Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/92 uku. 8
  • Jinsi ya Kusitawisha Kupendezwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kusitawisha Kupendezwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Ziara za Kurudia Huongoza Kwenye Mafunzo ya Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Jipe Ujasiri wa Kufanya Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kurudi Ili Kuchochea Kupendezwa Katika Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Ziara za Kurudia Sahili na Zenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 11/92 uku. 8

Jinsi ya Kusitawisha Kupendezwa

1 Katika kamusi moja tunajifunza kwamba “kusitawisha” humaanisha kutayarishia au kuchochea ukuzi. Lakini neno hilo pia laweza kumaanisha kufanyiza maendeleo kwa kazi, utunzi, au funzo. Kufanya wanafunzi ni kusudi la maana katika huduma yetu. (Mt. 28:19, 20) Kwa hiyo, tunahitaji kutia jitihada ili kusitawisha kupendezwa tunakopata katika huduma ya shambani.

2 Ziara za mara kwa mara ndizo mara nyingi hutakiwa ili kuchochea ukuzi wa kiroho wa watu mmoja-mmoja wenye mioyo minyoofu. Ziara za kurudia zenye matokeo zapaswa kuongoza kwenye funzo la Biblia la kawaida.

3 Je! wewe huwarudia wale tu wanaoonyesha kupendezwa sana? Hauhitaji kuangusha fasihi ili urudi. Painia mmoja hurudia kila mtu mwenye urafiki. Mazungumzo mazuri ambamo mnashiriki wazo la Kimaandiko yanaandaa msingi mzuri wa kufanya ziara ya kurudia.

4 Tumia Trakti Ili Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Ziara za Kurudia: Habari mbalimbali katika trakti zetu zinafaa kwa siku yetu. Zinakazia uhitaji wa kutwaa maarifa ya Biblia na kuyatumia.

Ungeweza kusema:

◼ “Wakati uliopita tulizungumza kuhusu baadhi ya sababu za kuiamini Biblia. Biblia husema juu ya wakati ujao wa aina gani?” Anza kusoma kuanzia fungu la pili katika ukurasa 3 wa trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani. Soma maandiko. Muulize mwenye nyumba anaonaje yale unayosoma. Malizia kwa kuzungumzia habari chini ya kichwa kidogo “Jinsi Jambo Hilo Linavyowezekana Kwako Wewe” katika ukurasa 4.

5 Kwa njia hiyohiyo, ungeweza kutumia trakti Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa?

Huenda ukasema:

◼ “Kama vile tulivyozungumza kifupi mbeleni, watu wengi huamini kuwako kwa Mungu. Hata hivyo, huenda wasielewe jibu la swali hili, ‘Ikiwa Mungu ni mwenye uwezo hivyo, kwa nini yeye huruhusu watu wafe?’ Trakti hii yaweza kusaidia kujibu swali hilo.” Elekeza fikira kwenye sehemu inayoanzia fungu la nne katika ukurasa 2. Uliza swali linalofaa baada ya kila fungu, na mzungumzie maandiko yaliyotajwa ambayo hayakunukuliwa. Ikiwa kundi lenu sasa lina ugavi wa kijitabu Je! Mungu Anajali?, kingeweza kutumiwa kwa njia hiyohiyo.

6 Kuendeleza Funzo: Kwa kufuata njia zilizodokezwa hapa, unaanzisha funzo la Biblia la nyumbani. Ili kuendeleza mazungumzo kwa ukawaida, muulize mwenye nyumba kwenye umalizio wa ziara yako: “Je umeona kwamba tumejibu maswali ya maana kwa muda wa dakika chache tu? Juma lijalo tungeweza kutumia wakati mwingi zaidi kidogo tukizungumza juu ya tumaini la ufufuo au habari nyingineyo inayokupendeza.” Ungeweza kutumia tu mojawapo maswali yaliyotajwa katika makala hizi au trakti kila unapozuru. Katika wakati ufaao, unaweza kubadilisha mjifunze broshua au uanzishe funzo katika kitabu Kuishi Milele.

7 Inaridhisha kama nini kuongoza funzo la Biblia pamoja na mtu anayetafuta kweli kikweli! Na tubarikiwe kwa huduma yenye matokeo kwa kutumia madokezo yaliyotolewa juu ya jinsi ya kusitawisha kupendezwa tunakopata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki