Habari Za Kitheokrasi
Bolivia: Ofisi ya tawi iliripoti kilele kipya cha wahubiri 9,588 katika Oktoba. Pia walifikia vilele vipya katika mafunzo ya Biblia nyumbani, ziara za kurudia, wahubiri wa kutaniko, na mapainia wa kawaida. Wahubiri wa kutaniko walifanya wastani wa muda wa saa 14 katika huduma ya shambani.
India: Katika Oktoba kilele kipya cha wahubiri 13,217 kilifikiwa. Hiki kilikuwa kilele chao cha tatu mfululizo.
Kenya: Kuwekwa Wakfu kwa Majumba ya Ufalme: Nairobi Githurai, Januari 11, 1994, 290 walihudhuria. Katika Banana Hill, Januari 29, 1994, 248 walihudhuria.
Lithuania: Ripoti ya Oktoba yaonyesha kilele kipya cha wahubiri 871, ongezeko la asilimia 39 kupita Oktoba 1992.