Habari Za Kitheokrasi
Benin: Ripoti ya Aprili inaonyesha kwamba wahubiri 2,793 waliongoza mafunzo ya Biblia nyumbani yapatayo 4,442 wakafanya ziara za kurudia 30,814. Tarakimu hizo zinaonyesha vilele vipya vitatu.
Bulgaria: Katika mwaka mmoja tu, idadi ya wahubiri imeongezeka kutoka 107 hadi 218 walioripoti katika Machi. Hiyo ilikuwa ongezeko la asilimia 104. Wahubiri walikuwa na wastani wa saa 19.7 katika utumishi wa shambani wakaongoza jumla ya mafunzo ya Biblia nyumbani yapatayo 585. Siku ya kusanyiko la pekee lao la kwanza ilikuwa katika Machi, kukiwa na 900 waliohudhuria.
Chekoslovakia: Kilele kipya cha wahubiri 25,111 waliripoti katika Machi. Hiyo ilikuwa ongezeko la asilimia 9 kupita wastani wa mwaka jana.
Ecuador: Hudhurio la Ukumbusho mwaka huu lilikuwa 99,987. Kukiwa na kilele kipya cha wahubiri 21,734 katika Aprili, ukuzi wenye kuendelea unatazamiwa.
Nicaragua: Vilele vipya vilifikiwa katika karibu kila sehemu ya utumishi wa Ufalme katika Aprili. Hudhurio la Ukumbusho lilikuwa mara tano zaidi ya jumla ya idadi ya wahubiri, iliyofikia 9,629 kwa mwezi huo.
Ujerumani: Katika Machi kulikuwako wahubiri 159,821 walioripoti, hilo likiwa ongezeko la asilimia 3 kupita wastani wa mwaka jana.