Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/93 kur. 3-4
  • Kujifunza Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujifunza Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Funzo la Kitabu la Kutaniko Huchochea Utendaji Wenye Kuelimisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Sehemu ya 1: Daraka la Kiongozi wa Funzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Tutaanza Kujifunza Kitabu Mkaribie Yehova Juma Linaloanza Januari 6
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 7/93 kur. 3-4

Kujifunza Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi

1 Wakati wa juma la Agosti 2, tutaanza kujifunza kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi katika Mafunzo yetu ya Kitabu ya Kutaniko. Itakuwa shangwe kama nini kupitia maisha na huduma ya Yesu Kristo! Kwa kuwa kitabu kimetengenezwa tofauti kidogo na vile vingine ambavyo tumejifunza, miongozo michache itasaidia.

2 Kitabu hicho hakina namba za ukurasa, kwa hiyo ratiba itakayochapishwa kwenye Huduma ya Ufalme Yetu itaorodhesha sura zitakazosomwa, mara nyingi zikiwa tatu au nne kila juma. Sura 35, 111, na 116 ni ndefu zaidi na zitasomwa mara mbili kila mojayazo. Baada ya ndugu anayestahili kusoma sura yote (au sehemu yote chini ya kichwa kidogo, kama katika zile sura 35, 111, na 116), kiongozi wa funzo atauliza maswali mwishoni mwa sura yanayolingana na sura hiyo au sehemu iliyotoka kusomwa. Majibu hayafuatani sikuzote katika sura. Maelezo mafupi na ya moja kwa moja yapaswa kutegemea habari ya somo hilo.

3 Baadaye, wakati ukiruhusu, maandiko yote yaliyotajwa bila manukuu mwishoni mwa sura yanapaswa kusomwa. Maandiko marefu yanaweza kugawanywa katika sehemu ndogo-ndogo ili kuruhusu wahubiri mbalimbali washiriki kusoma, kisha maelezo yanaweza kutolewa juu ya yale yaliyosomwa. Maswali ya moja kwa moja yaliyotayarishwa na kiongozi yatasaidia kutoa maelezo yenye kueleweka ambayo yatasaidia kuonyesha jinsi maandiko yaliyosomwa yanavyohusu mambo yaliyokaziwa katika kitabu. Maswali na maelezo yote yanapaswa kusaidia wanaohudhuria watoe uangalifu kwa Yesu Kristo, mwendo wake wa maisha, na mafundisho yake.

4 Kitabu Mtu Mkuu Zaidi chapitia maisha ya Yesu kwa utaratibu wa orodha ya matukio. Kuyaona akilini matukio na kukaza akilini mwetu mahali yalipotendeka kwaweza kutusaidia kwelikweli kuyakumbuka. Kwa hiyo, hakikisha unafikira vielezo vyenye rangi-rangi na ufanye marejezo ya kila mara kwenye ramani inayoonekana mwanzoni mwa kitabu, kufuatia utangulizi.

5 Utangulizi wa kitabu utafikiriwa katika juma la kwanza. Baada ya kusoma mafungu yote chini ya kichwa kidogo, kiongozi atauliza maswali yanayofaa aliyotayarisha. Funzo hilo la kwanza litawekea msingi mafunzo yatakayofuata wakati wa mwaka ujao. Kadiri ya kufanikiwa katika kujifunza habari hiyo kutategemea kwa kadiri kubwa utayarishaji wa wote wanaohudhuria. Hasa kiongozi anapaswa kujitayarisha vizuri kila juma ili kusaidia kikundi kifahamu vizuri yule mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi, Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki