Kuwasaidia Wengine Wamheshimu Mfanyi Wetu
1 Je! twahisi kama mtunga-zaburi aliposema: “Ee BWANA, . . . kwako Wewe iko chemichemi ya uzima”? (Zab. 36:5, 9) Twawezaje hata sisi kusaidia wengine wathamini na kumheshimu Yehova kuwa Muumba wetu? Kwa kutoa kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? wakati wa Juni. Kitabu hiki kwa kweli ni chenye kutokeza kwa kuwa hutoa ushuhuda kamili wa kuwapo kwa Mungu na huonyesha waziwazi kwa nini mageuzi hayawezi kuwa ya kweli. Pia hujenga itibari kwa Biblia likiwa Neno la Mungu. Kwa kweli twataka kila mtu ajue jinsi ambavyo uumbaji, wala si mageuzi, unaleta sifa kwa Yehova Mungu.
2 Huu ni utoaji rahisi, na wa moja kwa moja.
Baada ya kumsalimu mwenye nyumba, onyesha picha iliyoko kwenye ukurasa wa 6, na uulize:
◼ “Uhai ulianzaje kwenye dunia hii? Watu fulani husema ni kwa aksidenti tu. Biblia hutoa sifa yote kwa Mungu. Je! wewe wafikirije? [Ruhusu itikio.] Kitabu hiki huandaa majibu yaliyopatana na Biblia na mambo hakika ya kisayansi. Ningependa uwe nacho ili uweze kupitia ushuhuda wote na ujiamulie mwenyewe.”
3 Baada ya kujijulisha, unaweza kusema hivi:
◼ “Katika ulimwengu huu wa ki-siku hizi wa kisayansi, je, ni jambo la busara kuamini katika uumbaji, au wafikiri tulikuja kuwapo kwa nasibu tu? [Ruhusu itikio.] Ona kusababu kwa Biblia juu ya jambo hili. [Soma Waebrania 3:4.] Je! hukubali kwamba kila jengo lina mjenzi? Kwa hiyo, je, ulimwengu mzima ungejitokeza wenyewe?” Onyesha kielelezo kwenye ukurasa 114 wa kitabu Creation, kisha elekeza uangalifu kwa wazo lililoelezwa katika fungu la 2 ukurasa 115. Mwenye nyumba akionyesha kupendezwa na akichukua kitabu, mwambie wakati ujao utakaporudi mtazungumzia swali, Wakati ujao wa mwanadamu na dunia ni nini?
4 Toleo letu la badala mwezi huu ni kitabu “Kuokolewa” katika Kiswahili. Ungeweza kutumia mfikio huu:
◼ “Tunajitahidi kushiriki pamoja na jirani zetu mwono chanya wa wakati ujao. Wengi leo wanahangaikia kuokoka, nao wana sababu nzuri. Mapunguo ya chakula, uchafuzi wa hewa, jeuri, na hali nyinginezo zenye kutisha uhai zimesababisha wengi waogope yale yatakayokuja wakati ujao. Je! mambo haya hukuhangaisha wewe pia? [Ruhusu itikio.] Na bado, kuna tisho la hatari kubwa hata zaidi lililo mbele yetu. Ni nini hilo? Kuokoka ile vita ya Mungu inayokaribia sana. Kwani Biblia hata hututia moyo kwenye Sefania 3:8 tuitazamie vita hii. Ona maneno haya. (Soma) Lazima wewe na mimi tufanye nini ili tuokoke vita ya Mungu na hukumu Yake juu ya waovu? Sefania 2:2, 3 husema kwamba lazima tuyatende maamuzi ya kihukumu ya Mungu na kutenda uadilifu. Tafadhali soma pamoja nami maneno haya yenye kutumainisha. (Soma) Kwa wale wanaoishi kulingana na shauri hilo wakati ujao waweza kuwa mwangavu na wenye tumaini kama mandhari inayoonyeshwa kwenye kurasa 4 na 5 za kitabu hiki.” Unapotoa toleo hili unaweza kutumia habari iliyoko kwenye mafungu ya kwanza-kwanza au pengine mambo fulani kutoka sura za 2 au 4 au sura nyingineyo utakayochagua.
5 Je! watamani kusaidia wengine wajifunze kweli za ajabu juu ya Muumba wetu na kusudi lake lenye upendo kwa viumbe vyake? Kitabu Creation chaweza kukusaidia ufanye hivyo. Hicho humheshimu Muumba wetu Mtukufu, Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, kwa kutukuza kazi zake na kujulisha kusudi lake la ajabu la kutakasa jina lake na kubariki wanadamu kupitia Ufalme wa Kristo.