Tangaza Ujumbe Wenye Kusisimua Uliomo Katika Ufunuo
1 Kitabu Upeo wa Ufunuo kimetusaidia tuelewe ujumbe wenye kusisimua uliorekodiwa katika kitabu cha Ufunuo. Wasaidie wengine wathamini jinsi ujumbe huu unavyowaathiri kwa kutoa kitabu hiki katika huduma wakati wa Machi. Huenda ukaona madokezo yafuatayo kuwa yenye msaada katika kutayarisha utoaji wako.
2 Baada ya salamu inayofaa, unaweza kusema hivi:
◼ “Je! umepata kusikia juu ya wapanda-farasi wanne wa Apokalipsi? [Ruhusu jibu.] Maoni tofauti yametolewa juu ya kinachofananishwa na wapanda-farasi hao. Lakini je, ulijua kwamba uendeshaji wao wa ufananisho kwa kweli ni sehemu ya unabii wa Biblia unaotabiri matukio ambayo yametukia katika wakati wetu na kwamba sisi sote twahusika katika njia moja au nyingine? [Ruhusu jibu.] Je! ungependezwa kuelewa unabii huu na maana ya utimizo wao kwetu sisi?” Kisha, ungeweza kuonyesha vile vielezi katika sura ya 16 ya kitabu Upeo wa Ufunuo na uunganishe baadhi ya mistari yenye herufi nzito. Au ungeweza kueleza elezo juu ya sehemu fulani ya njozi kwa kutumia trakti Je! Ulimwengu Huu Utaokoka? Toa kitabu na uhakikishe umepanga kurudi ili mzungumze mengi zaidi juu ya njozi hiyo na maana yake.
3 Au labda ungependa kujaribu mfikio huu:
◼ “Umepata kusikia neno ‘Har–Magedoni’? [Ruhusu jibu.] Wengi wamefikiri kwamba neno hilo hurejezea vita ya nyukilia ya uharibifu katika wakati wetu. Kwa kweli, Har–Magedoni ni jambo tofauti kabisa. Kulingana na Biblia, italeta mabadiliko makubwa mazuri, yakitokeza ulimwengu wa amani yenye kudumu.” Waweza kuelekeza kwenye andiko kama vile Ufunuo 16:16 au Zaburi 37:10, 11 kisha kuelekeza uangalifu kwenye sura 39 ya kitabu Upeo wa Ufunuo na baada ya hapo utoe kitabu. Au sivyo, unaweza kuchagua kuzungumzia mambo yanayofaa katika trakti Je! Ulimwengu Huu Utaokoka?
4 Unaweza kutokeza kupendezwa kwa kutumia dokezo hili:
◼ “Wakati huu wa mwaka, watu wengi ulimwenguni pote wanafikiria kifo na ufufuo wa Yesu Kristo. Je! ulipata kujiuliza jambo ambalo amekuwa akifanya tangu ufufuo wake? Matukio mengi yenye kusisimua katika siku yetu yanalingana na daraka la Yesu la wakati huu katika kusudi la Mungu. Baadhi yayo yanasimuliwa katika kitabu cha Ufunuo. Je! ungependa kujifunza zaidi juu ya kusudi la Mungu la kutuma Mwana wake duniani na maana ya jambo hilo kwako na kwa wapendwa wako?” Huenda ukaweza kuelekeza fikira kwenye mafungu 1 na 2 ya sura ya 41 ya kitabu Upeo wa Ufunuo au uonyeshe mambo makuu yafaayo kutoka matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Au huenda ukataka kutumia trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani ili kuchochea kupendezwa.
5 Hakikisha umekaribisha watu wowote waonyeshao kupendezwa wahudhurie Ukumbusho. Kwa baraka ya Yehova, huenda ukaweza kumsaidia mtu ‘asikie maneno ya unabii huu, na kuyashika yaliyoandikwa humo.’—Ufu. 1:3.