“Ufundishaji Wa Kimungu” Mkusanyiko Wa Kimataifa—Nairobi
1 Sisi sote tunatazamia ile ambayo bila shaka itakuwa hatua kubwa katika historia ya kitheokrasi ya watu wa Yehova katika Afrika Mashariki. “Ufundishaji wa Kimungu” Mkusanyiko wa Kimataifa wa 1993/94 katika Nairobi utafika baada ya majuma machache tu. Ni baraka zipi za pekee zinazotungojea?
Wajumbe Kutoka Ng’ambo
2 Kama ilivyotangazwa mwaka jana tunatazamia ofisi za tawi tofauti-tofauti zaidi ya 25 zitume wajumbe kwenye mikusanyiko yote miwili ya kimataifa. Twaamini kwamba jumla ya ndugu zaidi ya 5,000 kutoka ng’ambo watahudhuria mikusanyiko yetu. Itakuwa shangwe iliyoje kushirikiana na wengi sana wenye imani ileile yenye thamani kubwa watokao mbali sana kama vile Japani, Australia, New Zealand, Naijeria, Ulaya, Visiwa vya Bahari ya Hindi, na United States. Itakuwa fursa tukufu kama nini kujionea badilishano la kitia-moyo la kweli!—Rum. 1:12.
3 Zaidi ya wajumbe wa kimataifa tuna furaha ya kutangaza kwamba washiriki watano wa Baraza Linaloongoza wamegawiwa mikusanyiko yetu. Kwa wawili kati ya ndugu hao, J. E. Barr na C. W. Barber, na wake zao, huo utakuwa mara yao ya kwanza kuja Afrika Mashariki. Ndugu W. L. Barry, L. A. Swingle, na Daniel Sydlik pamoja na wake zao watakuwa wakifanya ziara za kurudia eneo letu.
4 Ilikuwa shangwe kupata kujua kwamba twaweza kutazamia ndugu wengine kutoka makao makuu ya Brooklyn na ofisi nyingine za tawi wahudhurie mikusanyiko yetu na kutumikia kwenye programu ya mkusanyiko. Kwa kweli hiyo itakuwa programu ya pekee sana.
Habari ya Programu
5 Tafadhali angalieni kwamba programu ya mikusanyiko yote miwili ya Nairobi itaanza Alhamisi asubuhi. Wimbo wa kufungua umeratibiwa kuanza saa 4:50 za asubuhi. Programu ya muziki waanza saa 4:40 za asubuhi. Kwa hiyo kila mtu atataka kuja mapema Alhamisi asubuhi ili kunufaika kikamili na programu ya siku hiyo. Taarifa hii yahusu mikusanyiko ya Nairobi pekee. Mikusanyiko yote mingine yaanza saa 7:20 Alhamisi alasiri.
6 Mipango imefanya kwa ajili ya programu ya lugha ya ishara kwenye mkusanyiko wa kwanza wa Nairobi, yaani, Desemba 23-26, 1993.
7 Twawatia wote moyo wahudhurie mkusanyiko ambao kutaniko lenu limegawiwa kama ilivyoorodheshwa katika barua KWA MAKUTANIKO YOTE ya Juni 30 na Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1993. Ndugu wapendwa, tafadhali fuateni maagizo hayo kama yalivyoorodheshwa na Sosaiti ili kuhakikisha kwamba kuna vifaa vya kutosha wote kwenye kila mkusanyiko. Twawaomba waangalizi-wasimamizi na waratibu wa mkusanyiko wahakikishe kwamba kutaniko laelewa kwa wazi ni mkusanyiko upi ambao kutaniko lenu limegawiwa. Kila mkusanyiko utakuwa na mambo yaliyotajwa juu na kwa hiyo twawatia moyo tena mshirikiane na mipango hiyo na kuhudhuria mkusanyiko ambao kutaniko lenu limegawiwa.
Vikumbusha
8 Katika kutayarishia mkusanyiko itasaidia kujizoeza nyimbo ambazo zimeonyeshwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba 1993. Pia, tafadhali hakikisheni, hasa wale wanaosafiri katika mwezi wa Desemba, kuripoti kwa kutaniko lenu utendaji wenu wa utumishi wa shambani.
9 Twaomba baraka za Yehova juu ya mipango yote ya mkusanyiko katika eneo letu na twatazamia kwa hamu sana ile mikusanyiko miwili ya kimataifa itakayofanywa Nairobi.