Mikutano Ya Utumishi Kwa Januari
Juma Linaloanza Januari 3
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Taja kifupi mambo hususa katika magazeti ya karibuni ambayo yatawapendeza watu katika eneo la kwenu.
Dak 20: “Uhudhuriaji wa Mikutano—Ni Daraka Zito.” Ipitiwe kwa maswali na majibu. Kwa kupatana na fungu la 2, hoji wahubiri ambao wameshinda vizuizi ili kuhudhuria mikutano kwa ukawaida.
Dak 15: “Kuwasaidia Wengine Wathamini Thamani ya Vichapo Vyetu.” Zungumzia makala hiyo pamoja na kutaniko. Uwe na maonyesho mafupi yakifuata mafungu ya 3 na 4. Julisha wahubiri juu ya vichapo vya kurasa 192 ambavyo kutaniko lina akiba yavyo. Ikiwa kutaniko halina vitabu vya zamani, toa onyesho wa matumizi ya Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu ukifuata mazungumzo ya fungu la 5.
Wimbo 116 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 10
Dak 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yafaayo kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Angalia Habari za Kitheokrasi.
Dak 15: Je! Wewe Uko Tayari Kukabiliana na Hali ya Kitiba Yenye Kujaribu Imani? Hotuba yenye kuchochea ikitolewa na mzee anayestahili ya kusaidia kina ndugu wathamini thamani ya kadi ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia, akitumia mambo makuu kutoka mafungu 1-3 ya nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Novemba 1990. Kwenye Mikusanyiko ya Wilaya ya “Ufundishaji wa Kimungu,” zaidi ya asilimia 50 ya kadi zilizotumiwa kupata kitolewaji kipya zilikuwa hazina sahihi, hazikushuhudiwa, au zilikuwa za zamani. Gawanya kadi mpya kwa wahubiri waliobatizwa pekee, kisha angalia barua ya Oktoba 1, 1991, ya mwelekezo wa kujaza kadi. Washauri kina ndugu WASIJAZE kadi zao usiku huu bali waende nazo nyumbani, wafikirie kwa sala uhitaji wao, kisha wazijaze. Lakini MSITIE SAHIHI kadi wakati huo. Leteni kadi iliyojazwa kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko, ambapo wazee watasaidia kuona kwamba kadi zimetiwa sahihi, kushuhudiwa, na kuwekwa tarehe. Kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko atatumia orodha ya wakati huu kuhakikisha wote katika kikundi chake wamejaza. (Wazazi waliobatizwa waweza kusaidiwa kujaza Kadi za Utambulishi za watoto wao.) Mtu yeyote aliyekosa funzo hilo la kitabu bado aweza kusaidiwa na viongozi wa kitabu/wazee katika Mkutano wa Utumishi utakaofuata hadi wahubiri wote waliobatizwa wawe na kadi zao zilizojazwa vizuri na kutiwa sahihi. Wazee wapaswa kuwa na orodha ya wowote wanaobaki na wajaribu kumaliza kadi zote upesi iwezekanavyo.
Dak 20: “Kurudi Ili Kujenga Uthamini.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Ikiwa wahubiri wanatumia vichapo vya zamani, toa wonyesho wa jinsi ziara ya kurudia yaweza kufanywa kwa mtu aliyekubali kimojapo vitabu hivyo. Ama, toa wonyesho wa ziara ya kurudia kwa mtu ambaye alikubali kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu ukitumia madokezo katika fungu la 5.
Wimbo 154 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 17
Dak 10: Matangazo ya kwenu na ripoti ya hesabu. Tia ndani shukrani za upaji wa hiari. Eleza uthamini kwa utegemezo wa kifedha wa wahubiri wa utendaji wa Sosaiti na wa kutaniko. Kumbusha wowote ambao hawajakamilisha kadi yao ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia wafanye hivyo usiku huu kwa kumfikia kiongozi wao wa Funzo la Kitabu la Kutaniko au mmoja wa wazee wengine.
Dak 20: “Kufanyia Kazi Eneo Linalohubiriwa Mara Nyingi.” Ipitiwe kwa maswali na majibu ikiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Katika makutaniko yaliyo na eneo lenye kuhubiriwa mara nyingi, toa wonyesho wa moja ya matangulizi ya kitabu Kutoa Sababu yaliyorejezewa kwenye mafungu 4 na 5 na pia utangulizi unaofaa ama kwenye mafungu 6 na 7 au mmoja uliotayarishwa hasa kwa ajili ya eneo la kwenu. Katika makutaniko ambayo hayajahubiri eneo lao mara nyingi, matangulizi mengine yenye kustahiki kutoka kitabu Kutoa Sababu yapaswa kutolewa katika maonyesho. Maonyesho yapaswa kutayarishwa kwa kurudiwa.
Dak 15: Wakati Ujao wa Dunia ni Nini? Ikitegemea kitabu Kutoa Sababu, kurasa 78-83. (Dak. 5) Hotuba ikishughulikia mambo makuu chini ya vichwa-vidogo vinavyoanzia kurasa 78 na 79, vikishughulikia hadi habari iliyo katikati ya ukurasa 80. (Dak. 7) Mhubiri mpya na mhubiri aliyekomaa, wazungumzia habari iliyo kwenye ukurasa 80-2. Watu wa ukoo wa kilimwengu wa mhubiri mpya wamebisha kwamba Biblia yaonyesha dunia itaharibiwa. Mhubiri mpya auliza msaada wa mhubiri mwenye ustadi katika kuelewa maandiko ya Biblia juu ya dunia mpya. (Dak. 3) Kwa kumalizia, zungumzia swali lililo kwenye ukurasa 82 “Ni watu wa aina gani ambao Mungu atapendelea kuwapa uzima usio na mwisho duniani?” Tia moyo wote wajitahidi ili kustahili kupata pendeleo hilo.
Wimbo 176 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 24
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Tia moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani juma hili. Tangaza mipango ya kutaniko ya utumishi wa shambani.
Dak 20: “Ufundishaji wa Kimungu Watoa Uchocheo Wenye Nguvu.” Makala ipitiwe kwa maswali na majibu. Soma mafungu na maandiko yaliyowekwa bila manukuu wakati ukiruhusu. Ruhusu maelezo mafupi yanayoeleza uthamini wa binafsi kwa manufaa zilizopokewa kutokana na kuhudhuria mkusanyiko na kutumia vitolewaji vya mkusanyiko.
Dak 15: Utendaji wa Shambani wa Kutaniko. Mwangalizi wa utumishi na mzee mwingine wapitia utendaji wa shambani wa kutaniko wa miezi minne iliyopita. Theluthi moja ya mwaka wa utumishi imepita (Septemba-Desemba). Kutaniko laendeleaje? Toa pongezi la moyo mweupe katika maeneo ambayo kutaniko linafanya vizuri. Pia taja maeneo ambayo kutaniko laweza kufanyia maendeleo, na utoe madokezo yanayofaa. Tia ndani mambo yaliyoonwa mafupi moja au mawili yenye kutia moyo kutoka miezi minne ya kwanza ya mwaka wa utumishi. Malizia kwa hali nzuri, yenye kujenga. Shangwe ya Yesu ilitokana na kutimiza huduma yake. Sisi pia tutapata shangwe kuu kwa kujishughulisha na kazi ambayo Yehova ametupa.—Yn. 4:34; 1 Kor. 15:58.
Wimbo 179 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 31
Dak 5: Matangazo ya kwenu. Watie moyo wote waanze mapema katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu. Waweza kutoa mapendekezo ya msaada ya kutoa magazeti ya karibuni.
Dak 15: Toa Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani Nyumba kwa Nyumba. Hotuba fupi yenye idili juu ya uthibitisho wa thamani ya kitabu katika kusaidia watu wajue jinsi ya kumwabudu Yehova. Toa wonyesho wa jinsi mhubiri anavyoweza kutumia mapendekezo katika toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu kutayarisha kutumia kitabu hiki katika utumishi wa shambani.
Dak 15: Jumba la Ufalme. Hotuba ikitolewa na mzee. Shughulikia mambo makuu kutoka Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu kurasa 61-4. Kazia uhitaji wa kuwa na Jumba la Ufalme ambapo kutaniko halina Jumba la Ufalme. Tia moyo utunzi mzuri wa Jumba la Ufalme mahali ambapo kutaniko lina Jumba la Ufalme. Taja uhitaji kwa wazee kuona kwamba marekebisho ya lazima yanafanywa kila mwaka. Zungumzia mwenendo ufaao katika Jumba la Ufalme na upongeze kina ndugu kwa jitihada zao za kuwa na kutunza Majumba ya Ufalme.
Dak 10: Mahitaji ya kwenu. Au hotuba ikitolewa na mzee juu ya “Uwe na Maoni Yafaayo Juu ya Rehema ya Mungu,” ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 1993, kurasa 22-5.
Wimbo 188 na sala ya kumalizia.