Kutumia Broshua kwa Matokeo Katika Julai
1 Ili kusogeza upesi kazi ya kufanya wanafunzi, tengenezo limetoa kwa ukarimu vichapo vingi tofauti-tofauti. Miongoni mwa hivyo ni broshua ambazo zinashughulika na vichwa hususa, kama vile makusudi ya Mungu kwa dunia, ule Utatu, Jina la Mungu, serikali ya Ufalme, na kuruhusu kwa Mungu uovu. Tunaweza kutumiaje broshua kwa matokeo ili kusaidia watu katika eneo letu?
2 Ile broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? heulezea kwa kufuatana kwamba ulimwengu mpya usio na kuteseka uko karibu. Tunaweza kuitoleaje utangulizi? Mapendekezo yanaweza kupatikana katika kitabu Kutoa Sababu chini ya kichwa kikuu “Kuteseka,” kuanzia ukurasa wa 131, au huenda ukapendelea utangulizi kwenye ukurasa wa 12 chini ya kichwa “Udhalimu/Kuteseka.”
3 Unaweza kusema:
◼ “Je! umetaka kujua: ‘Je! kweli Mungu anajali udhalimu na kuteseka kwa wanadamu?’” Ruhusu itikio. Soma Zaburi 72:12-14. Kisha fungua ukurasa 22 wa broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? na uzungumzie vichwa vyenye herufi nzito katika sehemu ya 10, pamoja na maana ya kielezi kwenye ukurasa 23. Ikiwa broshua haikubaliwi, kwa nini usitoe trakti, kama vile Faraja kwa Walioshuka Moyo au Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani?
4 Kwa mtu anayesema yeye ni Mkristo tunaweza kurudi kwenye utoaji ufuatao:
◼ “Tunawauliza jirani zetu swali fulani na tungethamini maelezo yako juu yalo. Kwa kuwa Yesu alitufundisha tusali Ufalme wa Mungu uje na mapenzi Yake yafanywe duniani kama mbinguni, je, wewe unafikiri kwamba mapenzi ya Mungu kwelikweli yatafanywa hapa duniani?” Ruhusu jibu, kisha uelekeze uangalifu wa mwenye nyumba kwenye ahadi ya Ufunuo 21:3, 4 kama ipatikanavyo kwenye ukurasa 31 katika broshua Serikali. Unaweza kuendelea na mambo yaliyoonyeshwa kwenye ukurasa 29 wa hiyo broshua. Eleza jinsi serikali ya Ufalme wa Mungu itakavyohakikisha kwamba mapenzi ya Mungu yanafanywa duniani. Mwenye nyumba asipoikubali broshua, unaweza kutoa trakti Je! Ulimwengu Huu Utaokoka?
5 Ikiwa kuna woga wa uhalifu katika eneo lenu, utangulizi unaofuata unaweza kuvutia.
6 Unaweza kusema:
◼ “Watu wengi wanajiuliza, ‘Ikiwa Mungu ni upendo, kwa nini anaruhusu uovu?’ Je! umewahi kujiuliza juu ya hilo pia?” Ruhusu elezo, kisha useme: “Ona kwamba Mithali 19:3 hutahadharisha dhidi ya kumlaumu Mungu kwa mambo mabaya ambayo watu hufanya.” Baada ya kusoma andiko hilo, elekeza uangalifu kwenye ukurasa 15 wa ile broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” na usome fungu la 27. Hilo laweza kuongoza kwenye mazungumzo ya mafungu yanayofuata.
7 Kutumia broshua kufundisha watu wenye mfano wa kondoo kuhusu habari njema ni jambo ambalo sisi sote twaweza kufanya. Kutumia broshua wakati wa Julai na Agosti ni njia nzuri kwa wapya kuanza kushiriki katika huduma yenye maana sana. Vijana, pia, wanaweza kutumia broshua na trakti kwa matokeo katika utumishi wa shambani. Tunaweza kusaidia watu wa namna zote za maisha washirikiane na tengenezo la Mungu. Ni pendeleo letu kushiriki katika utendaji wa kuhubiri tutumiapo kwa matokeo broshua zetu za wakati unaofaa.