Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/94 uku. 1
  • Uhudhuriaji wa Mikutano—Ni Daraka Zito

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uhudhuriaji wa Mikutano—Ni Daraka Zito
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Tunapaswa Kukutanika Pamoja kwa Ajili ya Ibada?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Tanguliza Uhudhuriaji wa Mikutano kwa Ukawaida
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Mikutano ‘Inayotuchochea Katika Upendo na Matendo Mazuri’
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Hakikisha Unatanguliza Mambo Yanayopasa Kutangulizwa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 1/94 uku. 1

Uhudhuriaji wa Mikutano—Ni Daraka Zito

1 Je! wewe huona kwa uzito kadiri gani uhudhuriaji wa mikutano? Hilo ni swali lenye kugusa moyo, sivyo? Hakuna shaka kwamba wengi wetu twahisi kwamba twathamini mikutano. Hata hivyo, wengine huenda wakafanyiza tabia ya kukosa mikutano fulani. Sababu huenda ikawa ni nini? Je! wengine wetu tunaruhusu kazi isiyo ya lazima ya kuajiriwa, uchovu, masomo ya nyumbani, ugonjwa kidogo wa kimwili, au hali mbaya kidogo ya hewa vikatize jukumu letu la kuhudhuria mikutano kwa ukawaida? (Kum. 31:12) Kwa kuwa hili ni takwa la Kimaandiko, kila mmoja wetu apaswa kutoa ufikirio wa sala kwa swali hili, Mimi nachukuliaje kwa uzito uhudhuriaji wa mikutano?

2 Baadhi ya ndugu zetu hutembea muda wa saa nyingi kupitia barabara zenye vumbi na kuvuka mito iliyojaa mamba ili kuhudhuria mikutano. Katika kutaniko lenu mwenyewe, huenda kukawa kuna waaminifu ambao ‘hawakosi kamwe’ kujapokuwa na matatizo mabaya sana ya kiafya, kasoro za kimwili, kazi nyingi za kuchosha mahali pao pa kuajiriwa, au kazi nyingi ya shuleni. (Lk. 2:37, NW) Kwa nini wanajitahidi sana kuhudhuria? Kwa sababu wanajua kwamba hawawezi kushinda matatizo ya ulimwengu huu uliojawa na mbano kwa nguvu zao wenyewe. Ni lazima wategemee nguvu ambazo Mungu huandaa.—2 Kor. 12:9, 10.

3 Leo, twaiga kiolezo kilichowekwa na Wakristo wa mapema, ambao walikutana kwa ukawaida ili kusali, kushiriki mambo yaliyoonwa, na kujifunza Neno la Mungu. (Mdo. 4:23-30; 11:4-18; Kol. 4:16) Twapokea maagizo juu ya unabii na mafundisho ya Biblia, mwenendo wa kimungu na maadili ya Kikristo, himizo la wakati wake la jinsi ya kutumia vizuri maisha yetu sasa kwa kutumia kwa uangalifu kanuni za Kimaandiko. (1 Tim. 4:8) Pamoja na hayo, twakumbushwa juu ya tumaini letu kwamba siku moja kutakuwa na mwisho wa matatizo na kuteseka. Ni jambo muhimu kwamba tuendelee kuwa na tumaini hilo.—Ebr. 6:19.

4 Je! familia yako inaona kwa uzito kadiri gani uhudhuriaji wa mikutano? Je! ni sehemu ya ratiba yako sawa na wakati wa kula au kazi ya kuajiriwa? Siku za mikutano, je, wewe hujipata ukijiuliza ama uhudhurie au la, au ushirika wa kawaida pamoja na ndugu zako ni wa lazima nyumbani mwako? Wahubiri wengi wakumbuka kielelezo cha wazazi wao walio wakfu walipokuwa wakikua. “Jambo moja kuhusu baba,” mzee mmoja akumbuka kwa upendelevu, “ni kwamba sikuzote alihakikisha kuwa familia imeenda mkutanoni. Kama mtu alikuwa mgonjwa, mmoja wetu alibaki nyumbani pamoja naye, lakini wengine walienda mkutanoni!”

5 Katika makala zitakazofuata za Huduma ya Ufalme Yetu, tutazungumzia thamani ya kila mkutano wa kutaniko kwa kusudi la kusaidia kujenga uthamini wa maandalizi haya ya kiroho. Ikiwa utahudhuria mikutano kwa ukawaida, tuna uhakika kwamba makala hizo zitakusaidia utambue jambo unalokosa. Zitatia ndani vikumbusha kwa wale ambao huongoza mikutano, pamoja na madokezo ambayo sisi sote twaweza kutumia tunapotayarisha na kushiriki kwayo. Kwa nini msiketi mkiwa familia na mtoe sala ya ufikirio kwa mtindo wenu wa uhudhuriaji wa mikutano? Kisha fanyeni marekebisho yoyote ya lazima katika ratiba yenu. Uhudhuriaji wa ukawaida wa mikutano ni sehemu muhimu ya elimu yetu ya kitheokrasi na wapaswa kuchukuliwa kwa uzito kwelikweli.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki