65 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu, kutia ndani ripoti ya hesabu na shukrani kwa upaji. Pongeza kundi kwa utegemezo wa kifedha kwa kundi lenu na pia kwa kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote.
Dak. 20: “Tia Moyo Ufuatiaji wa Miradi ya Kiroho.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiongozwa na mzee. Baada ya kuzungumzia fungu la 6, mhoji mhubiri aliye mfano mzuri ambaye akiwa kijana aliitikia kitia-moyo cha kufikia miradi ya kiroho. Yeye alitiwaje moyo? Unaposhughulikia fungu la 7, taja faida halisi ambazo wazazi na vijana watapata kwa kupitia sura 22, 38, na 39 za kitabu Vijana Wanauliza.
Dak. 15: “Soma Upanue Mipaka ya Maarifa Yako.” Ishugulikiwe na mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Hotuba ikitegemea Amkeni!, Aprili 8, 1992, (Julai 22, 1991, kurasa 25-7, Kiingereza) inayokazia uhitaji wa kuwa wasomaji bora zaidi. Saidia wasikilizaji waelewe kwamba kuweza tu kusoma kama maji hakutoshi; ni lazima tukuze uwezo mzuri wa kufahamu.
Wimbo 213 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Mei 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Mambo yaliyoonwa kutokana na kampeni ya uandikishaji (hayo yapaswa yatayarishwe mapema kwa msaada wa ndugu anayeshughulikia maandikisho kundini).
Dak. 15: Jilinde Mwenyewe Dhidi ya Uasi-Imani. Mazungumzo kati ya mzee na mhubiri wakiwa wamekaa mezani. Mhubiri aeleza kwamba alikutana na mtu kwenye utumishi ambaye amekuwa akisoma fasihi ya waasi-imani. Mhubiri amwambia mzee kwamba anahisi mwenye nyumba alikuwa na moyo mweupe kwa maswali aliyouliza. Mhubiri alikataa toleo la mwenye nyumba la kichapo cha waasi-imani lakini angependa kujaribu kujibu maswali ya mwenye nyumba. Mzee ampongeza mhubiri kwa mwelekeo wake na matendo yake mazuri. Badala ya kuzungumzia yale ambayo waasi-imani wameandika au kusema, ni jambo la hekima kukazia fikira kwenye maoni ya Maandiko kuhusu mambo mbalimbali kama yanavyoonyeshwa katika kitabu Kutoa Sababu. Mzee amwomba mhubiri afungue kitabu chake Kutoa Sababu, na pamoja wanapitia kurasa 317-21. Mazungumzo yapasa yawe yenye uchangamfu na kitia-moyo wanapozungumzia fasili ya uasi-imani, kila kichwa kidogo chenye maandishi thabiti, na maandiko makuu yaliyochaguliwa kadiri wakati uruhusuvyo. Malizia mazungumzo kwa maelezo chanya kuhusu habari yote yenye kujenga na kutia moyo inayopatikana kwetu tuweze kujifunza. Shiriki ujumbe wenye kujenga pamoja na mwenye nyumba. Ikiwa yeye ana moyo mweupe, ataona tofauti kati ya mfikio chanya wa kweli, na mfikio hasi wenye kuchambua wa waasi-imani. Kwa kukataa mawazo na habari za waasi-imani, tunaonyesha uaminifu-mshikamanifu wetu kwa Yehova na tengenezo lake lionekanalo.
Dak. 20: “Chakula cha Kiroho cha Kila Siku—Cha Lazima kwa Familia ya Kikristo.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu.
Wimbo 108 na sala ya kumalizia.