Habari Za Kitheokrasi
Afrika Mashariki: Katika mikusanyiko 16 ya “Wachukuaji Nuru” kwenye eneo letu, jumla ya 37,185 walihudhuria na 1,237 wakabatizwa. Katika Rwanda, 149 kati ya 182 waliobatizwa walijaza fomu za painia msaidizi mara hiyo.
French Guiana: Ripoti ya Oktoba inaonyesha kilele cha 15 mfululizo cha wahubiri, kukiwa 948 walioripoti. Wahubiri wa kundi walikuwa na wastani wa saa 15.1 katika huduma ya shambani.
Hong Kong: Kilele kipya cha wahubiri 2,704 kilifikiwa katika Oktoba. Ni vema kuona waliongoza mafunzo ya Biblia 4,043.
Jamaika: Jumba la Kusanyiko la kwanza katika Jamaika liliwekwa wakfu Novemba 7, 1992 kukiwa na hudhurio la 4,469.
Madagaska: Mikusanyiko mitano ya Wilaya ya “Wachukuaji Nuru” ilihudhuriwa na 10,694, na 241 wakabatizwa. Hudhurio lilikuwa zaidi ya maradufu ya kilele chao cha wahubiri 4,542.