Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/94 uku. 1
  • Kufanyia Kazi Eneo Linalohubiriwa Mara Nyingi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kufanyia Kazi Eneo Linalohubiriwa Mara Nyingi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Matangulizi Yenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Je, Unatumia Kitabu Kutoa Sababu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Sitawisha Utangulizi Wenye Kuchochea
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Matangulizi ya Kuchochea Kupendezwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 1/94 uku. 1

Kufanyia Kazi Eneo Linalohubiriwa Mara Nyingi

1 Twafurahi kupokea ripoti kwamba makutaniko mengi yanafanyia kazi eneo lao mara nyingi. (Mt. 24:14; 1 Tim. 2:3, 4) Ijapokuwa jambo hili hutokeza ugumu wa kipekee, mambo yaliyoonwa yameonyesha kwamba jambo hilo laweza kutimizwa kwa mafanikio ikiwa tumejitayarisha vizuri na kujiandaa ifaavyo tukabiliane na hali mbalimbali zitakazotokea.

2 Matangulizi Yenye Mafanikio Ndiyo Msingi Wenyewe: Ni jambo muhimu kujitayarisha kutumia utangulizi mmoja au mawili yaliyofikiriwa vizuri. Yanapaswa kutia ndani maelezo yafaayo yanayoelewesha wazi sababu hasa za kurudi mara nyingi.

3 Kitabu Kutoa Sababu chatoa vielelezo vingi vya matangulizi yanayofaa ya kutumiwa. Matatu yameorodheshwa kwenye ukurasa wa 15 chini ya kichwa “Katika Eneo Linalohubiriwa Mara Nyingi.” Jizoeze yale ambayo ungependa kutumia katika eneo lako.

4 Wahubiri fulani wanapata mafanikio kwa kutumia mambo yaliyo kwenye magazeti ya kwao ili kuanzisha mazungumzo katika maeneo yanayohubiriwa mara nyingi. Kitabu Kutoa Sababu chatoa vielelezo vitatu vya jinsi hilo laweza kufanywa. Angalia utangulizi wa pili chini ya kichwa “Uhalifu/Kutopatwa na Madhara” kwenye ukurasa wa 13 na matangulizi mawili ya kwanza chini ya kichwa “Matukio ya Sasa” kwenye ukurasa wa 12.

5 Matangulizi Unayotayarisha: Uwe huru kutokeza na kutumia maelezo ya utangulizi kama yale yaliyo katika kitabu Kutoa Sababu. Yaeleze kwa njia yako ya kawaida ukitumia maneno yako mwenyewe. Unaweza kujizoeza pamoja na mhubiri aliye na maarifa kabla ya kuyatumia shambani.

6 Kwa mfano, waweza kusema hivi:

◼ “Tangu tulipokutembelea mara ya mwisho, [taja tukio la karibuni ambalo watu katika jamii wanalizungumzia]. Kwa sababu sisi sote twaathiriwa katika njia moja au nyingine, majirani wetu wengi wameonyesha hangaiko kubwa. Labda hata wewe umelifikiria pia. [Tulia kifupi uruhusu itikio lolote.] Kwa kuangalia hali za ulimwengu leo, je, hutakubaliana na yale ambayo nabii Yeremia aliandika katika sura ya 10, mstari 23?” Baada ya kusoma andiko hilo, jua maoni ya mwenye nyumba, kisha elekeza uangalifu kwenye andiko hususa ambalo laonyesha jinsi Yehova atatatua tatizo hilo hasa mnalozungumzia.

7 Au waweza kusema:

◼ “Bila shaka ulisoma katika gazeti leo [taja tukio hususa katika maeneo ya uhalifu na misiba. Epuka mambo ya kisiasa]. Labda utakubali kwamba hilo latuathiri sisi sote. [Tua kidogo kwa itikio lolote.] Twaweza kutumaini serikali zitoe utatuzi wa muda mfupi; hata hivyo, Biblia huonyesha jinsi tatizo hilo litakavyotatuliwa daima.” Elekeza uangalifu kwa andiko hususa ambalo laeleza jambo ambalo Mungu atafanya.

8 “Mbona Mnatembelea Watu Mara Nyingi Mno?” Maitikio yanayofaa ya vizuia-mazungumzo vinavyotokea yanatolewa katika kitabu Kutoa Sababu kwenye ukurasa wa 20 chini ya kichwa “Mbona Ninyi Mnatembelea Watu Mara Nyingi Mno?” Hata bila kuulizwa, twaweza kutoa ushahidi mzuri tukitumia kila pindi ifaayo kusaidia wengine wathamini kwamba upendo halisi wa Mungu na jirani hutuchochea sisi tuwatembelee mara nyingi iwezekanavyo. Mazungumzo ya maneno ya Yesu kwenye Yohana 21:15-17 yaweza kuthibitika kuwa yenye mafaa kuhusiana na hili.

9 Hadi Yehova aseme imetosha, na twendeleeni kukabiliana na ugumu wa kuhubiri maeneo yahubiriwayo mara nyingi. Tukiwa na azimio hilo, twaweza kuhakikishiwa uongozi, ulinzi na baraka yake hata mwisho.—Mt. 28:19, 20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki