Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/92 kur. 5-6
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 8/92 kur. 5-6

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Pitio vitabu vikiwa vimefungwa la habari iliyozungumziwa katika migawo ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kwa majuma ya Mei 4 hadi Agosti 24, 1992. Tumia karatasi tofauti ya kuandika majibu kwa maswali mengi kadiri uwezavyo kwa wakati uliogawiwa.

[Angalia: Wakati wa pitio la kuandika, ni Biblia pekee inayoweza kutumiwa kujibu swali lolote. Marejezo yanayofuata maswali ni kwa ajili ya utafiti wako wa kibinafsi. Nambari za ukurasa na fungu huenda zisipatikane katika marejezo yote kwenye Mnara wa Mlinzi.]

Jibu taarifa zifuatazo Kweli au Si Kweli:

1. Katika usomaji wa peupe, vituo vinavyofaa ni sehemu ya maana ya mkazo. [sg-SW uku. 30 fu. 6]

2. Imetupasa tujifunze kwa kusudi la kuikumbuka habari kwa matumizi ya baadaye, kwamba ni katika maisha zetu wenyewe au katika huduma ya shambani. [sg-SW uku. 36 fu. 10]

3. Kusudi la kutumia msamiati ulioongezeka ni kujionyesha kwa walimwengu kwamba Mashahidi wa Yehova ni watu wenye maarifa na wastadi. [sg-SW uku. 55 fu. 7]

4. Ushuhuda wenye nguvu zaidi wa kuunga mkono asilia ya Kumbukumbu la Torati ni akiolojia (mambo ya kale). [si uku. 37 fu. 8 (chapa 1983 uku. 37 fu. 8)]

5. Hesabu 35:16 isemapo, “Lakini kama alimpiga kwa chombo cha chuma,” inamaanisha kwamba chombo hicho kilitumiwa kimakusudi kuwa silaha. [Usomaji Biblia kila juma; ona g78 12/22 uku. 27.]

6. ‘Aliye mkubwa’ kwenye Kumbukumbu la Torati 1:17 angeonekana kuwa mkubwa kwa sababu ya vitu vya kimwili alivyonavyo, elimu, au mambo makubwa-makubwa ambayo ametimiza. [Usomaji Biblia kila juma; ona w77 uku. 148.]

7. Ni lazima tukate kauli kutokana na Kumbukumbu la Torati 19:21 kwamba adhabu ya kifo kwa uuaji wa kimakusudi ilikuwa sehemu ya sheria ya kimungu. [Usomaji Biblia kila juma; ona g74 7/22 uku. 28.]

8. “Mambo yaliyofunuliwa” kwenye Kumbukumbu la Torati 29:29 yalikuja kuhusisha habari yote iliyorekodiwa ndani ya Biblia. [Usomaji Biblia kila juma; ona w87-SW 5/15 uku. 31.]

9. Yehova alifanya mpango kabila la Yuda ‘limwagize Yakobo katika maamuzi ya kihukumu ya Mungu na Israeli katika sheria ya Mungu.’ (Kum. 33:10) [Usomaji Biblia kila juma; ona w88-SW 8/15 uku. 11 fu. 7.]

10. Wagibeoni walifananisha Mabaki. (Yos. 10:1-11) [Usomaji Biblia kila juma; ona w86-SW 12/15 uku. 22 fu. 8.]

Jibu maswali yafuatayo:

11. Ni tatizo lipi kubwa la kushinda mtu asomapo hati ya hotuba? [sg-SW uku. 31 fu. 9]

12. Kichwa cha hotuba chaweza kuamuliwaje? [sg-SW uku. 44 fu. 2]

13. Ni nini maana ya neno Kumbukumbu la Torati, na kitabu hicho kilihimiza nini? [si uku. 36 fu. 4 (uku. 36 fu. 4)]

14. Ni nini lililokuwa kusudi la Urimu na Thumimu kwenye Kumbukumbu la Torati 33:8? [Usomaji Biblia kila juma; ona w86-SW 1/15 uku. 8.]

15. Ni katika njia gani Sheria ya Mungu ‘ingetumika kama utepe katikati ya macho yako’ kwa Waisraeli? (Kum. 6:8) [Usomaji Biblia kila juma; ona w73 uku. 192.]

16. Maneno ya Yehova yanaweza kututegemezaje? (Kum. 8:2, 3) [Usomaji Biblia kila juma; ona w86-SW 6/1 uku. 30 fu. 15.]

17. Kwa nini sheria ya Mungu katika Kumbukumbu la Torati 22:28, 29 yasema kwamba mwanamume Mwisraeli aliyefanya ngono na bikira asiyeposwa afunge ndoa naye na hangeweza kumtaliki kamwe? [Usomaji Biblia kila juma; ona w89-SW 11/15 uku. 31.]

18. Tunapofikiria yale mataifa ya muungano yaliyokabili Israeli, ni hali gani inayofanana na hiyo tunayoiona leo? (Yos. 9:1, 2) [Usomaji Biblia kila juma; ona w86-SW 12/15 uku. 22 fu. 5.]

19. Badala ya msemo wa kisayansi kuhusu mwendo wa kisayari katika Yoshua 10:13, Yoshua alikusudia kutoa nini? [Usomaji Biblia kila juma; ona w81 10/1 uku. 5.]

20. Sentensi za kwanza za hotuba zapasa kuwa na makusudi gani mawili? [sg-SW uku. 46 fu. 9]

Toa neno au fungu la maneno linalohitajiwa kukamilisha kila ya taarifa zifuatazo:

21. Unapomaliza usomaji wa Biblia, ingefaa kutumia wakati fulani kufanya ikiwa mambo fulani hayako wazi kwako. [sg-SW uku. 35 fu. 7]

22. Unapotayarisha hotuba, yaondoe mambo yasiyohusiana sana na chako. [sg-SW uku. 41 fu. 10]

23. Kwa kufanya kazi nzuri ya kutayarisha kila mgawo katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, tunakubali na mpango huu wa elimu ambao Yehova ameandaa. [sg-SW uku. 43 fu. 18.]

24. ‘Kutwaa nafsi’ kungetokeza kutwaa . (Kum. 24:6) [Usomaji Biblia kila juma; ona w84-SW 11/1 uku. 24.]

25. Biblia hutoa fasili ya katika Hesabu 35:20, 21. [Usomaji Biblia kila juma; ona g74 5/8 uku. 27.]

Chagua jibu sahihi katika kila ya taarifa zifuatazo:

26. Inafaa kuuliza wenye nyumba maswali kwa sababu (huwafanya waelekee zaidi kusikiliza; huwafanya waone kwamba hawajui jibu; huwafanya wafahamu kwamba dini bandia haijawafundisha vizuri). [sg-SW uku. 52 fu. 12]

27. Nyoka ya shaba ilielekezewa (Shetani; Mfalme Daudi; Yesu). (Hes. 21:8, 9) [si uku. 35 fu. 34 (uku. 35 fu. 34)]

28. Petro anukuu kutoka (Mambo ya Walawi; Hesabu; Kumbukumbu la Torati) kwa kukazia hoja yake kwamba Yesu ndiye Kristo na Nabii mkubwa zaidi ya Musa. [si uku. 40 fu. 31 (uku. 40 fu. 31)]

29. Kitabu cha Yoshua chahusisha kipindi cha kuanzia (1513-1473; 1473-c. 1450; 1473-c. 1100) K.W.K. [si uku. 42 fu. 5 (uku. 43 fu. 5)]

30. Kutenda “kwa hekima” kungemaanisha kutenda (kulingana na maarifa yote yaliyopatikana Misri; kwa muono-ndani; kwa njia ya werevu). (Yos. 1:8, NW) [Usomaji Biblia kila juma; ona w89 3/15 uku. 13 fu. 10.]

Linganisha maandiko yafuatayo na taarifa zilizoorodheshwa chini:

Hes. 21:5, 6; 23:23; 32:23; Kum. 12:24; Mt. 28:19, 20

31. Kwa kuangalia maagizo haya, kila Mkristo anahitaji kufanyia maendeleo uwezo wake wa kufundisha. [sg-SW uku. 49 fu. 2.]

32. Kwa kuonya juu ya kunung’unika, Paulo alirejezea andiko hili. [si uku. 35 fu. 36 (uku. 35 fu. 36)]

33. Kwa sababu ya katazo hili, Mashahidi wa Yehova hawaruhusu ile njia ya damu yao wenyewe kuwekwa akibani na baadaye kurudishwa ndani yao. [Usomaji Biblia kila juma; ona w89 3/1 uku. 30.]

34. Kanuni hii ni sawa na ile ya Wagalatia 6:7: “Cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.” [Usomaji Biblia kila juma; ona w72 uku. 392.]

35. Mashahidi wa Yehova hawaogopi uchawi au ulozi wakikataa chochote kinachohusika na uchawi, kutia ndani hirizi au “dawa” iliyotayarishwa na mganga. [Usomaji Biblia kila juma; ona g70 8/22 uku. 7.]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki